• ePaper
Monday, July 27, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DHAHABU YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.2/- YAKAMATWA IKITOROSHWA DAR

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
July 27, 2026
in Habari, Kitaifa
0
DHAHABU YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.2/- YAKAMATWA IKITOROSHWA DAR
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

KUFUATIA  kuimarishwa kwa mfumo wa udhibiti wa biashara haramu ya madini unaofanywa na Wizara ya Madini kupitia Kikosi Kazi (Taskforce), madini aina ya dhahabu Gramu 4,402.20 yenye thamani ya shilingi bilioni 1.2, yamekamatwa wakati yakitoroshwa.

Hayo yamesemwa leo Julai 27, 2026 na Waziri wa Madini,  Anthony Mavunde, alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam.

Amesema serikali kupitia Wizara ya Madini iliunda Kikosi kazi ambacho kinahusisha vyombo vya dola ili kudhibiti biashara haramu ya madini na utoroshaji na hii, ni sehemu tu ya kazi ambazo zimeendelea kufanywa na Kikosi kazi hicho katika kuimarisha mfumo wa ufanyaji biashara ya madini.

“Ndugu zangu, dhahabu hii yenye zaidi ya thamani ya bilioni 1.2 haikupitia katika mfumo rasmi wa ufanyaji biashara ya madini,  hivyo kupelekea serikali kukosa mapato ambayo yangeisaidia kuimarisha utoaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi,” amesema Mavunde.

Aidha, Waziri Mavunde amebainisha kuwa, dhahabu hiyo iliyokamatwa imetaifishwa kwa mujibu wa taratibu za sheria na imehifadhiwa Benki Kuu ya Tanzania.

Vilevile, Waziri Mavunde amekielekeza Kikosi Kazi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola, kumhoji vizuri mtuhumiwa aliyekamatwa na dhahabu hizo kufahamu alikotoka na alikuwa anapeleka wapi, ili kutibu kabisa mzizi wa vitendo hivyo.

Pia, ameelekeza kuwa, kama mtuhumiwa huyo ana leseni ya ufanyaji biashara ya madini, afutiwe mara moja na kuingizwa kwenye orodha maalumu ya watu  ya wenye makosa (blacklisted), ili asiruhusiwe tena kufanya biashara hiyo.

Previous Post

RAIS DK. SAMIA ATAKA UADILIFU, USHIRIKIANO NA MATOKEO KWA VIONGOZI WAPYA

Next Post

50 BORA ‘FORM SIX’ KUSOMA AI NJE YA NCHI

Next Post
50 BORA ‘FORM SIX’ KUSOMA AI NJE YA NCHI

50 BORA 'FORM SIX' KUSOMA AI NJE YA NCHI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KARIA ATAKA WANAMICHEZO KUDUMISHA AMANI

KARIA ATAKA WANAMICHEZO KUDUMISHA AMANI

4 months ago
WASHIRIKI MISS WORLD TANZANIA WAPEWA SOMO

WASHIRIKI MISS WORLD TANZANIA WAPEWA SOMO

3 months ago

Popular News

  • 50 BORA ‘FORM SIX’ KUSOMA AI NJE YA NCHI

    50 BORA ‘FORM SIX’ KUSOMA AI NJE YA NCHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DHAHABU YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.2/- YAKAMATWA IKITOROSHWA DAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA ATAKA UADILIFU, USHIRIKIANO NA MATOKEO KWA VIONGOZI WAPYA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KAIRUKI YAFIKISHA WATOTO 160 UPANDIKIZAJI MIMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KILIO WANAOKATWA MATITI CHAPATA TIBA MUHIMBILI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?