• ePaper
Saturday, November 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

WAJUMBE WAJAWA MATUMAINI RAIS MWINYI AKIHUTUBIA BARAZA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 10, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa
0
WAJUMBE WAJAWA MATUMAINI RAIS MWINYI AKIHUTUBIA BARAZA

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi

0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na HANIFA RAMADHANI,
Zanzibar 

BAADHI ya Wajumbe wa Baraza la 11 la Wawakilishi Zanzibar (BWZ), wamesema wanatarajia kusikia hotuba yenye mikakati madhubuti na Dira ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2025/2030.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, leo anatarajiwa kulihutubia baraza hilo.

Wakizungumza na UHURU kwa nyakati tofauti, wajumbe hao, walisema hotuba za Dk. Mwinyi, mara zote huwa ni fupi, zenye uzito na kujaa mipango inayotekelezeka.

Hivyo, wanatarajia ujumbe wenye msukumo wa maendeleo na mwongozo wa awamu ya pili ya uongozi wake.

MWAKILISHI JIMBO LA KIJINI

Mwakilishi wa Jimbo la Kijini, Badria Atai Masaoud, alisema wanasubiri kwa hamu kusikia namna Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), itakavyotekeleza ilani mpya ya CCM kwa kipindi kijacho, ambayo imeweka vipaumbele 10 muhimu vilivyotangazwa na Rais Mwinyi wakati wa kampeni.

“Tunatarajia kusikia mkakati mahsusi wa namna ambavyo vipaumbele hivyo 10, vitafanyiwa kazi kwa ufanisi. 

“Rais Dk. Mwinyi, siku zote amekuwa akisisitiza utawala bora, uwajibikaji na uadilifu kwa viongozi, hivyo tunatarajia kuona msisitizo zaidi katika maeneo hayo,” alisema Badria.

Aliongeza kuwa jukumu lao kama wawakilishi ni kuhakikisha wananchi wanasimamiwa ipasavyo, wanapata huduma bora na kwamba, mipango yote ya maendeleo inayotangazwa na serikali, inatekelezwa kikamilifu.

“Sisi tupo tayari kushirikiana na Rais (Dk. Mwinyi) kwa karibu katika kuhakikisha ilani ya CCM, inatekelezwa kwa vitendo. “Wananchi wametupa dhamana, hivyo ni wajibu wetu kuwasemea na kuwasimamia katika kufanikisha malengo ya maendeleo ya nchi yetu,” alisisitiza.

MWAKILISHI JIMBO LA JANG’OMBE

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Jimbo la Jang’ombe, Ali Abdulghulam Hussein, alisema hotuba ya Rais Mwinyi, itakuwa dira ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuendeleza ahadi ambazo alizitoa wakati wa kampeni.

Alisema Dk. Mwinyi ni kiongozi mwenye maono makubwa na dhamira ya dhati ya kuwaletea wananchi maendeleo endelevu, hivyo hotuba yake, itatarajiwa kutoa mwongozo wa wazi wa kuimarisha sekta mbalimbali.

Aidha, wajumbe hao, walisema kipindi cha pili cha uongozi wa Dk. Mwinyi, kinatarajiwa kuwa cha kasi zaidi katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati, hususan inayolenga kuimarisha uchumi wa visiwa hivyo.

Previous Post

WASOMI, VIONGOZI WA DINI WAGUSIA UZALENDO, AMANI  

Next Post

UVCCM YAWAPA POLE WALIOPATA MADHILA

Next Post
UVCCM YAWAPA POLE WALIOPATA MADHILA

UVCCM YAWAPA POLE WALIOPATA MADHILA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWINYI ATANGAZA NEEMA WAZEE ZANZIBAR

DK. MWINYI ATANGAZA NEEMA WAZEE ZANZIBAR

2 months ago
MAJALIWA : MRADI GESI YA LNG KUIKOMBOA LINDI KIUCHUMI

MAJALIWA : MRADI GESI YA LNG KUIKOMBOA LINDI KIUCHUMI

2 months ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.