• ePaper
Saturday, November 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Burudani

SIMBA, NSINGIZINI BALAA ZITO CAFCL

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 26, 2025
in Burudani, Habari, Kimataifa, Michezo
0
SIMBA, NSINGIZINI BALAA ZITO CAFCL
0
SHARES
16
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

SAA kadhaa kabla ya kuvaana na Nsingizini Hotspurs ya Eswatini katika mechi ya marudiano ya hatua ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL), benchi la ufundi la Simba, limesema linahitaji timu yake kupata ushindi wa mabao mengi leo.

Simba itachuana na Nsingizini Hotspurs saa 11:00 jioni katika mchezo utakaopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Katika mtanange huo, Simba itaingia na mtaji wa mabao 3-0 iliyoupata katika mchezo wa kwanza uliopigwa nchini Eswatini.

Akizungumza Dar es Salaam, Kocha Msaidizi wa Simba, Selemani Matola, amesema timu yao imejipanga vyema kuhakikisha inapata ushindi mnono katika mtanange huo.

Matola alisema anajua hautakuwa mchezo mwepesi kwani kila timu inahitaji ushindi lakini watahakikisha wanafanya kila linalowezekana kuibuka na ushindi kujihakikishia nafasi ya kutinga makundi.

“Ni kweli tuna uzoefu mkubwa katika michuano hii lakini hatutaki kurudia kile kilichowahi kutukuta misimu kadhaa nyuma, hii ni mechi nyingine yenye uhitaji mkubwa kama ilivyokuwa ya ugenini,” alisema.

Kocha huyo alisema hana hofu na wachezaji wake kwani wanajua umuhimu wa mchezo huo hivyo watahakikisha wanapanga kikosi bora chenye ushindani mkubwa.

Matola alisema beki wa kikosi hicho, Wilson Nangu aliyepata majeraha mechi ya kwanza yupo fiti kucheza, huku kiungo mshambuliaji, Mohamed Bajaber akiendelea vizuri baada ya kupewa programu maalumu.

Nahodha wa timu hiyo, Shomari Kapombe, alisema pamoja na ushindi walioupata katika mechi ya kwanza ila wao kama wachezaji wamejipanga vizuri kuendeleza kiwango bora zaidi.

“Niwaombe mashabiki wetu wajitokeze kwa wingi kwa sababu mechi za kwanza hawakupata hiyo nafasi, hii ni fursa nyingine nzuri ya kuendelea kuandika historia mpya kwa umoja wetu,” alisema.

Naye kocha wa Nsingizini Hotspurs, Mandla Qhogi, alisema pamoja na kupoteza kwa mabao 3-0 katika mechi ya kwanza, lakini bado wana nafasi ya kurekebisha makosa yaliyojitokeza kupata ushindi katika mtanange wa leo.

“Kabla ya mechi yetu ya kwanza hakuna aliyetarajia pia kama Simba ingeshinda ugenini kwa idadi kubwa ya mabao, hii ni mechi nyingine ngumu ila tutapambana kadri ya uwezo wetu,” alisema Mandla.

Previous Post

MAAGIZO YA DK. MWINYI KWA WATUMISHI Z’BAR

Next Post

DK. NCHIMBI AELEZA MAFANIKIO YA KAMPENI ZA CCM NCHINI

Next Post
DK. NCHIMBI AELEZA MAFANIKIO YA KAMPENI ZA CCM NCHINI

DK. NCHIMBI AELEZA MAFANIKIO YA KAMPENI ZA CCM NCHINI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MAELFU  WAJITOKEZA  KUMSINDIKIZA  MAKONDA  KUCHUKUA  FOMU  ARUSHA

MAELFU WAJITOKEZA KUMSINDIKIZA MAKONDA KUCHUKUA FOMU ARUSHA

3 months ago
WASIRA : MAENDELEO YALIYOPO, UTHIBITISHO WA UONGOZI MAHIRI

WASIRA : MAENDELEO YALIYOPO, UTHIBITISHO WA UONGOZI MAHIRI

2 months ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.