• ePaper
Tuesday, July 28, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

RAIS DK. SAMIA ATAJA SIFA ZA MAWASILIANO SERIKALINI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
July 28, 2026
in Habari, Kitaifa
0
RAIS DK. SAMIA ATAJA SIFA ZA MAWASILIANO SERIKALINI
0
SHARES
0
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI MAALUMU, Zanzibar

RAIS Dk.  Samia Suluhu Hassan, amesema mawasiliano serikalini yanahitaji uratibu, weledi na mwelekeo wa kimkakati kujenga imani ya wananchi kwa serikali na kulinda maslahi ya Taifa.

Amesema hayo Ikulu ya Tunguu, Zanzibar, , alipofungua semina elekezi ya mawaziri, naibu mawaziri na makatibu wakuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuhusu umuhimu wa mawasiliano serikalini.

“Mawasiliano ni sehemu ya uongozi na nyenzo ya kimkakati ya kulinda maslahi ya taifa,” alisema.

Alieleza kuwa, mawasiliano yanapotumika vizuri hujenga ushirikishwaji na imani ya wananchi kwa serikali, huku taarifa sahihi zikiwawezesha kuelewa na kushiriki katika mipango ya maendeleo.

“Taarifa za serikali zinapaswa kutolewa kwa wakati, kwa lugha inayoeleweka na kwa takwimu zilizothibitishwa,” alisema.

Rais Dk. Samia alisema serikali zote mbili zimepata mafanikio katika sekta za elimu, afya, miundombinu, nishati na maeneo mengine ya maendeleo, ambayo yanapaswa kuelezwa kwa wananchi kwa ufasaha.

Kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Rais Dk. Samia alisema serikali zimeanza kutekeleza mageuzi ya uchumi na huduma zinazowagusa wananchi moja kwa moja.

Alisema takribani asilimia 70 ya utekelezaji wa Dira 2050 inategemea ushiriki wa sekta binafsi, hivyo mafanikio yake yanahitaji mawasiliano na ushirikiano wa karibu kati ya serikali na sekta hiyo.

Awali, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dk. Moses Kusiluka, alisema semina hiyo ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais Dk. Samia ya kuwajengea viongozi uwezo katika mawasiliano ya serikali na umma.

Alisema mafunzo hayo yatahusu utoaji wa taarifa kwa ufasaha na kwa wakati pamoja na matumizi sahihi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

Semina hiyo ya siku mbili imewakutanisha, kwa mara ya kwanza, viongozi waandamizi wa serikali kutoka pande zote mbili za Muungano, kwa lengo la kujenga uelewa na msimamo wa pamoja kuhusu mawasiliano ya serikali na umma.

Previous Post

50 BORA ‘FORM SIX’ KUSOMA AI NJE YA NCHI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MOTO WA DK. MWIGULU HAUPOI

MOTO WA DK. MWIGULU HAUPOI

5 months ago
KOCHA SIMBA AIPANIA MASHUJAA

KOCHA SIMBA AIPANIA MASHUJAA

6 months ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA ATAJA SIFA ZA MAWASILIANO SERIKALINI

    RAIS DK. SAMIA ATAJA SIFA ZA MAWASILIANO SERIKALINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • 50 BORA ‘FORM SIX’ KUSOMA AI NJE YA NCHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DHAHABU YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.2/- YAKAMATWA IKITOROSHWA DAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA ATAKA UADILIFU, USHIRIKIANO NA MATOKEO KWA VIONGOZI WAPYA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KAIRUKI YAFIKISHA WATOTO 160 UPANDIKIZAJI MIMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?