• ePaper
Saturday, November 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Burudani

YANGA , SILVER NI MECHI YA KISASI NA HESHIMA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 25, 2025
in Burudani, Habari, Kimataifa, Michezo
0
YANGA , SILVER NI MECHI YA KISASI NA HESHIMA
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na  NASRA KITANA

WAKATI kikosi cha timu ya Yanga kikitarajiwa kushuka dimbani leo kumenyana na Silver Strikers ya Malawi, kaimu kocha Mkuu wa Yanga, Patrick Mabedi amesema ushindi dhidi ya Silver Strickers ni muhimu, kuhakikisha timu inatinga hatua ya makundi katika Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF), mwaka huu.

Yanga leo itashuka dimbani katika mchezo wake wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Silver utakaochezwa katika Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam saa 11:00 jioni.

Timu hiyo itaingia katika mchezo huo ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza bao 1-0 katika mchezo wake wa kwanza uliochezwa nchini Malawi, hivyo Yanga anahitaji ushindi kutinga hatua inayofuata.

Akizungumza jijini Dar es Salaam,jana, Mabedi alisema mchezo huo ni muhimu kwa Yanga kushinda na kuwapa furaha mashabiki.

“Yanga ni klabu kubwa ina wachezaji wenye uwezo mkubwa wa kuyapindua matokeo ya kufungwa ugenini na kushinda nyumbani hivyo naamini watafuata kile ambacho nimewafundisha katika uwanja wa mazoezi kuhakikisha tunafanya vizuri,” alisema Mabedi.

Kocha huyo alisema kuwa baada ya kutua nchini Jumatatu wakitokea Malawi, walianza mazoezi Jumanne na kufanyia kazi kasoro zilizojitokeza katika pambano la kwanza na wapo tayari kukabiliana na wapinzani wao.

Kocha huyo alifafanua kuwa mpira wa miguu kila mechi ina presha yake, lakini hilo halimpi tabu kwa sababu ametoka katika timu yenye presha, ana imani kila kitu kitaenda sawa.

Kocha wa Silver Strickers, Etson Kadenge amesema anafahamu anakutana na Yanga yenye wachezaji bora, lakini kwa upande wao wapo tayari kumalizia dakika 90 za uamuzi wa kufuzu hatua ya makundi na kwamba anatarajia mchezo mzuri na wa ushindani.

“Wachezaji wangu wapo tayari na wameahidi kutumia dakika 90 kushindana na Yanga kupata nafasi ya kufuzu hatua inayofuata wanatambua wanakutana na wapinzani bora ambao pia wanataka matokeo ili kutinga hatua inayofuata,” alisema Kadenge.

Nyota wa Yanga, Dikson Job alisema kuwa kama wachezaji wamejipanga kuhakikisha wanapambana kwa jasho na damu ili kupata ushindi.

“Sisi tupo tayari kwa ajili ya mchezo na tunatambua umuhimu wa mchezo huu, tutahakikisha tunapata ushindi, niwambie tu mashabiki na wapenzi wa Yanga wanatakiwa kutupa sapoti ya kutosha tufikie malengo ya kutinga hatua ya makundi,” alisema Job.

Wakati huo huo, Ofisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe alisema kuelekea katika mchezo huo ambao hautakuwa na kiingilio mageti yatafunguliwa saa nne asubuhi na kufungwa saa nane na nusu mchana.

Alisema kuwa sababu kubwa ya kupanga muda huo wa mashabiki kuingia uwanjani ni kuepusha msongamano wa watu pamoja na kuwapa nafasi timu kuingia bila ya shida yeyote.

“Tumekaa kikao na wenzetu wa ulinzi na usalama hivyo tumekubaliana mageti yatafungulia rasmi saa nne kamili asubuhi na kufungwa saa nane na nusu mchana hiyo yote kuepusha msongomano wa watu,” alisema Kamwe.

MCHEZO MWINGINE

Wakati Yanga ikishuka dimbani kumenyana na Silver katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, timu ya Singida Black Stars nayo itashuka dimbani katika mchezo wake wa marudiano Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Flambeau ya Burundi.

Singida Black Stars inatarajiwa kucheza mchezo wake huo wa marudiano katika Uwanja wa Azam Complex, Chamanzi saa 1:00 usiku huku ikiwa na kumbukumbu ya sare ya bao 1-1 katika mchezo wake wa kwanza.

Kocha wa timu hiyo, Miguel Gamondi alisema wamejipanga vizuri kuhakikisha wanapata ushindi katika mchezo huo na kutinga hatua ya makundi.

“Tunatakiwa kushinda au kupata sare katika mchezo wetu huo, tumejipanga vizuri kuhakikisha tunapata ushindi na kusonga mbele hatua inayofuata,” alisema Gamondi.

Previous Post

CCM INAHESHIMU HAKI ZA BINADAMU – WASIRA

Next Post

WAKUU WA VYOMBO VYA HABARI NA WAHARIRI WAANDAMIZI NCHINI, WATOA MAAZIMIO WATANZANIA KUTUNZA AMANI

Next Post
WAKUU WA VYOMBO VYA HABARI NA WAHARIRI WAANDAMIZI NCHINI, WATOA MAAZIMIO WATANZANIA KUTUNZA AMANI

WAKUU WA VYOMBO VYA HABARI NA WAHARIRI WAANDAMIZI NCHINI, WATOA MAAZIMIO WATANZANIA KUTUNZA AMANI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWINYI ATANGAZA NEEMA WAZEE ZANZIBAR

DK. MWINYI ATANGAZA NEEMA WAZEE ZANZIBAR

2 months ago
CHAMA MENO NJE SINGIDA BLACK STARS

CHAMA MENO NJE SINGIDA BLACK STARS

2 months ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.