• ePaper
Saturday, November 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Biashara

YANGA, SIMBA KAZI KAZI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 15, 2025
in Biashara, Kimataifa, Michezo
0
YANGA, SIMBA KAZI KAZI

SIMBA & YANGA

0
SHARES
1
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

IKISALIA wiki moja kabla ya kucheza mechi zake za kwanza za hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL), Simba na Yanga zinatarajiwa kucheza mechi za kirafiki kujifua.

Katika CAFCL wiki ijayo, Yanga iliyopo kundi B inatarajiwa kuchuana na FAR Rabat ya Morocco wakati Simba iliyopo kundi D, ikicheza na Petro de Luanda.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, amesema timu yao imeshaanza mazoezi kwa wachezaji ambao hawapo katika timu ya taifa na mwalimu ameomba mchezo mmoja wa kirafiki kabla ya kuchuana na Petro de Luanda.

Amesema mwalimu wao ametaka mchezo huo ikiwa ni moja ya maandalizi katika mechi ya kimataifa kwani anahitaji kuona wapi kuna mapungufu afanye marekebisho ya mapema.

Ahmed amesema lengo kubwa la mchezo huo wa kifariki ni kuwaweka sawa wachezaji wao ambao hawajaitwa katika kikosi cha Stars.

Naye Ofisa habari wa Yanga Ally Kamwe amesema timu yao leo inatarajiwa kushuka dimbani kupambana na KMC katika mchezo wa kirafiki.

Amesema mchezo huo ni muhimu kwa wachezaji wao kwani itakuwa ni moja ya maandalizi kabla ya kushuka dimbani kumenyana na FAR Rabat.

“Tunajua tunaingia katika mchezo mgumu hivyo mwalimu ameona bora kupata mchezo wa kirafiki dhidi ya KMC kujiweka sawa kabla ya kukabiliana na wapinzani wetu,” amesema.

Katika kundi B, Yanga imepangwa na timu za Al Ahly ya Misri, AS FAR ya Morocco na JS Kabyile ya Algeria wakati Simba ikiwa kundi D na Esperance kutoka Tunisia, Petro De Luanda ya Angola na Stade Malien kutoka Mali.

Previous Post

KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

CCM YAAHIDI KILIMO CHA BIASHARA KWA WAKULIMA

CCM YAAHIDI KILIMO CHA BIASHARA KWA WAKULIMA

2 months ago
DK. SAMIA ATAJA SIFA ZA VIONGOZI WANAOFAA

DK. SAMIA ATAJA SIFA ZA VIONGOZI WANAOFAA

1 month ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.