• ePaper
Sunday, August 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

SERIKALI YATUMIA BILIONI 64/- KUBORESHA UWANJA WA NDEGE IRINGA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 17, 2026
in Habari, Kitaifa
0
SERIKALI YATUMIA BILIONI 64/- KUBORESHA UWANJA WA NDEGE IRINGA
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MICHAEL KATONA, Iringa

SERIKALI imetumia sh. bilioni 64 kuboresha miundombinu ya Uwanja wa Ndege wa Iringa, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kukuza utalii na kuimarisha uchumi wa mkoa huo.

Akizungumza katika kongamano la wadau wa habari Kusini mwa Tanzania (MISA TAN SUMMIT), Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James alisema serikali inalenga kuboresha huduma za usafiri wa anga ili kurahisisha upatikanaji wa safari kwa watalii, wasafiri wa ndani na nje ya nchi.

Alisema sehemu ya fedha hizo imetumika kujenga jengo jipya la abiria na eneo la maegesho ya magari kwa gharama ya takribani sh. bilioni 41.06, ambapo jengo hilo linatarajiwa kuhudumia abiria 120 kwa wakati mmoja.

“Serikali inaendelea kuhakikisha miundombinu ya uwanja wa ndege inaboreshwa ili kuchochea ukuaji wa sekta ya utalii katika Nyanda za Juu Kusini,” alisema James.

Aidha, James, alisema kufanyika kongamano mkoani humo, kutasaidia kuongeza uelewa kwa wananchi kuhusu shughuli za maendeleo na kutangaza fursa zilizopo Iringa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa MISA Tanzania, Edwin Soko, aliomba serikali ya mkoa kutenga eneo kwa ujenzi wa kituo cha mawasiliano kitakachosaidia kuboresha upatikanaji wa taarifa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Benjamin Sitta, aliwataka wanahabari kutumia majukwaa yao kuelimisha vijana kuhusu matumizi sahihi ya fursa za kiuchumi ili kupunguza umaskini.

Previous Post

MWIGULU AWAWEKA MTEGONI VIGOGO WILAYA, HALMASHAURI

Next Post

MANDONGA AJA KIVINGINE

Next Post
MANDONGA AJA KIVINGINE

MANDONGA AJA KIVINGINE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KIBADENI, MANARA, MAYAY WAFUNGUKA MANUFAA YA AMANI

KIBADENI, MANARA, MAYAY WAFUNGUKA MANUFAA YA AMANI

7 months ago
ARAJIGA, KAYOKO HAOO CAFCL

ARAJIGA, KAYOKO HAOO CAFCL

11 months ago

Popular News

  • KIINI DABI KARIAKOO KUPIGWA ZANZIBAR

    KIINI DABI KARIAKOO KUPIGWA ZANZIBAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TAMU, CHUNGU DABI YA K’KOO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AKUTANA NA VIONGOZI WA TEC

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AWAPA RAHA VIGOGO USHIRIKA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • BILIONI 30/- KUJENGA UWANJA WA KISASA SIMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?