• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

ZIARA YA KIHONGOSI MWANZA YAREJESHA MATUMAINI KWA WANANCHI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 13, 2026
in Habari, Kitaifa, Siasa
0
ZIARA YA KIHONGOSI MWANZA YAREJESHA MATUMAINI KWA WANANCHI
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

ZIARA ya Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Kenan Kihongosi, mkoani Mwanza, imerejesha matumani kwa wananchi wa jiji hilo.

Kihongosi ambaye amefanya mkutano wa hadhara katika Viwanja vya Furahisha, Nyamagana mkoani humo, ametatua baadhi ya changamoto za wananchi papo kwa papo.

Miongoni mwa wananchi waliotatuliwa changamoto zao ni mama mmoja aitwaye Happiness Benedict, aliyeomba msaada wa matibabu kutokana na tatizo la kusagika kwa nyonga lililomsumbua kwa takribani miaka mitano.

Amesema madaktari walimwambia anatakiwa kufanyiwa upasuaji, ambapo gharama ya matibabu inakadiriwa kufikia zaidi ya Sh. milioni 14.

Happiness amesema awali alikuwa na bima ya afya lakini ilikwisha muda wake, hivyo sasa hana uwezo wa kumudu gharama za matibabu.

“Hatuwezi kushindwa kupata Sh. milioni 14 au 15 kwa ajili ya kuokoa maisha ya mtu, tutashughulikia suala hili,” amesema Kihongosi.

Baada ya kumalizika mkutano, Kihongosi alimwita DMO kumhabarisha kuwa amepokea kiasi cha Sh. milioni 15 kupitia akaunti ya NMB kwa ajili ya matibabu ya Happiness.

Pia, amesaidia kupatikana kwa ada ya mwanafunzi wa chuo ambaye aliomba msaada katika mkutano huo ili aweze kuendelea na masomo, na fedha hizo zilipatikana hapo hapo.

Previous Post

IBENGE FURAHA TELE

Next Post

WATANZANIA SABA WAWASILI NCHINI KUTOKEA IRAN

Next Post
WATANZANIA SABA WAWASILI NCHINI KUTOKEA IRAN

WATANZANIA SABA WAWASILI NCHINI KUTOKEA IRAN

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

COMORO YAENDELEA KUDUMISHA USHIRIKIANO NA TANZANIA KATIKA SEKTA YA AFYA

COMORO YAENDELEA KUDUMISHA USHIRIKIANO NA TANZANIA KATIKA SEKTA YA AFYA

5 months ago
DK. SAMIA AVUTIA MAELFU KILA KONA

DK. SAMIA AVUTIA MAELFU KILA KONA

6 months ago

Popular News

  • KIGOGO CHAUMMA ‘AIPA TANO’ TUME YA JAJI CHANDE

    KIGOGO CHAUMMA ‘AIPA TANO’ TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MUYUNGI ASISITIZA WANANCHI KUFANYA BIASHARA YA KABONI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KAMATI YA UTALII, BIASHARA NA KILIMO BARAZA LA WAWAKILISHI YADHAMIRIA MAMLAKA YA VIPIMO ZANZIBAR IFIKIE VIWANGO VYA WMA BARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • LAZARUS CHAKWERA AMALIZA ZIARA YA SIKIU 9 NCHINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA KISHINDO SGR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?