• ePaper
Sunday, February 1, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

URASIMU SASA BASI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 23, 2026
in Habari, Kitaifa
0
URASIMU SASA BASI
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Dodoma

NA MUSSA YUSUPH

WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba, amekemea urasimu unaofanywa na baadhi ya watumishi wa umma katika kutatua kero za wananchi kwa kisingizio cha taasisi kuandikiana barua kama sehemu ya utekelezaji wa utatuzi wa changamoto ilhali ofisi husika zipo karibu.

Kwa sababu hiyo, ameagiza kukomeshwa vitendo hivyo kwani kwa sasa ofisi zote za wizara zipo katika eneo moja na hakuna sababu ya kuchelewa kuwahudumia wananchi kwa kigezo cha kusubiri majibu ya barua.

Pia, Dk. Mwigulu ameitaka Wizara ya Madini kuongeza kasi ya utafiti kubaini maeneo yenye rasilimali madini ambazo zitatumika katika kuliletea Taifa maendeleo.

Waziri Mkuu aliyasema hayo alipokagua majengo ya Wizara ya Maji na Wizara ya Madini yaliyopo Mji wa Serikali, Mtumba jijini Dodoma.

“Tunataka kazi za serikali zifanyike makao makuu ya nchi ili kuwasogezea huduma Watanzania. Tumeendekeza sanduku la Posta mpaka ofisini, ofisi zote za serikali zipo hapa (Mji wa Serikali) linapokuja jambo linalohusu Watanzania yenye kuhitaji utatuzi, ofisi zetu zipo karibu.

“Hakuna haja kuandikiana barua, hapa mnaweza kutembea hata kwa miguu kutatua jambo husika, nimekuwa nikiona katika kikao taarifa ya utekelezaji jambo ninataarifiwa kwamba barua imeshaandikwa. Mnaandikaje wakati ofisi zinatizamana, si mkae muandike muhtasari wa kikao kama mnatafuta kumbukumbu.

Dk. Mwigulu alisisitiza: “Barua ni nusu ya kuonana, sasa si mpo hapa kwanini mnaonana nusunusu? tunapoandika barua tunamia muda mrefu, haya mambo yalikuwa zamani. Kama tunataka kumbukumbu zibaki katika nyaraka za serikali, tuandike yale mambo katika vikao ili twende kwenye utekelezaji. Hii ya kuripoti kumbukumbu ya barua kwamba ni utekelezaji ni kuchelewesha utatuzi wa kero za wananchi.”

MAJENGO YASIYOTUMIKA

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu aliagiza kuundwa timu kuchunguza majengo ya serikali ambayo hayatumiki licha ya uwepo wa baadhi ya taasisi za umma ambazo zimekuwa zikipanga hatua ambayo imekuwa ikiibebesha mzigo serikali kulipa gharama za pango.

Alisema Dodoma ndiyo Makao Makuu ya Serikali na siyo kambini ambapo alisisitiza kamwe nchi haitokuwa na makao makuu katika maeneo mawili.

“Serikali ilikuwa inaingia gharama kuweka taasisi zake katika mejengo ya kupanga, Makao makuu ya nchi ni Dodoma na tumehamia.Hapa (Dodoma) ndipo makao makuu, hii siyo kambi. Ukienda kambini unawaza kuna muda utarudi nyumbani lakini hapa ndipo makao makuu ya nchi, wala hatutakuwa na makao makuu mbili.

“Wale ambao ofisi zimeshakamilika na bado wameshikilia ofisi zingine wakati bado zipo taasisi za serikali ambazo zinapanga. Nimuagize Katibu Mkuu kuunda timu kupata orodha ya majengo yasiyotumika ili tuyagawe kwa taasisi ambazo zinapanga wakati kuna majengo ambayo hayatumiki,” alisisitiza Dk. Mwigulu.

UTEKELEZAJI DIRA 2050

Waziri Mkuu alisema dira ya maendeleo ilikuwepo tangu enzi za uongozi wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere ya kuhamishia makao makuu ya serikali mkoani Dodoma.

Alisema Serikali ya Awamu ya Tano iliyoongozwa na Hayati Dk. John Magufuli ilianza utekelezaji kwa kujenga majengo na miundombinu ya muda ili kuhamia wakati masuala mengine ya ujenzi majengo ya kudumu yakiandaliwa.

“Ilipoingia Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, majengo rasmi ya kudumu yakaanza kujengwa. Twendeni tukachapekazi kuhakikisha tunatekeleza yale ambayo yapo katika majukumu yetu.

Aliongeza: “Na sasa tunaanza utekelezaji Dira 2025 hadi 2050, kuna mambo yalikuwa yakifanyika mfano kugawana maji 50 kwa 50 mfano wananchi asilimia 50 na 50 yanapotea, natolea mfano. Lakini nilichokuwa nataka kusema ni kwamba ni kukomesha kabisa upotevu wa maji.”

“Tunapokwenda kutekeleza dira mpya tunatakiwa kwenda na ustaarabu na miundombinu inayomwakikishia Mtanzania kupata maji. Dira ya Rais Dk. Samia ambayo imeonyesha katika ilani ni kwenda kuwa na gridi ya taifa ya maji, tunatakiwa kama ilivyorasilimali zingine tujihakikishie matumizi bora na kulinda miundombinu ya maji,” alifafanua.

WIZARA YA MADINI

Akiwa katika jengo la Wizara ya Madini, alitoa wito kwa wizara hiyo kuongeza kasi ya utafiti kubaini maeneo yenye rasilimali madini.

“Dunia ya sasa ni ya rasilimali, dunia ya misaada imeshakwisha, utajiri ni rasilimali, tuendeleze utafiti ili Watanzania waweze kunufaika kupitia rasilimali zao. Usipojua una utajiri kiasi gani ni rahisi kuibiwa.

Alisisitiza: “Maandalizi ya bajeti yanaendelea, lazima kila mwaka tujiwekee lengo tunaongezaje kiwango cha utafiti kama kuwekeza rasilimali tuwekeze kwa sababu maeneo ambayo tumegundua madini huwa yanaisha. Najua tume (Tume ya Maidini) ipo kwenu, tuendelee kukomesha migogoro hasa ile yenye sura ya uonevu.”

Previous Post

KIHONGOSI ATOBOA SIRI UIMARA WA CCM

Next Post

AL AHLY, YANGA UBORA UTAONGEA

Next Post
AL AHLY, YANGA UBORA UTAONGEA

AL AHLY, YANGA UBORA UTAONGEA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

COMORO YAENDELEA KUDUMISHA USHIRIKIANO NA TANZANIA KATIKA SEKTA YA AFYA

COMORO YAENDELEA KUDUMISHA USHIRIKIANO NA TANZANIA KATIKA SEKTA YA AFYA

3 months ago

Miji ya Tanzania inaendelea kukua na miradi mpya

5 months ago

Popular News

  • MAKONDA ASISITIZA KUTOVUMILIA WAKANDARASI WAZEMBE AFCON

    MAKONDA ASISITIZA KUTOVUMILIA WAKANDARASI WAZEMBE AFCON

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NMB YAONGEZA  MAGARI MAALUMU YA HUDUMA ZA KIFEDHA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, AL AHLY MECHI YA MAAMUZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA ALIVYOIPAISHA MICHEZO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • PAPA LEO XIV APOKEA UJUMBE WA RAIS DK. SAMIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?