• ePaper
Friday, June 5, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

MWIGULU: MAMBO MAZURI YANAKUJA, AIPA TANO SERENGETI BOYS

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
June 4, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
MWIGULU: MAMBO MAZURI YANAKUJA, AIPA TANO SERENGETI BOYS
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na FRED ALFRED
Dodoma

WAZIRI Mkuu, Mwigulu Nchemba, ameipongeza timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17, Serengeti Boys, kwa kuiheshimisha Tanzania katika ulimwengu wa soka, huku akisema si muda mrefu taifa litashuhudia Kombe la Afrika likitua nchini.

Dk. Mwigulu alitoa pongezi hizo bungeni jijini Dodoma kabla ya kuanza kujibu maswali ya papo kwa papo.

Alisema mafanikio ya Serengeti Boys yanaonyesha  mchezo wa soka umepiga hatua.

“Niwapongeze vijana wetu wa Serengeti Boys kwa hatua kubwa na yenye heshima waliyofikia katika mashindano ya vijana chini ya miaka 17, kwa kucheza hatua ya fainali yenye ushindani mkubwa na kukosa bahati ya kuleta kombe.

“Niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kuwa si muda mrefu Kombe la Afrika litatua hapa nchini, kwa sababu mwelekeo tulionao ni sahihi na tupo vizuri. Mambo makubwa yanakuja,” alisema Waziri Mkuu.

Aidha, Waziri Mkuu alisema hatua zilizofikiwa na klabu za Simba na Yanga katika michuano mikubwa ya klabu barani Afrika ni ishara kuwa soka la Tanzania linaendelea kupiga hatua na lina uwezo wa kutwaa mojawapo ya mataji ya Afrika katika siku zijazo.

Serengeti Boys, Jumanne usiku ilishika nafasi ya pili katika fainali za AFCON U 17, baada ya kufungwa mikwaju ya penalti 4-2 dhidi ya Senegal katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Moulay El Hassan, Rabat, Morocco.

Serengeti Boys ilianza michuano hiyo kwa kuifunga Msumbiji mabao 3-0, iliichapa Angola 3-0, ilipoteza mbele ya Mali kwa mabao 2-1, ikaitandika Algeria penalti 4-3 kabla ya kuirarua Misri kwa penalti 4-3.

Kwa mara ya kwanza Serengeti Boys ilishiriki michuano hiyo mwaka 2017 nchini Gabon kabla ya kucheza tena 2019 katika fainali zilizofanyika Tanzania ambapo timu hiyo ilitolewa hatua ya makundi.

Previous Post

SERENGETI BOYS HESHIMA KILA KONA

Next Post

HESHIMA KUBWA KWA TANZANIA

Next Post
HESHIMA KUBWA KWA TANZANIA

HESHIMA KUBWA KWA TANZANIA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

‘TUMUOMBEE KARDINALI PENGO’

‘TUMUOMBEE KARDINALI PENGO’

5 months ago
NEEMA LUKUKI BANDARI KILWA

NEEMA LUKUKI BANDARI KILWA

6 months ago

Popular News

  • MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WFP KUENDELEZA USHIRIKIANO NA TANZANIA USIMAMIZI WA MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • HESHIMA KUBWA KWA TANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU: MAMBO MAZURI YANAKUJA, AIPA TANO SERENGETI BOYS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERENGETI BOYS HESHIMA KILA KONA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?