Toleo Maalumu

Habari

SAFARI KUMALIZA CHANGAMOTO UMEME IRINGA, DODOMA YAIVA

Na FRED ALFRED, Dodoma  ‎SERIKALI imezindua kituo cha kupoza umeme Mtera, chenye thamani ya sh. bilioni 9.7, kitakacho hudumia Mkoa wa Iringa na wilaya mbili mkoani Dodoma, ambazo zilikabiliwa na changamoto ya kukatika kwa umeme. ‎‎Akizungumza katika uzinduzi wa kituo hicho, Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi alisema kuanza kazi kwa kituo hicho kutasaidia hali ya umeme kutengamaa […]

TANZANIA YAINGIA 10 BORA KUVUTIA UWEKEZAJI AFRIKA

Na ATHNATH MKIRAMWENI TANZANIA imeingia katika orodha ya nchi 10 bora zinazovutia zaidi kwa uwekezaji barani Afrika, ikishika nafasi ya tisa, yakiwa matokeo ya mageuzi makubwa ya kisera yaliyofanywa na serikali chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan. Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo, katika  […]

DK. SAMIA AMREJESHA MAKONDA AFCON

Na NASRA KITANA RAIS Dk.Samia Suluhu Hassan, amempa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, maagizo matatu kuhusu Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON), 2027, ambayo anapaswa kujifunza Morocco. Miongoni mwa maagizo hayo ni kujifunza mbinu walizotumia Morocco katika mashindano ya AFCON mwaka huu, kuhakikisha Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa […]

SAUTI YA WATANZANIA IHESHIMIWE -DK. SAMIA

DodomaNa Selina Mathew RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema sauti ya Watanzania imesikika kupitia sanduku la kura katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 29 mwaka, hivyo inapaswa kuheshimiwa.Dk. Samia aliyasema hayo katika hafla ya ufunguzi wa mwaka mpya wa mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini, Ikulu Chamwino Dodoma.   Alisema demokrasia ni safari ya ukuaji na kwamba […]

‘MOSHI MWEUPE’ WAFUKA UWANJA NDEGE MSALATO

Na FRED ALFRED, Dodoma MOSHI mweupe wenye ishara ya matumaini, umeanza kufuka Uwanja wa Msalato, baada ya Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, kusema ndege zitaanza kutua na kuruka Juni mwaka huu. Profesa Mbarawa, amesema ujenzi huo, hadi sasa umefikia asilimia 75.9, ukihusisha kazi mbalimbali, ikiwemo barabara ya kuruka na kutua ndege. Kazi hiyo imefikia […]

UCHAGUZI

WATANZANIA 37,647,235 KUPIGA KURA LEO

Na WAANDISHI WETU TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza maandalizi yote muhimu ya Uchaguzi Mkuu wa wa Rais, Wabunge na Madiwani, yamekamilika.Jumla ya wapigakura 37,647,235, wamethibitishwa kushiriki uchaguzi huo. Mwenyekiti wa INEC, Jaji Jacobs Mwambegele, amesema hayo kupitia taarifa ya tume hiyo na kusisitiza, uchaguzi huo, unafanyika kwa mujibu wa masharti ya Ibara […]

KISHINDO SIKU 60 ZA DK. SAMIA

Na MUSSA YUSUPH,Mwanza SHAMRASHAMRA za maandalizi ya mkutano wa kufunga kampeni za Uchaguzi Mkuu, zimeendelea kuutikisa Mkoa wa Mwanza ambapo Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuhutubia maelfu ya wananchi, wapenzi, wanachama na wakereketwa wa CCM. Katika mkutano huo unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28, mwaka huu, katika Uwanja wa CCM […]

DK. MWINYI AJAWA MATUMAINI KIBAO

Na HANIFA RAMADHANI, Zanzibar MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema wana matumaini kuwa CCM itashinda kwa kishindo katika Uchaguzi wa kesho kutwa. Dk. Mwinyi alisema hayo, katika ufungaji kampeni za Uchaguzi Mkuu wa CCM, uliofanyika viwanja vya Mnazi Mmoja, Mjini Unguja Alisema kutokana na wingi wa wanachama […]

