• ePaper
Wednesday, March 18, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

KAHAWA YA TANZANIA KUONGEZEWA THAMANI KABLA YA KUPELEKWA NJE

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 24, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
KAHAWA YA TANZANIA KUONGEZEWA THAMANI KABLA YA KUPELEKWA NJE
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema serikali imejipanga kuhakikisha kahawa inayozalishwa nchini inaongezwa thamani kabla ya kusafirishwa nje ya nchi.

Alieleza hayo katika mkutano wa kampeni uliofanyika uwanja wa VETA mjini Songea ambapo alisema Januari, mwaka huu, Tanzania ilikuwa mwenyeji wa mkutano wa nchi 25 za Afrika zinazozalisha kahawa.

Dk. Samia alisema katika mkutano huo, liliwekwa lengo la ndani ya miaka 10 ijayo (2025-2035) asilimia 50 ya kahawa bora inayozalishwa Afrika iwe inasindikwa kabla ya kuuzwa nje ya Afrika.

Alibainisha lengo la serikali kutekeleza azimio hilo, ambapo CCM imeweka ahadi kuweka mitambo ya kukoboa kahawa kabla haijauzwa.

Alisema serikali imetekeleza mradi wa ujenzi maghala 28 ya kuhifadhia mazao mkoani Ruvuma akiainisha Halmashauri ya Wilaya ya Songea ina maghala 11, Madaba (tisa), Namtumbo (saba) na ghala moja kwa Manispaa ya Songea.

Aidha, alisema katika Manispaa ya Songea, serikali itakamilisha ujenzi wa soko la kisasa Manzese A na B.

“Soko hilo ambalo mmelisubiri kwa muda mrefu hivi sasa linajengwa na hatujawasahau wanangu wamachinga mtakuwa na sehemu katika soko hilo.

“Niseme pia mkoa huu umebarikiwa kuwa na madini mengi kuanzia dhahabu, shaba, makaa ya mawe, madini ujenzi na vito hadi urani yanapatikana ndani ya mkoa huu,” alisisitiza.

Dk. Samia alieleza endapo CCM ikipatiwa ridhaa, serikali yake itaanzisha na kuendeleza kongani za viwanda zinazohusiana na madini.

Aliongeza hatua hiyo itasaidia kuongeza thamani ya madini kabla ya kuuzwa huku kipaumbele kikiwa katika uchimbaji na wachimbaji wadogo.

Previous Post

DK. SAMIA : TUNATAKA USHINDI WA HESHIMA

Next Post

RC MAKALLA ATAKA MPANGO MKAKATI WA UTALII UKIJUMUISHA FURSA NA MAANDALIZI YA AFCON 2027

Next Post
RC MAKALLA ATAKA MPANGO MKAKATI WA UTALII UKIJUMUISHA FURSA NA MAANDALIZI YA AFCON 2027

RC MAKALLA ATAKA MPANGO MKAKATI WA UTALII UKIJUMUISHA FURSA NA MAANDALIZI YA AFCON 2027

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RAIS DK. SAMIA AMLILIA STEVEN HIZA

RAIS DK. SAMIA AMLILIA STEVEN HIZA

4 weeks ago
TANZANIA NA GHANA KUIMARISHA USHIRIKIANO KIUCHUMI NA AJIRA KWA VIJANA

TANZANIA NA GHANA KUIMARISHA USHIRIKIANO KIUCHUMI NA AJIRA KWA VIJANA

2 weeks ago

Popular News

  • MANDONGA AJA KIVINGINE

    MANDONGA AJA KIVINGINE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YATUMIA BILIONI 64/- KUBORESHA UWANJA WA NDEGE IRINGA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU AWAWEKA MTEGONI VIGOGO WILAYA, HALMASHAURI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ALAMA TATU KUMUENZI JPM

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI KUIFANYA TANZANIA KITOVU CHA BIASHARA – DK. YONAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?