• ePaper
Sunday, July 26, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DK. SAMIA AVUNJA NGOME YA UPINZANI MKOANI LINDI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 27, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. SAMIA AVUNJA NGOME YA UPINZANI MKOANI LINDI

Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
10
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na Mussa Yusuph,

Lindi

KIMBUNGA cha Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, kimeendelea kushika kasi kwa kusambaratisha ngome mbalimbali za vyama vya upinzani mkoani Lindi.

Hali hiyo imeendelea kudhihirika katika mikutano ya kampeni za Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu, ambapo vigogo kutoka vyama hivyo, waliamua kujiunga CCM, huku wakieleza kuguswa utekelezaji wa miradi ya maendeleo na mazuri yaliyopo katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM (2025–2030).

katika mkutano wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Ilulu mkoani Lindi, wanachama kutoka vyama vya CHADEMA, CHAUMMA na CUF wamerejesha kadi za vyama hivyo kisha kupokelewa CCM mbele ya Mwenyekiti wa Chama Taifa, Dk. Samia.

Akizungumza katika mkutano huo, aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Lindi na Makamu Mwenyekiti Kanda ya Kusini, Salum Bar’wan, alisema ameguswa na Ilani ya CCM 2025–2030, ikiwemo dhamira ya kuufungua Mkoa wa Lindi kupitia uboreshaji wa miundombinu ya barabara, ujenzi wa uwanja wa ndege na utekelezaji mradi wa kimkakati wa gesi asilia (LNG).

Alisema ameamua kujiunga CCM kwa sababu kimeonesha dira ya maendeleo ya kweli, huku akiwataka wananchi wa Lindi kujitokeza kwa wingi kumpa kura Dk. Samia.

Naye, Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mchinga kupitia CHAUMMA, Yusuph Issa Tamba, alisema amefikia uamuzi huo kwa ridhaa yake mwenyewe bila kushawishiwa na mtu yeyote.

“Natuma salamu kwa chama changu wametuma ujumbe wa vitisho, waambieni mimi siyo mtoto mdogo, sitishiki. Huku ndiyo nyumbani, mitano tena. Nimerudi nyumbani, naomba mnipokee,” alisema.

Tamba aliahidi kushirikiana na CCM kuhakikisha ushindi wa kishindo katika Uchaguzi Mkuu wa 2025 na kuwataka  wananchi wa Mchinga na Mkoa wa Lindi kwa ujumla kuunga mkono maendeleo yanayoletwa na Dk. Samia.

Previous Post

DK. SAMIA KULETA TEKNOLOJIA YA KILIMO

Next Post

MAJALIWA : MRADI GESI YA LNG KUIKOMBOA LINDI KIUCHUMI

Next Post
MAJALIWA : MRADI GESI YA LNG KUIKOMBOA LINDI KIUCHUMI

MAJALIWA : MRADI GESI YA LNG KUIKOMBOA LINDI KIUCHUMI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

‘MLIOGHUSHI AKAUNTI ZA JKT MITANDOANI ZIFUTENI HARAKA’

‘MLIOGHUSHI AKAUNTI ZA JKT MITANDOANI ZIFUTENI HARAKA’

9 months ago
NONDO ZA RAIS SAMIA AKIWAAPISHA VIONGOZI

NONDO ZA RAIS SAMIA AKIWAAPISHA VIONGOZI

6 months ago

Popular News

  • KATIBA MSINGI WA HAKI – DK. NCHIMBI

    KATIBA MSINGI WA HAKI – DK. NCHIMBI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MABASI YA UMEME REKODI ZANZIBAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KOCHA AIPA JEURI YANGA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWALIMU, GUEYE WAPO SIMBA SANA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI ASHTUKIA ‘USANII’ WA WACHIMBAJI MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?