• ePaper
Sunday, November 16, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Burudani

KOCHA GAMONDI AJIVUNIA TAIFA STARS

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 12, 2025
in Burudani, Kitaifa, Michezo
0
KOCHA GAMONDI AJIVUNIA TAIFA STARS

KAIMU Kocha Mkuu wa timu hiyo, Miguel Gamondi

0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

WAKATI kikosi cha timu ya Taifa Stars kikianza mazoezi rasmi kwa maandalizi ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Kuwait, Kaimu Kocha Mkuu wa timu hiyo, Miguel Gamondi amesema kuwa anajivunia kikosi alichokuwa nacho kuwa kitaienda kufanya vizuri.

Gamond ambaye ni Kocha wa Singida Black Stars, ameiongoza Stars kwa mara ya kwanza katika maandalizi hayo baada ya kurithi mikoba ya aliyekuwa mtangulizi wake Hemed Suleiman ‘Morocco’.

Stars inatarajiwa kushuka dimbani Novemba 15, mwaka huu katika mchezo wa kirafiki Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa (FIFA) dhidi ya Kuwait utakaochezwa Uwanja wa Al Salam jijini Cairo nchini Misri kuanzia saa 1:00 usiku.

Akizungumza baada ya mazoezi yake ya kwanza alisema anajivunia wachezaji wote aliowaita kikosini na kwamba ana imani kila mmoja atatimiza majukumu yake katika mchezo huo.

Alisema kutokana na wachezaji wote kuwa wanazitumikia klabu zao, hivyo anaamini wapo fiti na atafanya uboreshaji mdogo ili kuwa na kikosi kitakachompa matokeo chanya.

Alisema kuwa muda ni mchache umekabia wa kufanya maandalizi, ana imani kuwa kila mchezaji aliyenaye kikosini ana uzoefu wa kucheza mechi kubwa.

“Tumeanza mazoezi yetu na nafurahi kuona kila mchezaji yupo fiti na amejipanga vyema, mimi nitarekebisha mapungufu nitakayoyaona ili niweze kuwa na kikosi imara na kitakachofanya vizuri katika mchezo huo muhimu.

“Ninafurahia wachezaji nilionao kikosini kwani wanatoka katika klabu tofauti, hivyo ninaamini tutafikia malengo ya kufanya vyema katika mechi zitakazotukabili,” alisema Gamondi.

Kocha huyo alisema kuwa ana imani kila mchezaji ataonyesha uwezo mkubwa aliokuwa nao na kuipambania timu  kupata ushindi.

Hata hivyo Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Cliford Ndimbo alisema kuwa maandalizi yote ya safari yapo vizuri na leo saa 5 asubuhi kikosi kitaondoka kwenda nchini Misri.

“Maandalizi yote yapo vizuri, timu itaondoka kesho (leo) saa 5 asubuhi kwenda Misri kwa maandalizi ya mwisho ya mchezo huo,” alisema Ndimbo.

Ndimbo alisema Watanzania wanatakiwa kuendelea kuiunga mkono timu yao kila inapocheza ili wachezaji waweze kupata morari ya kutosha ya kufanya vizuri.

Previous Post

SPIKA ZUNGU : NITAZINGATIA HAKI, UWAZI

Next Post

WADAU WA SOKA WAMPONGEZA ZUNGU 

Next Post
WADAU WA SOKA WAMPONGEZA ZUNGU 

WADAU WA SOKA WAMPONGEZA ZUNGU 

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. NCHIMBI AELEZA MKAKATI WA RELI SGR HADI KIGOMA

DK. NCHIMBI AELEZA MKAKATI WA RELI SGR HADI KIGOMA

1 month ago
DK. SAMIA AACHA GUMZO SONGEA AKIAHIDI NEEMA TELE

DK. SAMIA AACHA GUMZO SONGEA AKIAHIDI NEEMA TELE

2 months ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.