• ePaper
Sunday, May 10, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

MWAKINYO KUPANDA ULINGONI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 12, 2025
in Burudani, Kitaifa, Michezo
0
MWAKINYO KUPANDA ULINGONI

MWAKINYO

0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

BONDIA wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo, anatarajia kupanda ulingoni kuzichapa katika pambano la ‘Boxing on Boxing Day’, linalotarajiwa kufanyika Desemba 26, mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Kocha wa Mwakinyo, Kanda Kabongo amesema bondia wake yupo tayari kwa pambano kufuatia kufanya maandalizi ya kutosha.

Amesema anaamini Mwakinyo atafanya vyema katika pambano hilo, japokuwa bado mpinzani wake hajajulikana.

Amesema Mwakinyo alishaingia kambini kwa muda mrefu kuhakikisha anakuwa fiti kupata ushindi na kutoa burudani murua kwa mashabiki wake.

“Tulishaanza mazoezi kwa muda mrefu hivi sasa, Mwakinyo yupo tayari kwa pambano na ninaamini atafanya vyema.

“Japokuwa bado mpinzani wa Mwakinyo hajajulikana, nina imani atafanya vyema kutokana na mazoezi ninayoendelea kumpatia.

“Mwakinyo ana muda mrefu hanajapanda ulingoni, hivyo ni fursa pekee ya mashabiki kujitokeza kwa wingi kwenda kumpa sapoti bondia wao katika pambano hilo,” alisema.

Kocha huyo alisema wamefurahi kuona pambano hilo limehamishiwa Mkoa wa Dar es Salaam baada ya mwanzo kupelekwa Mwanza.

Naye bondia wa ngumi za kulipwa, Debora Mwenda alisema amepata nafasi ya kucheza katika pambano hilo atahakikisha anapambana ili kuibuka kidedea.

Alisema anahitaji kupata ushindi kuwapa furaha mashabiki zake baada ya kufanya vibaya pambano lilofanyika Julai 25, mwaka huu kufuatia kupigwa kwa pointi na mpinzani wake Asia Meshack.

Previous Post

WADAU WA SOKA WAMPONGEZA ZUNGU 

Next Post

RONALDO KUTUNDIKA DALUGA

Next Post
RONALDO KUTUNDIKA DALUGA

RONALDO KUTUNDIKA DALUGA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

ZANZIBAR YANG’ARA KIMATAIFA

ZANZIBAR YANG’ARA KIMATAIFA

5 months ago
JELA MIAKA 25 KWA KUSAFIRISHA DAWA ZA KULEVYA

JELA MIAKA 25 KWA KUSAFIRISHA DAWA ZA KULEVYA

5 months ago

Popular News

  • MTIHANI MZITO KWA MOALIN

    MTIHANI MZITO KWA MOALIN

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU ATAJA MWAROBAINI MAFURIKO DARAJA LA DUMILA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA ATIA NENO BEI MAFUTA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA MBELE KWA MBELE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WATAALAMU WAFUNGUKA MITAZAMO YA MIKATABA 8

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?