• ePaper
Wednesday, April 29, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Biashara

MAJALIWA : MRADI GESI YA LNG KUIKOMBOA LINDI KIUCHUMI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 27, 2025
in Biashara, Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
MAJALIWA : MRADI GESI YA LNG KUIKOMBOA LINDI KIUCHUMI
0
SHARES
13
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na Mussa Yusuph,

Lindi

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, amesema utekelezaji wa mradi wa gesi ya LNG unaotarajiwa kufanyika mkoani Lindi ni ukombozi wa kiuchumi katika mkoa huo na Taifa.

Kutokana na hilo, Majaliwa ametoa wito kwa wananchi mkoani Lindi kumpigia kura Mgombea Urais wa CCM, Dk. Samia Suluhu Hassan akamilishe taratibu zilizobaki kutekeleza mradi huo wa kimkakati.

Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Ilulu mkoani Lindi, Majaliwa alisisitiza kwamba mradi huo umewekwa katika Ilani ya CCM ya mwaka 2025–2030, jambo linaloonesha dhamira ya Chama kuhakikisha wananchi wa Lindi na Watanzania wananufaika.

“Ilani hii inakuja kutukomboa na kufungua milango ya mkoa wetu. Mradi mkubwa wa LNG unakuja kutekelezwa hapa Lindi. Kwa kuwa utekelezaji huu upo kwenye Ilani ya CCM 2025–30, basi ni juu yetu wana Lindi kumpigia kura, Dk. Samia ili akamilishe taratibu zilizobaki,” alisema.

Akizungumzia ujenzi wa kiwanja cha ndege katika mkoa huo, alisema uwanja huo utakuwa wa kisasa wenye uwezo wa kuhudumia ndege mbalimbali.

“Kiwanja chetu cha ndege kina njia kuu tatu tofauti na viwanja vyote vya ndege Tanzania. Unaweza kutua kutoka popote, jambo linalokwenda sambamba na mradi unaokuja wa LNG. Ilani hii inakuja kutukomboa na kufungua milango ya mkoa wetu,” alisema.

Alibainisha kuwa ilani hiyo pia inatilia mkazo uhifadhi wa mazingira kwa kujenga ukuta maalumu utakaosaidia kuzuia mmomonyoko katika fukwe za Lindi.

Previous Post

DK. SAMIA AVUNJA NGOME YA UPINZANI MKOANI LINDI

Next Post

YANGA, SINGIDA, MLANDEGE MZIGONI TENA KIMATAIFA

Next Post
YANGA, SINGIDA, MLANDEGE MZIGONI TENA KIMATAIFA

YANGA, SINGIDA, MLANDEGE MZIGONI TENA KIMATAIFA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SERIKALI ZANZIBAR YAONGEZA TEKNOLOJIA KUDHIBITI MAKOSA YA BARABARANI

SERIKALI ZANZIBAR YAONGEZA TEKNOLOJIA KUDHIBITI MAKOSA YA BARABARANI

4 months ago
TANZANIA NA CHINA ZAKUBALIANA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIMKAKATI

TANZANIA NA CHINA ZAKUBALIANA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIMKAKATI

4 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?