• ePaper
Sunday, February 1, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

MAKONDA ASISITIZA KUTOVUMILIA WAKANDARASI WAZEMBE AFCON

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 31, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
MAKONDA ASISITIZA KUTOVUMILIA WAKANDARASI WAZEMBE AFCON
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

NA SELINA MATHEW, Dodoma

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesisitiza kutovumilia wakandarasasi na watendaji wazembe watakaokwamisha kukamilika kwa utekelezaji mradi wa ujenzi wa Uwanja wa Soka wa Arusha na uboreshaji miundombinu ya michezo nchini ambayo itatumika katika fainali za michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2027).

Michuano hiyo msimu ujao inatarajia kufanyika katika nchi tatu za Tanzania, Kenya na Uganda.

Amewataka wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo kuhakikisha inakamilika kwa mujibu wa mkataba na siyo vinginevyo.

Makonda aliyasema hayo bungeni jioni, wakati akichangia hotuba ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa katika Bunge, Novemba, mwaka jana ambayo ilihitimishwa juzi.

Alisema Dk. Samia amewekeza katika miundombinu ya michezo ambapo kiasi cha sh. trilioni 1.27 zimetolewa kubadilisha mazingira na kuwatenegenezea vijana mazingira mazuri kupitia sekta hiyo.

“Mfano uwanja wa mpira wa Arusha ambao unajengwa umeshazidi asilimia 70 ya ujenzi ambapo sh. bilioni 338 zinatumika, mkandarasi ameshalipwa sh.bilioni 55 katika mkataba.

“Kadhalika, viwanja vya mazoezi vya AFCON 2027 sh. bilioni 51, ukarabati Uwanja wa Benjamin Mkapa sh. bilioni 31, Uwanja wa Uhuru sh.bilioni 19, Rais Dk. Samia amedhamiria kubadilisha na kujenga miundombinu ya michezo kwa ajili ya kizazi cha sasa na baadae,” alisema Makonda.

Makonda alitoa rai kwa wasimamizi na wajenzi wa miradi hiyo ambao ni wizara na wakandarasi kuhakikisha wanafanya kazi kwa mujibu wa mkataba.

“Tunataka viwanja vikamilike kabla ya mashindano ya AFCON 2027, vitabeba sura ya taifa na kuliweka katika ramani ya dunia kwa namna ya jinsi ndoto ya Rais Dk. Samia alivyotaka.

“Sitamvumilia mtu yeyote atakayekuwa mzembe, atakayeshindwa kukamilisha miradi hii kama ambavyo mikataba inataka,” alisema.

Pia aliipongeza Taifa Stars ambayo iliingia katika hatua ya 16 bora ya michuano ya AFCON 2025, iliyomalizika hivi karibuni nchini Morocco.

Waziri Makonda alisema serikali inakuja na mipango mizuri kuhakikisha kila mkoa unakuwa na timu yake ili kuweka ushindani wa michezo nchini.

“Tunatamani kuwa na mifumo ya kuandaa vijana katika umri mdogo waliopo shule wapate fursa ya kutumia nafasi ambayo Mwenyezi Mungu amewapa kupitia vipaji vyao ambapo shule 56 za mfano zinajengwa kwa ajili ya kuwatenegeneza watakaofanya vizuri.

“Ninawaomba wakuu wa mikoa, kila mkoa iwepo timu ya mkoa ili kuwatengenezea mazingira mazuri vijana wenye vipaji.

“Pia, mashirika ya umma yamiliki timu za mpira wa soka ili kuongeza hamasa, tuhakikishe watu wanashiriki michezo kila mahali,” alisema Makonda.

Previous Post

NMB YAONGEZA  MAGARI MAALUMU YA HUDUMA ZA KIFEDHA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MAWAZIRI SABA NA MIKAKATI YA KAZI

MAWAZIRI SABA NA MIKAKATI YA KAZI

2 months ago
DK. SAMIA AELEZA VIPAUMBELE SIKU 100 ZA KWANZA AKIWA RAIS

DK. SAMIA AELEZA VIPAUMBELE SIKU 100 ZA KWANZA AKIWA RAIS

5 months ago

Popular News

  • MAKONDA ASISITIZA KUTOVUMILIA WAKANDARASI WAZEMBE AFCON

    MAKONDA ASISITIZA KUTOVUMILIA WAKANDARASI WAZEMBE AFCON

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NMB YAONGEZA  MAGARI MAALUMU YA HUDUMA ZA KIFEDHA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, AL AHLY MECHI YA MAAMUZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA ALIVYOIPAISHA MICHEZO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • PAPA LEO XIV APOKEA UJUMBE WA RAIS DK. SAMIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?