• ePaper
Tuesday, July 14, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Biashara

MAJALIWA : MRADI GESI YA LNG KUIKOMBOA LINDI KIUCHUMI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 27, 2025
in Biashara, Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
MAJALIWA : MRADI GESI YA LNG KUIKOMBOA LINDI KIUCHUMI
0
SHARES
14
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na Mussa Yusuph,

Lindi

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, amesema utekelezaji wa mradi wa gesi ya LNG unaotarajiwa kufanyika mkoani Lindi ni ukombozi wa kiuchumi katika mkoa huo na Taifa.

Kutokana na hilo, Majaliwa ametoa wito kwa wananchi mkoani Lindi kumpigia kura Mgombea Urais wa CCM, Dk. Samia Suluhu Hassan akamilishe taratibu zilizobaki kutekeleza mradi huo wa kimkakati.

Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Ilulu mkoani Lindi, Majaliwa alisisitiza kwamba mradi huo umewekwa katika Ilani ya CCM ya mwaka 2025–2030, jambo linaloonesha dhamira ya Chama kuhakikisha wananchi wa Lindi na Watanzania wananufaika.

“Ilani hii inakuja kutukomboa na kufungua milango ya mkoa wetu. Mradi mkubwa wa LNG unakuja kutekelezwa hapa Lindi. Kwa kuwa utekelezaji huu upo kwenye Ilani ya CCM 2025–30, basi ni juu yetu wana Lindi kumpigia kura, Dk. Samia ili akamilishe taratibu zilizobaki,” alisema.

Akizungumzia ujenzi wa kiwanja cha ndege katika mkoa huo, alisema uwanja huo utakuwa wa kisasa wenye uwezo wa kuhudumia ndege mbalimbali.

“Kiwanja chetu cha ndege kina njia kuu tatu tofauti na viwanja vyote vya ndege Tanzania. Unaweza kutua kutoka popote, jambo linalokwenda sambamba na mradi unaokuja wa LNG. Ilani hii inakuja kutukomboa na kufungua milango ya mkoa wetu,” alisema.

Alibainisha kuwa ilani hiyo pia inatilia mkazo uhifadhi wa mazingira kwa kujenga ukuta maalumu utakaosaidia kuzuia mmomonyoko katika fukwe za Lindi.

Previous Post

DK. SAMIA AVUNJA NGOME YA UPINZANI MKOANI LINDI

Next Post

YANGA, SINGIDA, MLANDEGE MZIGONI TENA KIMATAIFA

Next Post
YANGA, SINGIDA, MLANDEGE MZIGONI TENA KIMATAIFA

YANGA, SINGIDA, MLANDEGE MZIGONI TENA KIMATAIFA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RAIS DK. SAMIA ATIA NENO BEI MAFUTA

RAIS DK. SAMIA ATIA NENO BEI MAFUTA

2 months ago
MATOLA AWAFUNGIA KAZI WASHAMBULIAJI SIMBA SC

MATOLA AWAFUNGIA KAZI WASHAMBULIAJI SIMBA SC

7 months ago

Popular News

  • CHINA YAZIDI KUSISITIZA USHIRIKIANO KWA AFRIKA

    CHINA YAZIDI KUSISITIZA USHIRIKIANO KWA AFRIKA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, SINGIDA BS MACHO ‘KAGAME CUP’

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI : TAMKO LA PAMOJA CCM NA ACT-WAZALENDO LAFUNGUA NJIA YA UTEKELEZAJI WA SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • BIL.8/- KUISUKA AZAM FC

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WADAU WAMGOMEA SAMATTA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?