• ePaper
Saturday, November 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

UVCCM YAWAPA POLE WALIOPATA MADHILA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 10, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa
0
UVCCM YAWAPA POLE WALIOPATA MADHILA
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na REHEMA MAIGALA

UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), umetoa pole kwa madhila waliyoyapata baadhi ya Watanzania, yaliyotokea siku ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, mwaka huu, katika baadhi ya mikoa nchini, huku ukiwasihi vijana kutojiingiza katika vitendo vya machafuko.

Pia, umelaani vitendo hivyo vya uvunjifu wa amani na kuwataka vijana, wazazi na jamii, kushikamana kwa pamoja kwa sababu, amani ndiyo msingi wa maendeleo ya nchi.

Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Mohammed Kawaida, alisema hayo jijini Dar es Salaam, alipotoa tamko la umoja huo na kusema kilichotokea Oktoba 29 ni vitendo vya uvunjifu wa amani ndani ya nchi, ambavyo vilifanywa na vijana.

“Leo ni tofauti na siku nyingine, nimesimama mbele yenu waandishi wa habari siyo kwa furaha, ila ni huzuni moyoni mwangu kutokana na kile kilichofanyika Oktoba 29, ninawapa pole Watanzania wote waliofikwa na madhila hayo,” alisema.

Kawaida, alisema uchaguzi ulikuwa na matokeo mazuri ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), lakini ndani yake ulikuwa na vurugu ambazo zimeacha alama za maumivu na hasara kubwa.

“Katika hili, nina huzuni zaidi na vijana wetu ambao tunaamini ni nguzo na nguvu kazi ya taifa katika uzalishaji,” alisema.

Kawaida, alisema analaani kwa dhati vitendo hivyo, kwa sababu vinakiuka sheria na utaratibu wa jamii, pia vinahatarisha maisha ya watu wengine, yakiwemo maendeleo ya taifa kwa ujumla.

“Ninaumia zaidi kuona vurugu hizo zikirabitiwa na vijana wenzetu, ambao wengi hawapo nchini na baadhi siyo raia wa nchi yetu, tena huenda hawatarudi tena hapa nchini, huku wakiwashawishi vijana wa Kitanzania kupitia mitandao ya kijamii, huku wao wakiwa wamestarehe nchi za nje wakitunzwa na wale waliowatuma.

“Nchi yetu wanaichoma moto huku wao wakipokea malipo, bahati mbaya waliwarubuni vijana waliokuwa na nia njema, wakidhani ni kusanyiko la halali kuelezea maoni yao,  kumbe wenzetu walikuwa na nia mbaya,”alisema.

Kawaida aliwaomba wazazi na walezi, kuwakumbusha vijana kuwa uhuru wa kuandamana siyo haki ya kutoa maangamizi na kuhatarisha maisha ya watu wengine, siyo sahihi kuchoma mali ambazo zimejengwa kwa kodi za Watanzania.

“Taa za barabarani, vituo vya mabasi, vituo vya polisi, zahanati ni vituo vinavyotoa huduma kwenu wenyewe na walioshiriki vurugu, wengine walipoumia, ilitakiwa wapelekwe zahanati zilizopo jirani, lakini zilichomwa moto, hali iliyosababisha baadhi ya watu kupoteza maisha kwa sababu ya kukosa huduma ya afya mapema,”alisema.

Alisema kilichotokea anakiita ni vurugu, badala ya maandamano kwa sababu, sheria ya nchi ya maandamano ni lazima yawe na kibali, njia na muda.

ATHARI ZA VURUGU

Mwenyekiti huyo wa UVCCM, alisema kutokea kwa vurugu hizo, kulisababisha kufungwa biashara nyingi, hususan maeneo makubwa jijini Dar es Salaam, ambako masoko makubwa hayakuwahudumia Watanzania.

Alisema hali hiyo, ilisababisha hasara kwa wafanyabiashara wadogo na wakubwa na kuathiri maisha ya kila mwananchi.

“Katika hili sote ni mashahidi, kwani amri ya kukaa ndani, imetutesa wengi na kuathiri familia nyingi zenye kipato cha chini, ambazo ni asilimia kubwa ya Watanzania,” alisema.

Aliongeza vurugu hizo, zimeathiri biashara ya Kikanda kwa nchi jirani, zikiwemo Kenya, Malawi, Zambia, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Burundi na Uganda, ambao hutegemea Bandari ya Dar es Salaam kusafirisha bidhaa muhimu kama mafuta na mazao mengine.

“Vijana wenzangu, tunapofanya vurugu hapa nchini, athari zake haziishi hapa hapa Tanzania, maumivu yanasafiri hadi kwa vijana wenzetu wa nchi jirani.

“Vijana wenzangu wapendwa, mnapoamka kila asubuhi kwa vurugu za aina ile, wafikirieni wale wanaotegemea amani ambayo inawaongoza kupata chakula au mahitaji muhimu,”    alisema 

FAIDA ZA AMANI NCHINI

Kawaida, alisisitiza amani ya nchi ina nguvu kubwa kwa sababu, siyo udhaifu, bali ni nguvu ya kutoa maendeleo endelevu.

“Tushikamane na tuzungumze kwa pamoja, siyo kuwa na mitazamo ya kufanya vurugu. Amani inatufanya kushiriki pamoja katika mchakato wa kidemokrasia kupitia chaguzi na mazungumzo na siyo vurugu,” alisema.

Aidha, alisema amani ndiyo kitu pekee kinachofungua milango ya maisha bora na siyo vurugu, hivyo aliwahamasisha vijana kuendelea kuitunza amani.

PONGEZI

Kawaida alimpongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa ushindi katika Uchaguzi Mkuu na kumtakia kila la kheri katika kazi iliyo mbele yake ya kuwatumikia Watanzania.

Previous Post

WAJUMBE WAJAWA MATUMAINI RAIS MWINYI AKIHUTUBIA BARAZA

Next Post

TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

Next Post
TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WASIRA : TUSAHAU MCHAKATO WA UCHAGUZI, SASA TUUNGANE KUSAKA DOLA

WASIRA : TUSAHAU MCHAKATO WA UCHAGUZI, SASA TUUNGANE KUSAKA DOLA

3 months ago
DK. SAMIA, MWINYI WAMELETA MAENDELEO NCHINI – DK. NCHIMBI

DK. SAMIA, MWINYI WAMELETA MAENDELEO NCHINI – DK. NCHIMBI

1 month ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.