• ePaper
Saturday, November 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

WAKUU WA VYOMBO VYA HABARI NA WAHARIRI WAANDAMIZI NCHINI, WATOA MAAZIMIO WATANZANIA KUTUNZA AMANI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 26, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
WAKUU WA VYOMBO VYA HABARI NA WAHARIRI WAANDAMIZI NCHINI, WATOA MAAZIMIO WATANZANIA KUTUNZA AMANI
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na WAANDISHI WETU 

WAKUU wa Vyombo vya Habari na Wahariri Waandamizi nchini, wametoa maazimio yao kuhusu umuhimu wa kutunza amani kuelekea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu, huku wakiungana na viongozi wa dini na makundi mengine yaliyosisitiza kutunza amani.

Tamko hilo la maazimio lilisomwa kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na  Mkurugenzi Mtendaji wa ITV na Redio One, Joyce Mhavile kwa niaba ya wakuu hao wa vyombo vya habari zaidi ya 20 na Wahariri Waandamizi.

“Sisi Wakuu wa Vyombo vya Habari na Wahariri Waandamizi tuliokutana wiki hii, tunaamini katika kushamiri kwa demokrasia ya vyama vingi.

“Ni dhahiri kuwa vyombo vyetu, vimetoa mchango mkubwa katika kuijenga na kuishamirisha demokrasia ya vyama vingi kwa miongo zaidi ya mitatu sasa,”alinukuu.

Akisoma maazimio mengine, Joyce alisema Watanzania kwa umoja wao, wakatae kuhudhuria karamu ya uchochezi wenye lengo la kuwashawishi kulewa ‘Uwendawazimu wa Kihalaiki’ unaoweza kulisambaratisha Taifa kama ilivyotokea katika mataifa mengine.

“Tanzania imekuwa kisiwa cha amani kwa sababu ya misingi iliyowekwa na waasisi wa taifa letu na utamaduni wa kukaa katika meza ya mazungumzo kumaliza tofauti zetu.

“Na kwa miaka mingi, Tanzania imekuwa ni makazi ya matumaini kwa wakimbizi wanaokimbia machafuko ya kisiasa na vita katika nchi zao.

“Zipo nchi nyingi zikiwemo jirani zetu wa Rwanda na Congo, Sierra Leone, Sudan, Somalia, Liberia, Ivory na nyinginezo ambazo zimebaki na makovu ya “Uwendawazimu wa Kihalaiki” ambayo hata pale amani iliporejea au itakaporejea, bado makovu hayo yataendelea kubaki kama sanamu ya kumbukumbu ya majuto,” alisoma Joyce.

Alieleza, katika siku za hivi karibuni, kumesikika kauli zinazochochea chuki na shari, jambo ambalo haliakisi kabisa utamaduni wa Watanzania.

“Kauli zinazohamasisha wananchi kufanya vurugu, kuchoma vituo vya mafuta, vituo vya polisi na mali nyinginezo, siyo tu ni makosa kisheria, bali ni kauli zisizoakisi Utanzania wetu, zinatakiwa kukemewa na kila Mtanzania,”alisema.

Joyce alieleza kuwa, kwa muda mrefu, vyombo vya habari vimeripoti matukio ya vurugu, uvunjifu wa amani, vita vya wao kwa wao na hata mauaji ya kimbari yaliyotokea katika mataifa ya Afrika, yaliyoathiriwa na siasa chafu na kuingiliwa na maadui wa nje.

Alifafanua kuwa, machafuko hayo, mateso na mauaji ya wananchi wasiokuwa na hatia katika nchi hizo, yalisababishwa na ubinafsi wa vikundi vya wanasiasa walioamua kutumia propaganda za kugawa watu, bila kujali maslahi mapana ya mataifa yao.

Alisisitiza kuwa, mara kwa mara, vyombo vya habari vimeendelea kuripoti na kuandika tahariri pale vyama vya siasa viliposuguana hasa nyakati za uchaguzi na kusababisha vurugu kama ilivyowahi kutokea Zanzibar mwaka 2001 baada ya Uchaguzi Mkuu.

Alieleza kuwa, demokrasia ya taifa bado ni change, inahitaji muda, kwani ni mchakato endelevu, unaotakiwa kujengwa kila siku kwa kuhakikisha kila hatua inalindwa na wadau wote.

Alisema ni vyema wanachi kukumbuka kuwa, Tanzania ilipata uhuru wake kwa jitihada za majadiliano, mazungumzo na hoja za wanasiasa, wakipingana bila kupigana, hivyo Watanzania wana wajibu wa kuendelea kujenga demokrasia kwa njia hizo za mazungumzo na siyo vinginevyo.

 Awali akimkaribisha msomaji wa waazimio hayo, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Utangazaji (TBC), Ayoub Ryoba, alisisitiza vyombo vya habari kuendelea kuripoti maazimio hayo yenye msingi wa kudumisha amani nchini.

Alisema vyombo vya habari vina mchango mkubwa kwa jamii hususan kuhamasisha amani na utulivu katika jamii kuwepo maendeleo zaidi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Deodatus Balile, alisema maazimio hayo ni ya msingi katika kujenga amani na umoja wa kitaifa kuelekea uchaguzi mkuu.

Previous Post

YANGA , SILVER NI MECHI YA KISASI NA HESHIMA

Next Post

DK. SAMIA AVUTIA MAELFU KILA KONA

Next Post
DK. SAMIA AVUTIA MAELFU KILA KONA

DK. SAMIA AVUTIA MAELFU KILA KONA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MBAPPE AMFIKIA HENRY UFARANSA

MBAPPE AMFIKIA HENRY UFARANSA

2 months ago
DK. SAMIA : TUNATAKA USHINDI WA HESHIMA

DK. SAMIA : TUNATAKA USHINDI WA HESHIMA

2 months ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.