• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home AFYA

COMORO YAENDELEA KUDUMISHA USHIRIKIANO NA TANZANIA KATIKA SEKTA YA AFYA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 6, 2025
in AFYA, Habari, Kitaifa
0
COMORO YAENDELEA KUDUMISHA USHIRIKIANO NA TANZANIA KATIKA SEKTA YA AFYA
0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na Mwandishi Wetu,
Dar es Salaam

MAKAMU wa Rais wa Comoro ambaye pia ni Spika wa Bunge la Taifa hilo, Moustadroine Abdou, amesema Serikali ya Comoro itaendelea kudumisha ushirikiano wa kidugu na Tanzania, hususan katika sekta ya afya ambayo imekuwa mfano wa mafanikio ya ushirikiano wa kikanda.

Akizungumza alipotembelea Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI) jijini Dar es Salaam, baada ya kuwasili nchini kumwakilisha Rais wa Comoro katika sherehe za uapisho wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, Abdou amesema amevutiwa na maendeleo makubwa ya huduma za afya nchini.

“Nimefika Tanzania kwa mara ya tatu. Nchi hii ni tulivu, yenye amani na watu wenye upendo. Nawapongeza kwa uchaguzi mzuri na kumpata kiongozi bora, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan,” amesema Abdou.

Ameongeza kuwa ushirikiano kati ya Tanzania na Comoro katika sekta ya afya umeendelea kuimarika, ambapo madaktari wa Tanzania wamekuwa wakitoa huduma na mafunzo nchini humo, sambamba na wananchi wa Comoro kufika Tanzania kupata matibabu kutokana na vifaa vya kisasa na miundombinu bora iliyopo.

Kwa upande wake, Balozi wa Tanzania nchini Comoro, Said Yakoub, amemshukuru Makamu wa Rais huyo kwa kuitembelea ORCI na kueleza kuwa amekuwa balozi mzuri wa kuitangaza Tanzania kwa wananchi wa Comoro kutokana na mapenzi makubwa aliyonayo kwa nchi hii.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa ORCI, Dk. Diwani Msemo, amesema uhusiano wa Tanzania na Comoro ni wa kihistoria na umejikita katika misingi ya urafiki wa watu na serikali zao, ambao sasa unaendelea kuimarishwa kupitia sekta mbalimbali ikiwemo afya.

“Tuna furaha kuona viongozi wa Comoro wanatambua mchango wa Tanzania katika afya na kuendeleza ushirikiano huu wa kidugu,” amesema Dk. Msemo.

Previous Post

MBETO : RAIS DK. SAMIA, MWINYI WAMEAPA KULINDA WATANZANIA NA AMANI YA TAIFA

Next Post

NECTA : TUMETOA MATOKEO KWA NAMBA KULINDA TAARIFA BINAFSI ZA WANAFUNZI

Next Post
NECTA : TUMETOA MATOKEO KWA NAMBA KULINDA TAARIFA BINAFSI ZA WANAFUNZI

NECTA : TUMETOA MATOKEO KWA NAMBA KULINDA TAARIFA BINAFSI ZA WANAFUNZI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MKENDA AANIKA MAGEUZI MAKUBWA SEKTA YA ELIMU

MKENDA AANIKA MAGEUZI MAKUBWA SEKTA YA ELIMU

4 months ago
AZAM, YANGA MECHI YA KISASI, HESHIMA

AZAM, YANGA MECHI YA KISASI, HESHIMA

1 month ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?