• ePaper
Thursday, June 4, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

WATALII WAENDELEA KUFURIKA NGORONGORO, WASIFU AMANI NA VIVUTIO VYA TANZANIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 6, 2025
in Habari, Kitaifa
0
WATALII WAENDELEA KUFURIKA NGORONGORO, WASIFU AMANI NA VIVUTIO VYA TANZANIA
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na LILIAN JOEL,
ARUSHA

WATALII kutoka mataifa mbalimbali duniani wanaotembelea Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) wameendelea kufanya shughuli zao za utalii kwa amani, usalama na utulivu, huku wakifurahia vivutio lukuki vilivyopo katika hifadhi hiyo maarufu duniani.

Akizungumza katika lango kuu la Laoduare, Ofisa Uhifadhi Mkuu wa Idara ya Huduma za Utalii na Masoko wa NCAA, Peter Makutian, amesema katika kipindi chote cha uchaguzi mkuu wa Tanzania hadi kufikia Novemba 5, 2025, jumla ya wageni takribani 1,200 kutoka mataifa mbalimbali wametembelea hifadhi hiyo na kushiriki shughuli za utalii.

“Hifadhi ya Ngorongoro tunaendelea kupokea watalii wa ndani na wa kimataifa. Kwa sasa tuko katika msimu wa wastani, lakini tunaamini kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka idadi ya watalii itaongezeka zaidi,” amesema Makutian.

Kwa upande wake, Isabella Jerónimol, mtalii kutoka Colombia aliyefika nchini akiwa na familia ya watu 26, alisema walichagua kutembelea Tanzania kwa kuvutiwa na hali ya amani, ukarimu wa wananchi na utajiri wa vivutio vya asili.

“Safari hii tuliipanga kwa muda mrefu. Tumefurahi kufika Tanzania, nchi yenye vivutio vingi vya kipekee. Tulichagua Hifadhi ya Ngorongoro kwa sababu ni sehemu yenye historia kubwa na mandhari ya kuvutia. Tulikaribishwa vizuri na kupewa maelezo kuhusu wanyama na urithi wa hifadhi hii,” amesema Jerónimol.

Previous Post

RAIS DK. SAMIA APOKEA UJUMBE WA RAIS PUTIN

Next Post

CHAMA CHA MAWAKILI WA SERIKALI CHAMPONGEZA JOHARI

Next Post
CHAMA CHA MAWAKILI WA SERIKALI CHAMPONGEZA JOHARI

CHAMA CHA MAWAKILI WA SERIKALI CHAMPONGEZA JOHARI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA AVUNJA NGOME YA UPINZANI MKOANI LINDI

DK. SAMIA AVUNJA NGOME YA UPINZANI MKOANI LINDI

8 months ago
MANNY PACQUIAO KUTUA BONGO NA MAMBO MAWILI

MANNY PACQUIAO KUTUA BONGO NA MAMBO MAWILI

5 months ago

Popular News

  • TANZANIA, RUSSIA KUPAISHA UCHUMI

    TANZANIA, RUSSIA KUPAISHA UCHUMI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ASANTE SERENGETI BOYS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?