• ePaper
Sunday, November 16, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

DK. NCHIMBI AAHIDI HUDUMA ZA AFYA KWA WATANZANIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 21, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. NCHIMBI AAHIDI HUDUMA ZA AFYA KWA WATANZANIA

Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. Emmanuel Nchimbi

0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NJUMAI NGOTA,

Songwe

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema iwapo kitapewa ridhaa ya kuendelea kuongoza nchi, kitahakikisha huduma za afya, zinapatikana kwa kila Mtanzania ndani ya umbali wa kilometa tano kutoka mahali anapoishi.

Ahadi hiyo, ilitolewa katika mkutano wa kampeni uliofanyika Chitete, Jimbo la Momba, mkoani Songwe na Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. Emmanuel Nchimbi, alipohutubia mamia ya wananchi waliokusanyika, kumsikiliza akinadi Ilani ya Uchaguzi ya Chama ya mwaka 2025-2030 na kuelezea utekelezaji wa Ilani ya mwaka 2020-2025.

Dk. Nchimbi, alisema katika kipindi cha miaka mitano ijayo, serikali ya CCM, itaendelea kusogeza huduma muhimu za kijamii kwa wananchi, hasa afya ambazo ni haki ya msingi ya kila Mtanzania.

“Tunataka kila Mtanzania awe na uhakika wa huduma ya afya ndani ya kilometa tano kutoka eneo analoishi.

“Pia, Serikali ya CCM katika miaka mitano ijayo inakwenda kuanzisha utaratibu wa bima ya afya kwa Watanzania wote.

“Tunataka ndani ya miaka mitano huduma ya afya ya kila Mtanzania pamoja kuimarika, apate huduma hiyo karibu zaidi,”alisema.

MIUNDOMBINU YAAFYA KUIMARISHWA

Akieleza mikakati ya kuboresha miundombinu ya afya katika Jimbo la Momba, Dk. Nchimbi, alisema serikali ya CCM, itakamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Momba kwa viwango vya kisasa, kujenga vituo vya afya vinne, zahanati 12 na nyumba 24 za watumishi wa sekta hiyo.

ELIMU BILA MALIPO

Katika sekta ya elimu, Dk. Nchimbi, alisema serikali ya CCM, itaendeleza utaratibu wa elimu bila malipo kuanzia chekechea hadi kidato cha sita, huku ikiongeza madarasa mapya na miundombinu bora ya kujifunzia.

“Tutajenga madarasa 104 katika shule za msingi na sekondari,  tuna mpango wa kujenga maabara 51 za kisasa, kuwajengea watoto wetu uwezo wa kisayansi na kiteknolojia,” alisema.

KILIMO

Kwa upande wa sekta ya kilimo, ambayo ndiyo uti wa mgongo wa wananchi wengi wa Momba na Mkoa wa Songwe, Dk. Nchimbi, alisema serikali ya CCM, itaongeza ruzuku ya mbolea, mbegu na kuhakikisha zinatolewa kwa wakati na ubora wa hali ya juu.

UFUGAJI

Akizungumzia sekta ya ufugaji, aliahidi kujengwa majosho saba, minada minne na machinjio manne, kuinua maisha ya wafugaji na kuongeza thamani ya mifugo yao.
Dk. Nchimbi, alisema katika sekta ya barabara, wanakusudia kujenga kwa kiwango cha lami, changarawe na ujenzi wa madaraja mbalimbali, kurahisisha usafirishaji wa watu na bidhaa vijijini na mijini.

Kuhusu huduma ya maji, Dk. Nchimbi, alisema katika miaka mitano ijayo, wakipewa ridhaa ya kuongoza, wataendeleza miradi mikubwa ya maji, kwa lengo la kuongeza upatikanaji huduma hiyo, kutoka asilimia 44 hadi asilimia 80, ndani ya jimbo hilo.

Katika mkutano huo, Dk. Nchimbi, alimwombea kura Mgombea Urais wa CCM, Rais Dk. Samia, wagombea ubunge na udiwani wanaotokana na Chama.
Dk. Nchimbi, aliwasisitiza wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura Oktoba 29, mwaka huu, kwa kukichagua Chama kwa ushindi wa kishindo

CONDESTER SICHALWE

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Momba kwa tiketi ya CCM, Condester Sichalwe, aliwahimiza wananchi kuendelea kuiamini CCM kwa kuangalia utekelezaji mkubwa wa miradi ya maendeleo iliyofanyika katika kipindi cha miaka minne na nusu chini ya uongozi wa Dk. Samia.
“CCM ni Chama chenye uwezo, sera madhubuti, na dhamira ya dhati ya kuwaletea wananchi maendeleo ya kweli. Tunaomba kura zenu kwa Dk. Samia, wabunge na madiwani wote,” alisema.

CECILIA PARESO

Kada wa CCM, Cecilia Pareso, aliwahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi huo, huku akisisitiza umuhimu wa kupiga kura kwa usahihi, kwa kuwachagua wagombea wote wa CCM.
“Tupige kura zetu kwa alama ya tiki katika alama ya jembe na nyundo,  tuendelee na safari ya maendeleo iliyoanza,” alisema.

Previous Post

DK. SAMIA AWAONYA WATU WENYE NIA OVU

Next Post

KAPIGENI KURA, NCHI SHWARI – DK. SAMIA

Next Post
KAPIGENI KURA, NCHI SHWARI – DK. SAMIA

KAPIGENI KURA, NCHI SHWARI - DK. SAMIA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. NCHIMBI : DK. SAMIA KIONGOZI WA MAJAWABU

DK. NCHIMBI : DK. SAMIA KIONGOZI WA MAJAWABU

1 month ago
DK. SAMIA AWAONYA WATU WENYE NIA OVU

DK. SAMIA AWAONYA WATU WENYE NIA OVU

4 weeks ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.