DK. NCHIMBI AELEZA MAFANIKIO YA KAMPENI ZA CCM NCHINI

Na NJUMAI NGOTA,UKEREWEMGOMBEA Mwenza wa Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, amefunga kampeni za Chama kwa kishindo huku akisema amezunguka takribani mikoa yote kwa mafanikio makubwa.Katika mikutano yake ya kampeni, Dk. Nchimbi, ameinadi Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2025–2030 na kumwombea kura za Urais, Dk. Samia Suluhu […]

MAAGIZO YA DK. MWINYI KWA WATUMISHI Z’BAR

Na MWANDISHI WETU, Zanzibar RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amewasisitiza watumishi wa umma kuendelea kufanya kazi kwa uzalendo na uwajibikaji wakizingatia misingi ya utumishi na utawala bora ili kutoa huduma bora kwa wananchi. Amesema lengo la serikali ni kuimarisha zaidi maslahi ya watumishi wa umma nchini, kulingana na […]

Siasa

TULIENI NYUMBANI

>>Ni agizo la Waziri Mkuu Dk. Mwigulu >>Simbachawene  asema maandamano ni haramu Na IRENE MWASOMOLA SERIKALI imewataka wananchi wasiokuwa na ulazima wa kutoka leo, watulie nyumbani. Agizo hilo limetolewa na Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba, alipowasilisha salamu za Rais Dk. Samia Suluhu Hassan za maadhimisho ya miaka 64 ya Uhuru, ambapo aliwatakia Watanzania kheri. Kupitia […]

KIHONGOSI ATOA MAAGIZO KWA MADIWANI 

Na ATHNATH MKIRAMWENI CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimewataka madiwani kufanya kazi zinazobeba ajenda za wananchi, zitakazotoa majawabu ya kero katika maeneo yao. Pia, CCM imesema itaendelea kusimamia vyema misingi ya uadilifu kwa watendaji wa Chama. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Kenani Kihongosi, jijini Dar es Salaam, alipozungumza na […]

WASIRA : VIJANA MSIKUBALI KUTUMIKA KUVURUGA AMANI

Na MWANDISHI WETU MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, amewataka vijana kutokubali kutumika kuvuruga amani na utulivu nchini kwa madai ya kudai haki. Amesema Tanzania haina uadui na nchi nyingine, lakini yapo baadhi ya mataifa, yanayoumizwa na kasi ya maendeleo iliyopo nchini. Amesema wanafahamu Tanzania inaelekea kujikomboa kiuchumi, hivyo kuondoka […]

TUTAILINDA NCHI YETU KWA GHARAMA – PM MWIGULU

Na ELIZABETH JOHN WAZIRI Mkuu Dk. Mwigulu Nchemba, ametoa wito kwa Watanzania, kuwa makini dhidi ya makundi ya watu wenye nia ovu ya kuichafua na kuiharibu Tanzania kwa maslahi binafsi. Dk. Mwigulu, amesema serikali itawalinda Watanzania na rasilimali zake zote kwa gharama yoyote kupitia vyombo vya ulinzi na usalama. Waziri Mkuu, aliyasema hayo kufuatia matukio […]

MAWAZIRI SABA NA MIKAKATI YA KAZI

Na WAANDISHI WETU, Dodoma ZIKIWA zimepita siku nane (Sawa na saa 192), tangu Rais Dk. Samia Suluhu Hassan awaapishe mawaziri na naibu mawaziri, wametaja vipaumbele vyao katika utekelezaji wa majukumu yao vyenye dhamira ya kuwatumikia wananchi. Baadhi ya mawaziri baada ya kukabidhiwa vijiti vya kuongoza wizara zao, wameeleza walivyojipanga kutimiza ahadi zilizotolewa na Rais Dk. […]

Biashara

TRA INAVYOIMARISHA USHIRIKIANO NA WAFANYABIASHARA KUKUZA UCHUMI

Na IRENE MWASOMOLA TANGU kuingia madarakani kwa serikali ya Awamu ya Sita, inayoongozwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, imesaidia kuweka mazingira rafiki kwa wafanyabiashara kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Hakika kazi kubwa imefanyika ya kuongeza makusanyo ya kodi kupitia TRA, hivyo kufanikisha dhima ya serikali ya utekelezaji wa maendeleo kwa wananchi na taifa.  […]

