• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

AHADI 5 ZA MGOMBEA URAIS WA CCM, IGUNGA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 12, 2025
in Habari, Kitaifa
0
AHADI 5 ZA MGOMBEA URAIS WA CCM, IGUNGA

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
0
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, ametoa ahadi tano zitakazofungua uchumi wa wananchi wilayani Igunga mkoani Tabora.

Akizungumza na wananchi katika mkutano wa kampeni wilayani Igunga mkoani Tabora, Dk. Samia, aliwaomba wananchi kuipa ridhaa CCM kushika hatamu ya uongozi katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu. 

Dk. Samia, alisema serikali yake pindi itakapoingia madarakani, itajenga stendi ya kisasa ya mabasi katika mji huo.

Vilevile, aliahidi kujenga soko la kisasa, ambalo likikakamilika, linafungua na kuongeza wigo wa biashara na kuvutia uwekezaji.

Aliahidi kujenga kwa kiwango cha lami barabara ambazo zinapita katika maeneo ya uzalishaji wa mpunga, mbaazi, dengu, choroko na madini hatua ambayo, itachangia ukuaji uchumi.

Alisema pamoja na kazi kubwa katika kusambaza umeme katika vijiji na vitongoji na kuahidi kujenga kituo cha kupokea na kupooza umeme katika wilaya hiyo.

Dk. Samia, alisema Igunga itaanzisha kongani ya viwanda na kuongeza thamani ya mazao.

Kuhusu changamoto ya wanyamapori, alisema serikali itakuja na njia sahihi ya kudhibiti wanyamapori waharibifu ambao wamekuwa kero kwa wananchi wa vijiji vinavyopakana na hifadhi.

Pia, aliahidi kuendelea kuimarisha huduma za afya, maji na elimu hasa kutokana na kuwepo kwa uhitaji wa huduma hizo kwa wananchi.

“Ili tuyafanye haya na mengine ambayo yako katika ilani ya uchaguzi kwa Igunga ni lazima ushindi kwa CCM. Sina mashaka na Igunga kuwa tutapata ushindi. 

“Tunachotaka siyo ushindi pekee, bali ushindi wa heshima tuwazibe midomo wale wengine.”

“Kumekuwa na idadi kubwa ya kuhudhuria mikutano, nawapongeza kwa hilo, sasa uwingi huu wa watu, pia ukaonekane katika sanduku la kura,” alisema.

Previous Post

WAZIRI MKUU AGUSIA UMUHIMU WA TATHIMINI

Next Post

CCM YAELEZA KUONGEZEKA MBOLEA YA RUZUKU

Next Post
CCM YAELEZA KUONGEZEKA MBOLEA YA RUZUKU

CCM YAELEZA KUONGEZEKA MBOLEA YA RUZUKU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA AAHIDI MAGEUZI MAKUBWA YA KILIMO

DK. SAMIA AAHIDI MAGEUZI MAKUBWA YA KILIMO

1 month ago
VYAMA 18 Z’BAR VYASAINI FOMU KUELEKEA UCHAGUZI

VYAMA 18 Z’BAR VYASAINI FOMU KUELEKEA UCHAGUZI

2 months ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.