• ePaper
Saturday, November 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Burudani

JKT TZ, SIMBA BALAA LIPO HAPA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 8, 2025
in Burudani, Kitaifa, Michezo
0
JKT TZ, SIMBA BALAA LIPO HAPA

JKT VS SIMBASC

0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

TIMU ya soka ya Simba leo itashuka dimbani dhidi JKT Tanzania katika mchezo wa kuwania kukaa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu.

Mchezo huo unatarajiwa kupigwa saa 1:00 usiku katika Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo uliopo Mbweni, Dar es Salaam.

Katika ligi hiyo, JKT Tanzania ipo nafasi ya tano kwa pointi saba katika mechi tano wakati Simba ipo nafasi ya saba kwa alama sita katika mechi mbili, yeyote kati ya hizo ina nafasi ya kukaa kileleni mwa msimamo kama itavuna pointi tatu katika mtanange wa leo.

Miamba hiyo ipo chini ya Yanga iliyopo nafasi ya nne kwa alama saba katika michezo mitatu, Mashujaa, Dodoma Jiji na Mbeya City ambayo kila moja ina pointii nane zikicheza mechi sita.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Kocha Msaidizi wa Simba, Suleiman Matola, alisema wataingia katika mchezo huo kwa kuwaheshimu wapinzani lakini watahakikisha wanapata pointi tatu muhimu.

Kocha Matola alisema JKT ni timu nzuri yenye wachezaji wenye viwango bora hivyo wataingia kwa tahadhari kubwa na kufanya mashambulizi ya kushtukiza kupata ushindi.

“Ni mchezo mgumu lakini tunaiheshimu JKT Tanzania, tutaingia kwa tahadhari na kupambana mwanzo mwisho, tunataka kupata ushindi na kujizolea pointi tatu muhimu,” alisema Matola.

Kocha huyo alisema hana hofu na kikosi chake kwani kila mchezaji anajua jukumu lake la kuipambania timu katika kila mchezo wanaocheza.

Matola alisema kuwa wachezaji wote wapo fiti isipokuwa kipa wake Moussa Camara atakosekana kutokana na majeraha lakini wana kikosi kipana chenye ushindani.

Kocha wa JKT Tanzania, Ahmad Ally alisema timu yao imejipanga vizuri kupambana na Simba japokuwa ina wachezaji wazuri wenye viwango bora.

Alisema hawana presha na mchezo huo kwani wamefanya maandalizi ya kutosha na anaifahamu vyema Simba hivyo ataingia na mbinu mbadala kupata ushindi.

“Simba ni timu kubwa na yenye wachezaji bora, lakini hatuna presha kwani tumejipanga vyema kuhakikisha tunapata ushindi katika mchezo huo hasa katika uwanja wa nyumbani,” alisema Ahmad.

Previous Post

‘MLIOGHUSHI AKAUNTI ZA JKT MITANDOANI ZIFUTENI HARAKA’

Next Post

SADC WAMPONGEZA RAIS DK. SAMIA KWA USHINDI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 2025

Next Post
SADC WAMPONGEZA RAIS DK. SAMIA KWA USHINDI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 2025

SADC WAMPONGEZA RAIS DK. SAMIA KWA USHINDI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 2025

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

ARAJIGA, KAYOKO HAOO CAFCL

ARAJIGA, KAYOKO HAOO CAFCL

2 months ago
DK. SAMIA, MWINYI WAMELETA MAENDELEO NCHINI – DK. NCHIMBI

DK. SAMIA, MWINYI WAMELETA MAENDELEO NCHINI – DK. NCHIMBI

1 month ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.