• ePaper
Monday, June 8, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Biashara

YANGA, SIMBA KAZI KAZI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 15, 2025
in Biashara, Kimataifa, Michezo
0
YANGA, SIMBA KAZI KAZI

SIMBA & YANGA

0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

IKISALIA wiki moja kabla ya kucheza mechi zake za kwanza za hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL), Simba na Yanga zinatarajiwa kucheza mechi za kirafiki kujifua.

Katika CAFCL wiki ijayo, Yanga iliyopo kundi B inatarajiwa kuchuana na FAR Rabat ya Morocco wakati Simba iliyopo kundi D, ikicheza na Petro de Luanda.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, amesema timu yao imeshaanza mazoezi kwa wachezaji ambao hawapo katika timu ya taifa na mwalimu ameomba mchezo mmoja wa kirafiki kabla ya kuchuana na Petro de Luanda.

Amesema mwalimu wao ametaka mchezo huo ikiwa ni moja ya maandalizi katika mechi ya kimataifa kwani anahitaji kuona wapi kuna mapungufu afanye marekebisho ya mapema.

Ahmed amesema lengo kubwa la mchezo huo wa kifariki ni kuwaweka sawa wachezaji wao ambao hawajaitwa katika kikosi cha Stars.

Naye Ofisa habari wa Yanga Ally Kamwe amesema timu yao leo inatarajiwa kushuka dimbani kupambana na KMC katika mchezo wa kirafiki.

Amesema mchezo huo ni muhimu kwa wachezaji wao kwani itakuwa ni moja ya maandalizi kabla ya kushuka dimbani kumenyana na FAR Rabat.

“Tunajua tunaingia katika mchezo mgumu hivyo mwalimu ameona bora kupata mchezo wa kirafiki dhidi ya KMC kujiweka sawa kabla ya kukabiliana na wapinzani wetu,” amesema.

Katika kundi B, Yanga imepangwa na timu za Al Ahly ya Misri, AS FAR ya Morocco na JS Kabyile ya Algeria wakati Simba ikiwa kundi D na Esperance kutoka Tunisia, Petro De Luanda ya Angola na Stade Malien kutoka Mali.

Previous Post

KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

Next Post

RAIS DK. SAMIA AWAKOSHA VIONGOZI WA DINI NCHINI

Next Post
RAIS DK. SAMIA AWAKOSHA VIONGOZI WA DINI NCHINI

RAIS DK. SAMIA AWAKOSHA VIONGOZI WA DINI NCHINI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RAIS DK. SAMIA, DK. NCHIMBI WAIMWAGIA SIFA STARS

RAIS DK. SAMIA, DK. NCHIMBI WAIMWAGIA SIFA STARS

5 months ago
TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

1 month ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA ZATOA MSIMAMO LIGI KUU BARA

    YANGA, SIMBA ZATOA MSIMAMO LIGI KUU BARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WFP KUENDELEZA USHIRIKIANO NA TANZANIA USIMAMIZI WA MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • HESHIMA KUBWA KWA TANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU: MAMBO MAZURI YANAKUJA, AIPA TANO SERENGETI BOYS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?