TASAF KIELELEZO CHA MAFANIKIO MIAKA 64 YA UHURU

NA SULEIMAN JONGO WATANZANIA wanaadhimisha miaka 64 ya Uhuru wa Tanganyika (Tanzania Bara) ambao ulipatikana Desemba 9, mwaka 1961 huku kukiwa na mafanikio mbalimbali ya mfano. Kupatikana kwa Uhuru kunatokana na msukumo wa wananchi wa Tanzania Bara kutaka kujinasua katika makucha ya wakoloni ambayo hawakutoa nafasi kwa Waafrika weusi kujiletea maendeleo katika sekta mbalimbali zenye […]

SERIKALI YAIVALIA NJUGA TANZANITE

Na MWANDISHI WETU WAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde, amesema serikali imejipanga upya kuyatangaza na kuyainua madini ya Tanzanite kimataifa kupitia mkakati wa kurejesha hadhi ya jiwe hilo adimu duniani. Akizungumza katika mkutano na wachimbaji wadogo na wafanyabiashara wa madini ya vito katika eneo tengefu la ukuta wa Magufuli, Mirerani mkoani Manyara, Waziri Mavunde, alisema hatua […]

DK. MWIGULU ATOA SIKU 10

Na MWANDISHI MAALUMU WAZIRI Mkuu Dk. Mwigulu Nchemba, ametoa siku 10 kwa watendaji wa taasisi zinazohusika na usafiri wa mwendokasi jijini Dar es Salaam, kuainisha maeneo ya kufanyiwa kazi haraka, kurejesha hali ya mpito wakati serikali ikitafuta suluhisho la kudumu. “Wizara ya Ujenzi, TANROADS, DART, UDART, OWM-TAMISEMI, TANESCO na wadau wengine, kaeni kuanzia leo (jana), […]

TRENI ZA JIJI DAR, DODOMA ZANUKIA

Na ELIZBAETH JOHN MAANDALIZI ya ujenzi wa njia za treni za mijini katika majiji ya Dar es Salaam na Dodoma yameanza rasmi, hatua inayotarajiwa kubadili kwa kiasi kikubwa mfumo wa usafiri wa abiria na kupunguza msongamano wa magari. Akizungumza Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni […]

Michezo

DK. SAMIA AMREJESHA MAKONDA AFCON

Na NASRA KITANA RAIS Dk.Samia Suluhu Hassan, amempa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, maagizo matatu kuhusu Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON), 2027, ambayo anapaswa kujifunza Morocco. Miongoni mwa maagizo hayo ni kujifunza mbinu walizotumia Morocco katika mashindano ya AFCON mwaka huu, kuhakikisha Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa […]

CARRICK KOCHA MPYA MAN UNITED

MANCHESTER, England UONGOZI wa Klabu ya Manchester United umemtangaza Michael Carrick kuwa kocha wa muda wa kikosi hicho hadi mwishoni mwa msimu huu. Katika benchi la ufundi hivi sasa, Carrick atasaidiana na beki wa zamani wa England, Steve Holland, Jonathan Woodgate, Jonny Evans na Travis Binnion. Kiungo huyo wa zamani wa United mwenye umri wa […]

SHAGEMBE ATAMBA

Na AMINA KASHEBA BONDIA wa ngumi za kulipwa, Mtanzania Frank Shagembe, ametamba kwamba hapa nchini bado hajaona bondia wa kupigana naye na kama kuna mzawa anaamini ana uwezo huo, anamkaribisha ulingoni. Shagembe ambaye hivi sasa ni bingwa wa WBO Afrika anayecheza uzito wa juu (kilo 76), amesema mabondia wenye uzito wake nchini wamekuwa wakihofia kuchuana […]

MAKONDA WEMBE ULE ULE AFCON

Na MWANDISHI WETU WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amesisitiza maandalizi ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 kuanza mara moja. Makonda ametoa kauli hiyo ikiwa bado michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 inaendelea nchini Morocco, ambapo fainali inatarajiwa kupigwa Jumapili hii. AFCON 2027 itafanyika katika nchi za […]

TAJI LAONGEZA MZUKA YANGA

Na NASRA KITANA SIKU moja baada ya kutwaa Kombe la Mapinduzi 2026, Kocha wa Yanga, Pedro Goncalves, amefurahia kiwango cha timu yake na anaamini michuano hiyo itakuwa chachu ya kuendelea kutikisa Ligi Kuu Tanzania Bara na michuano mingine. Yanga ilibeba taji la Mapinduzi juzi baada ya kushinda kwa mikwaju ya penalti 5-4 baada ya dakika […]

Mitandao ya Kijamii

Instagram

Tiktok

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?