• ePaper
Sunday, November 16, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Burudani

WADAU WA SOKA WAMPONGEZA ZUNGU 

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 12, 2025
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
WADAU WA SOKA WAMPONGEZA ZUNGU 
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

AMINA KASHEBA Na NASRA KITANA

BAADA ya Mbunge wa Jimbo la Ilala, Mussa Zungu kuibuka mshindi wa kinyang’anyiro cha Kiti cha Uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano ambapo anakuwa Spika wa tisa wa Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wadau wa soka wamempongeza kwa kuibuka kidedea.

Zungu aliibuka mshindi na kutangazwa jana jijini Dodoma, kwa kupata kura 378 dhidi ya wapinzani wake Veronica Charles Tyeah wa Chama cha NFA ambaye hakupata kura, Anitha Alfan wa Chama cha NLD, aliyepata kura moja, Ndoge Said Ndonge wa AFP aliyepata kura moja na Amin Alfred Yango wa ADC ambaye hakupata kura.

Zungu ambaye ni mdau mkubwa wa soka, amekuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka 20 hadi hivi sasa, ambapo aliingia bungeni rasmi mwaka 2005 na kushika nyadhifa mbalimbali kama Mwenyekiti wa Bunge 2012-2021, Naibu Spika 2022 mpaka 2025 kabla ya jana kuwa Spika.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Meneja wa Habari na Mawasiliano Simba, Ahmed Ally alisema kuwa kama Simba wanampongeza Zungu kwa kuteuliwa kuwa Spika wa Bunge.

Alisema kuwa hiyo ni fahari kubwa kwa Simba wanajivunia kuwa na Spika wa Bunge ambaye ni mdau mkubwa wa mchezo wa soka.

“Sisi kama Simba tunampongeza Zungu kwa hatua kubwa ya kuchaguliwa kuwa Spika wa Bunge, tuna imani kuwa atafanya vyema katika majukumu yake kwani pia ni mdau mkubwa wa soka,” alisema Ahmed.

Mchezaji wa zamani Simba, Yanga na Taifa Stars,  Zamoyoni Mogella alisema ushindi wa Zungu ni fahari kwa wanamichezo kutokana na yeye kuwa mdau mkubwa wa sekta hiyo.

Alisema anampongeza Zungu kwa hatua hiyo kwani imeonyesha hata sekta ya michezo kuna watu mahiri ambao wanaweza kuongoza bunge.

“Nampongeza kwa ushindi huo kwani Zungu amekuwa mdau mkubwa wa michezo hasa ni shabiki wa Simba, hivyo kwetu wanamichezo ni furaha kwa sababu ni mwenzetu,” alisema.

Mongella alisema hiyo ni hatua kubwa ambayo amefikia Zungu ana imani atafanya vyema kazi kutokana na uzoefu aliokuwa nao.

“Mwanzo alikuwa Naibu Spika alifanya kazi vizuri na kuaminiwa, hivi sasa ni Spika wa Bunge nina imani ataendelea kufanya kazi kwa umakini na kusimamia bunge vizuri,” alisema Mongella.

Previous Post

KOCHA GAMONDI AJIVUNIA TAIFA STARS

Next Post

MWAKINYO KUPANDA ULINGONI

Next Post
MWAKINYO KUPANDA ULINGONI

MWAKINYO KUPANDA ULINGONI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WAJUMBE WAJAWA MATUMAINI RAIS MWINYI AKIHUTUBIA BARAZA

WAJUMBE WAJAWA MATUMAINI RAIS MWINYI AKIHUTUBIA BARAZA

6 days ago
DK. SAMIA AAHIDI UWANJA WA SOKA DODOMA KUKAMILIKA MWAKA 2027

DK. SAMIA AAHIDI UWANJA WA SOKA DODOMA KUKAMILIKA MWAKA 2027

3 months ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.