• ePaper
Wednesday, September 9, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

WAJUMBE WAJAWA MATUMAINI RAIS MWINYI AKIHUTUBIA BARAZA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 10, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa
0
WAJUMBE WAJAWA MATUMAINI RAIS MWINYI AKIHUTUBIA BARAZA

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi

0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na HANIFA RAMADHANI,
Zanzibar 

BAADHI ya Wajumbe wa Baraza la 11 la Wawakilishi Zanzibar (BWZ), wamesema wanatarajia kusikia hotuba yenye mikakati madhubuti na Dira ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2025/2030.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, leo anatarajiwa kulihutubia baraza hilo.

Wakizungumza na UHURU kwa nyakati tofauti, wajumbe hao, walisema hotuba za Dk. Mwinyi, mara zote huwa ni fupi, zenye uzito na kujaa mipango inayotekelezeka.

Hivyo, wanatarajia ujumbe wenye msukumo wa maendeleo na mwongozo wa awamu ya pili ya uongozi wake.

MWAKILISHI JIMBO LA KIJINI

Mwakilishi wa Jimbo la Kijini, Badria Atai Masaoud, alisema wanasubiri kwa hamu kusikia namna Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), itakavyotekeleza ilani mpya ya CCM kwa kipindi kijacho, ambayo imeweka vipaumbele 10 muhimu vilivyotangazwa na Rais Mwinyi wakati wa kampeni.

“Tunatarajia kusikia mkakati mahsusi wa namna ambavyo vipaumbele hivyo 10, vitafanyiwa kazi kwa ufanisi. 

“Rais Dk. Mwinyi, siku zote amekuwa akisisitiza utawala bora, uwajibikaji na uadilifu kwa viongozi, hivyo tunatarajia kuona msisitizo zaidi katika maeneo hayo,” alisema Badria.

Aliongeza kuwa jukumu lao kama wawakilishi ni kuhakikisha wananchi wanasimamiwa ipasavyo, wanapata huduma bora na kwamba, mipango yote ya maendeleo inayotangazwa na serikali, inatekelezwa kikamilifu.

“Sisi tupo tayari kushirikiana na Rais (Dk. Mwinyi) kwa karibu katika kuhakikisha ilani ya CCM, inatekelezwa kwa vitendo. “Wananchi wametupa dhamana, hivyo ni wajibu wetu kuwasemea na kuwasimamia katika kufanikisha malengo ya maendeleo ya nchi yetu,” alisisitiza.

MWAKILISHI JIMBO LA JANG’OMBE

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Jimbo la Jang’ombe, Ali Abdulghulam Hussein, alisema hotuba ya Rais Mwinyi, itakuwa dira ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuendeleza ahadi ambazo alizitoa wakati wa kampeni.

Alisema Dk. Mwinyi ni kiongozi mwenye maono makubwa na dhamira ya dhati ya kuwaletea wananchi maendeleo endelevu, hivyo hotuba yake, itatarajiwa kutoa mwongozo wa wazi wa kuimarisha sekta mbalimbali.

Aidha, wajumbe hao, walisema kipindi cha pili cha uongozi wa Dk. Mwinyi, kinatarajiwa kuwa cha kasi zaidi katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati, hususan inayolenga kuimarisha uchumi wa visiwa hivyo.

Previous Post

WASOMI, VIONGOZI WA DINI WAGUSIA UZALENDO, AMANI  

Next Post

UVCCM YAWAPA POLE WALIOPATA MADHILA

Next Post
UVCCM YAWAPA POLE WALIOPATA MADHILA

UVCCM YAWAPA POLE WALIOPATA MADHILA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RAIS DK. SAMIA ATOA MWELEKEO WA KITAIFA

RAIS DK. SAMIA ATOA MWELEKEO WA KITAIFA

5 months ago
WAJUE WAKALI WA MABAO AFCON 2025

WAJUE WAKALI WA MABAO AFCON 2025

8 months ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI AONYA, ATOA SIKU 60 WENYE SILAHA HARAMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NDEJEMBI MZIGONI RASMI, AKEMEA KAZI KWA MAZOEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASAUNI AANIKA UMAHIRI WA TANZANIA INAVYOLINDA UDONGO, MATUMIZI MBOLEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?