• ePaper
Saturday, January 10, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

WANADIPLOMASIA WATAJA FAIDA TANO ZA AMANI NCHINI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 7, 2026
in Habari, Kitaifa
0
WANADIPLOMASIA WATAJA FAIDA TANO ZA AMANI NCHINI
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na IRENE MWASOMOLA

BAADHI ya Wataalamu wa Diplomasia  na Uhusiano wa Kimataifa, wametaja faida  tano za umuhimu wa kudumisha amani nchini, huku wakishauri serikali kuendelea na juhudi za kuimarisha umoja wa kitaifa.

Pia, wameshauri vijana  na wananchi wote kwa ujumla kujiepusha na chuki na propaganda zenye lengo la kuligawa taifa.

FAIDA ZA AMANI

Faida hizo ni pamoja na kuvutia wawekezaji na watalii,  kuchochea maendeleo, kujenga umoja wa kitaifa, kukuza diplomasia, kuongeza fursa za ajira na kukuza shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Akizungumza na UHURU, Mhadhiri  wa Diplomasia kutoka Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dk. Salim Ahmed Salim, Godwin Gonde, alisema uwepo wa amani nchini una mchango mkubwa katika kuvutia wawekezaji wa kigeni kuja kuwekeza hapa nchini , hatua ambayo inaongeza fursa za ajira.

Pia, Gonde alisema amani  ya Tanzania ndio inabeba sura ya nchi kimataifa na ni msingi wa diplomasia ya taifa lolote duniani.

Alisema, uwepo wa amani nchini unasaidia kuwepo uwanda mpana wa kushirikiana na mataifa mbalimbali, hivyo ni wajibu wa kila Mtanzania kuhakikisha tunu hiyo inalindwa .

 “Amani ina mchango mkubwa sana nchini, kwa sababu ndio ina weka mwanya wa nchi yetu  kuwa na mashirikiano na nchi yoyote duniani, amani  ndio inabeba taswira ya taifa mnapokuwa na amani ndio mnawahakikishia wageni usalama hata wakuja kufanya uwekezaji .  

 “Amani ni msingi katika mawanda ya kidiplomasia na mawanda ya mashirikiano ya kimataifa, changamoto tulizopitia (Oktoba 29) ziliweza kutia doa kidogo, lakini bado tuna nafasi ya kufanya juhudi za kuendeleza umoja wa kitaifa,”aliongeza.

Kwa upande wake Mhadhiri kutoka Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dk. Salim Ahmed Salim, Dk. Innocent Shoo, alisema vijana na wananchi  kwa ujumla wana wajibu kulinda tunu ya amani kwa heshima na kujiepusha na propaganda na chuki zinazo chochea kuligawa taifa.

“Vijana wana wajibu wa kutunza amani  kutatua migogoro kwa njia ya utulivu, kujiepusha na chuki na propaganda hatarishi.

“Tukumbuke kwamba amani ndio inaleta wawekezaji, fursa za kazi na maendeleo ya kweli na Tanzania imejenga historia ya utulivu na mshikamano, ni jukumu la kila Mtanzania kuhifadhi na kuendeleza urithi huo,”aliongeza.

Mchambuzi wa Diplomasia na Uhusiano wa Kimataifa kutoka Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dk. Salim Ahmed Salim, Denis Konga, alisema amani endelevu inajengwa kwa ushirikiano wa pamoja, hatua ambayo ina chochea uwepo wa maendeleo katika nyanja mbalimbali za kijamii, kisiasa na kiuchumi.

Aidha, Konga alisema kuna umuhimu mkubwa wa kuwepo kwa maridhiano kwa ajili ya kuwepo kwa mustakabali wa kujenga  taifa moja.

“Ili maendeleo yaendelee kuwepo lazima kuwe na amani endelevu na amani endelevu inajengwa, hata diplomasia ina kuwepo katika maeneo ambayo kunakuwa na utulivu na utengamano,”aliongeza.

Previous Post

TAIFA STARS AFCON 2027 INAWEZEKANA

Next Post

REKODI MPYA ZANZIBAR

Next Post
REKODI MPYA ZANZIBAR

REKODI MPYA ZANZIBAR

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

JELA MIAKA 25 KWA KUSAFIRISHA DAWA ZA KULEVYA

JELA MIAKA 25 KWA KUSAFIRISHA DAWA ZA KULEVYA

2 weeks ago
KIBU DENIS, MANULA WATEMWA STARS

KIBU DENIS, MANULA WATEMWA STARS

4 months ago

Popular News

  • SIMANZI WATOTO WAKIFIA NDANI YA SWIMMING POOL

    SIMANZI WATOTO WAKIFIA NDANI YA SWIMMING POOL

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AONYA WAVURUGA AMANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TANZANIA NA CHINA ZAKUBALIANA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIMKAKATI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MRADI WA UMEMEJUA KISHAPU KULETA MAPINDUZI SEKTA YA NISHATI – MAKAMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KATIBU MKUU CCM AWATAKA WANACHAMA KUSHIRIKI KIKAMILIFU VIKAO VYA MASHINA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?