• ePaper
Saturday, November 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

RAIS DK. SAMIA ATOA MAAGIZO KWA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA NCHINI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 3, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa
0
RAIS DK. SAMIA ATOA MAAGIZO KWA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA NCHINI

RAIS na Amiri Jeshi Mkuu, Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

DODOMA

RAIS na Amiri Jeshi Mkuu, Dk. Samia Suluhu Hassan, ameagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha wananchi wanaendelea na shughuli zao kama kawaida kuanzia leo, Novemba 3, 2025, kufuatia machafuko yaliyotokea baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 29 mwaka huu.

Ameonya kuwa waliohusika kuchochea uvunjifu wa amani watachukuliwa hatua kali za kisheria, akisisitiza kuwa vurugu huishia kupimana nguvu.

Akizungumza baada ya kuapishwa kuongoza kwa muhula wa pili katika Serikali ya Awamu ya Sita, Rais Dk. Samia amesema mchakato wa uchaguzi ni wa msimu mmoja tu ndani ya miaka mitano, hivyo maisha lazima yaendelee.

Amesisitiza kuwa jukumu la kujenga taifa ni la Watanzania wote, kwa kuimarisha umoja, upendo na mshikamano.

Rais Dk. Samia amesema matukio ya uvunjifu wa amani yaliyojitokeza katika baadhi ya maeneo nchini hayalingani na utamaduni wa Kitanzania, akibainisha kuwa baadhi ya vijana waliokamatwa wametoka nje ya nchi.

Amezielekeza Kamati za Ulinzi za Kitaifa, Mikoa na Wilaya kuhakikisha hali ya utulivu inarejea mara moja, huku akiwataka Watanzania kuchagua hekima, busara, upendo, uvumilivu na amani badala ya ghadhabu na chuki.

Aidha, amesisitiza kuwa ukuaji wa demokrasia haupimwi kwa matokeo ya uchaguzi pekee bali kwa jinsi taifa linavyoshughulikia masuala yake baada ya uchaguzi.

Ameishukuru jamii ya viongozi wa dini kwa kuhimiza amani na kupongeza viongozi wa mataifa jirani waliohudhuria sherehe za kuapishwa kwake.

Katika halfa hiyo ya uapisho, viongozi kutoka mataifa mbalimbali walihudhuria wakiongozwa na Rais wa Burundi, Evaliste Ndayishimiye na Rais wa Zambia, Haikande Hichilema ambao walipata fursa ya kutoa salamu zao.

Katika salamu zao viongozi hao walimpongeza Rais Dk. Samia kwa ushindi wa kishindo huku wakitoa wito kwa Watanzania kuendeleza kudumisha amani, umoja na mshikamano.

Katika hatua nyingine, Rais Dk. Samia amempongeza Dk. Hussein Ali Mwinyi kwa kuchaguliwa kuendelea kuongoza Zanzibar, na kuvipongeza vyama 17 vilivyosimamisha wagombea wa urais kwa kuonesha ukomavu wa kisiasa na kuendesha kampeni za hoja.

Previous Post

WATANZANIA 37,647,235 KUPIGA KURA LEO

Next Post

DK. SAMIA AAPISHWA JIJINI DODOMA

Next Post
DK. SAMIA AAPISHWA JIJINI DODOMA

DK. SAMIA AAPISHWA JIJINI DODOMA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. NCHIMBI AMTAJA DK. SAMIA UJENZI BANDARI YA KWALA

DK. NCHIMBI AMTAJA DK. SAMIA UJENZI BANDARI YA KWALA

1 month ago
LIVERPOOL, ARSENAL KAZI IPO

LIVERPOOL, ARSENAL KAZI IPO

3 months ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.