• ePaper
Saturday, November 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 15, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa
0
MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA
0
SHARES
1
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na SELINA MATHEW,
Dodoma

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameeleza kuhusu ushindani mkubwa uliopitiwa katika mchakato wa uteuzi wa Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba.

Pia, amempa maagizo matatu yenye lengo la kuimarisha zaidi utendaji kazi wa serikali.

Amesema uteuzi wa Dk. Mwigulu, umepitia mchakato mrefu huku akimtaka kiongozi huyo, kusimamia mapato, uwajibikaji kwa watumishi wa umma na kudhibiti makundi.

Hayo aliyasema jijini hapa katika hafla ya kumwapisha Dk. Nchemba, iliyofanyika Ikulu ya Chamwino, Dodoma.

“Dk. Mwigulu uteuzi wako umepitia ushindani mkubwa na katika vigezo kadhaa, umeibuka kuwa na sifa nyingi kidogo kuliko wengine ulioshindana nao.

“Vigezo vyote ulivyopimwa, tumepima maeneo mbalimbali ya kuitumikia nchi hii na taifa hili, kubwa zaidi, kuwatumikia wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” alisema.

Alisema kazi zake na maelekezo yote, yapo katika katiba, lakini amemkabidhi vitabu vinavyoeleza majukumu na mambo yote anayotakiwa kuyaangalia.

“Umepokea kijiti kutoka kwa Waziri Mkuu mstaafu, Kassim Majaliwa, ambaye amefanya kazi nzuri kufanikisha  tunayotamba nayo leo.

“Tukitamba na ujenzi wa shule, vituo vya afya, hospitali za kanda za rufaa, kila tunachotamba nacho leo, yeye alikuwa nyuma yangu kuhakikisha yanakwenda vizuri.

“Kwa hiyo, umepokea kijiti kutoka kwa mfanyakazi mzuri, sina shaka utafuata majukumu yake na kutengeneza pale unapohisi panahitajika kuongezwa nguvu,” alisema.

Alimpongeza na kumtakia kila la kheri katika utekelezaji wa majukumu yake mapya, huku akimtaka kwenda kusimamia utekekezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya 2025-2030.

“Tuna Ilani ya Uchaguzi ya 2025-2030, kuna mengi tumeahidi kuwafanyia wananchi, ukiangalia mambo yote na muda tulionao ni finyu, hivyo hatuna budi kuongeza kasi katika utendaji wetu.

“Wewe utakwenda kusimamia mawaziri ambao nao wanaongoza sekta tofauti, ni wajibu wako kuhakikisha kasi ya utekelezaji wa yale tuliyopanga, inaongezwa tuweze kuyatimiza ndani ya muda mfupi,” alieleza.

Alisema utekelezaji wa kazi hizo zote unahitaji fedha na kwa kuwa ametoka sekta ya fedha kwa muda wa miaka mitano anajua vichochoro vyote vya kutafuta fedha, hivyo amsimamie atakayekaa katika nafasi aliyotoka kupita njia aliyopita ili fedha ipatikane na kazi ifanyike.

“Kwa ufupi una kazi kubwa sana, leo (jana), nitalifungua Bunge la 13 ambapo nitaeleza yote tunayotakiwa kuyafanya ndani ya kipindi hiki cha miaka mitano.

“Kuna ambayo umesema juzi bungeni, naamini hukuyasema tu, una moyo wa dhati kuyasimamia.

“Mzigo huu siyo mdogo na kwa umri wako, vishawishi ni vingi vya marafiki, ndugu, jamaa na wengine, nafasi yako haina rafiki, ndugu wala jamaa ni nafasi ya kulitumikia taifa hili,”alisisitiza Dk. Samia.

Previous Post

NI MARIDHIANO

Next Post

TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

Next Post
TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWINYI ATANGAZA NEEMA KWA VIJANA

DK. MWINYI ATANGAZA NEEMA KWA VIJANA

1 month ago
DK. SAMIA  AELEZA MAFANIKIO YA UONGOZI WAKE

DK. SAMIA AELEZA MAFANIKIO YA UONGOZI WAKE

2 months ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.