• ePaper
Saturday, November 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

CHAMA CHA MAWAKILI WA SERIKALI CHAMPONGEZA JOHARI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 6, 2025
in Habari, Kitaifa
0
CHAMA CHA MAWAKILI WA SERIKALI CHAMPONGEZA JOHARI
0
SHARES
1
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

CHAMA cha Mawakili wa Serikali (GAT) kimempongeza, Hamza Johari kwa kuteuliwa tena kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kikiuelezea uteuzi huo kuwa ni kielelezo cha ubobezi na uadilifu wake katika taaluma ya sheria.

Kwa mujibu wa taarifa ya chama hicho, uteuzi huo pia unaendana na matakwa ya Ibara ya 59 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inayotaka Mwanasheria Mkuu awe na sifa za uwakili kwa angalau miaka 15.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa Johari ana uzoefu wa zaidi ya miaka 20 katika utumishi wa umma, hususan katika masuala ya mikataba, sheria za anga, bahari na udhibiti.

Ana Shahada ya Sheria (LL.B) na Shahada ya Uzamili (LL.M) katika Sheria za Kimataifa kutoka Chuo Kikuu cha Kiev, Ukraine, pamoja na cheti cha Uongozi na Usimamizi kutoka Chuo cha Utawala cha India.

Johari amewahi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania kwa kipindi cha miaka tisa, na pia amehudumu kama Mwenyekiti wa CANSO Afrika, CASSOA na kamati mbalimbali za kisheria za kikanda na kimataifa.

Aidha, amewahi kufundisha katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Mzumbe na Chuo Kikuu cha Alexandria nchini Misri.

Mbali na hayo, Johari amekuwa Mlezi wa Chama cha Mawakili wa Serikali, Mjumbe wa Tume ya Utumishi wa Mahakama, na Mwenyekiti wa timu za majadiliano ya Serikali katika mikataba mikubwa ya kimataifa ikiwemo ya DP World (U.A.E) na Bandari ya Adani (India).

Pia ameshiriki katika timu za kitaifa za kutatua migogoro ya mipaka na majadiliano ya miradi ya kimkakati ya kitaifa.

Johari ni Mmakonde, mzaliwa wa Wilaya ya Mtwara Vijijini, Tarafa ya Ziwani, Kata ya Nalingu.

Previous Post

WATALII WAENDELEA KUFURIKA NGORONGORO, WASIFU AMANI NA VIVUTIO VYA TANZANIA

Next Post

GAMONDI AMPA MAJUKUMU KELVIN JOHN

Next Post
GAMONDI AMPA MAJUKUMU KELVIN JOHN

GAMONDI AMPA MAJUKUMU KELVIN JOHN

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MAELFU WAFURIKA UZINDUZI WA KAMPENI ZA CCM DAR

MAELFU WAFURIKA UZINDUZI WA KAMPENI ZA CCM DAR

3 months ago
DK. SAMIA, AHIMIZA WAKULIMA WAJISAJILI KATIKA MFUMO WA RUZUKU YA MBEGU, PEMBEJEO

DK. SAMIA, AHIMIZA WAKULIMA WAJISAJILI KATIKA MFUMO WA RUZUKU YA MBEGU, PEMBEJEO

2 months ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.