• ePaper
Monday, January 19, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

TAIFA STARS AFCON 2027 INAWEZEKANA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 7, 2026
in Burudani, Kitaifa, Michezo
0
TAIFA STARS AFCON 2027 INAWEZEKANA
0
SHARES
11
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

WAKATI timu ya taifa ‘Taifa Stars’ ikionyesha kiwango cha kushangaza katika Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka 2025, magwiji wa soka wamesema miamba hiyo inaweza kutikisa katika AFCON mwaka 2027 kama maandalizi yatafanyika mapema na kwa usahihi.

Taifa Stars chini ya Kocha Miguel Gamond iliwashangaza watu wengi Afrika baada ya kuonyesha kiwango bora katika AFCON mwaka huu ikitinga hatua ya 16 bora kwa mara ya kwanza katika historia.

Katika michuano hiyo mikubwa zaidi Afrika, Taifa Stars ilitoka sare dhidi ya Tunisia na Uganda huku ikionyesha ubora ilipochuana na miamba Nigeria na Morocco japokuwa ilipoteza.

Awali, miamba hiyo ilizoeleka ‘kusindikiza’ wenzao katika michuano hiyo ambapo kabla ya AFCON hii, Taifa Stars ilikuwa na rekodi ya kutocheza hatua ya mtoano ikipoteza mechi sita na kutoka sare tatu kati ya tisa ilizocheza hatua ya makundi.

Lakini kutinga mtoano kumeifanya Taifa Stars kuwa moja na timu 16 bora zilizopenya hatua hiyo katika AFCON hii ambayo imekuwa na ushindani mkubwa.

Kiwango hicho kimewafanya magwiji wa soka nchini waliokipiga timu hiyo kuamini kwamba kuna kila sababu ya Stars kutikisa katika AFCON ya mwakani itakayopigwa Tanzania,  Kenya na Uganda.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, mchezaji wa zamani wa Simba na Taifa Stars, Idd Pazi alisema kikosi hicho kina nafasi ya kufanya vizuri katika AFCON 2027 kama kitafanya maandalizi mapema.

“Mwalimu Miguel Gamondi anafaa kupewa mikoba rasmi, pia tumeona wachezaji wakipambana kwa ari ya juu kuhakikisha wanapata matokeo mazuri katika kila mchezo, nafikiri hakuna cha kutusimamisha kufanya vyema kama tutakuwa na maandalizi bora,” alisema.

Kiungo wa zamani wa Simba, Zamoyoni Mogella, alisema Taifa Stars ya sasa ni tofauti ya awali, ubora wake sasa umeongezeka na anaamini utazidi kufikia AFCON 2027.

Alisema ana imani Stars itafanya vizuri kwa sababu Gamondi atapata muda wa kuandaa mkakati wake ambao atautumia katika maandalizi ya AFCON msimu unaokuja ili kufika mbali zaidi.

“Maandalizi ya mapema ndiyo yanahitajika kwa Stars nina imani watafanya vizuri kutokana aina ya mfumo wa mwalimu wao, Gamondi kitu kingine wachezaji wakianza kujiandaa itawapa muda wa kujipanga,” alisema.

Previous Post

KIWANGO SIMBA CHAMKERA BARKER

Next Post

WANADIPLOMASIA WATAJA FAIDA TANO ZA AMANI NCHINI

Next Post
WANADIPLOMASIA WATAJA FAIDA TANO ZA AMANI NCHINI

WANADIPLOMASIA WATAJA FAIDA TANO ZA AMANI NCHINI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MAELFU WAMSUBIRI DK. SAMIA MWANZA

MAELFU WAMSUBIRI DK. SAMIA MWANZA

3 months ago
RAIS DK. MWINYI KUSHUSHA RUNGU WATENDAJI GOIGOI

RAIS DK. MWINYI KUSHUSHA RUNGU WATENDAJI GOIGOI

2 months ago

Popular News

  • KOFANE ALIVYOANDIKA HISTORIA CAMEROON AFCON MSIMU HUU

    KOFANE ALIVYOANDIKA HISTORIA CAMEROON AFCON MSIMU HUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MIGIRO KATIBU MKUU WA  KWANZA MWANAMKE NA MIKAKATI YA KUIMARISHA MASHINA KATIKA MITAA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SAFARI KUMALIZA CHANGAMOTO UMEME IRINGA, DODOMA YAIVA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TANZANIA YAINGIA 10 BORA KUVUTIA UWEKEZAJI AFRIKA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AMREJESHA MAKONDA AFCON

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?