• ePaper
Thursday, April 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

RONALDO KUTUNDIKA DALUGA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 12, 2025
in Burudani, Kimataifa, Michezo
0
RONALDO KUTUNDIKA DALUGA
0
SHARES
9
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

RIYADH, Saudi Arabia

STAA Cristiano Ronaldo, amethibitisha kwamba atastaafu kucheza soka baada ya kumalizika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2026.

Mkongwe huyo raia wa Ureno mwenye umri wa miaka 40, amesema anatarajia kustaafu soka baada ya mwaka mmoja au miwili ijayo.

Msimu ujao wa michuano ya Kombe la Dunia, unatarajiwa kufanyika katika nchi za Canada, Mexico na Marekani ambapo Ronaldo utakuwa msimu wake wa sita.

Amesisitiza michuano ya Kombe la Dunia msimu ujao ndiyo itakuwa mara yake ya mwisho kushiriki, hivyo atastaafu na kuwaachia vijana kuendelea pale atakapoishia.

“Baada ya kumalizika msimu ujao wa Kombe la Dunia nitakuwa nimeshafikisha miaka 41, hivyo nitalazimika kustaafu kucheza soka.

“Michuano  ijayo ya Kombe la Dunia ninatarajia itakuwa na ushindani mkubwa, baada ya hapo nitastaafu kucheza soka na kuwaachia vijana waendelee pale nitakapoishia,” alisema.

Ronaldo anayeichezea Al-Nassr ya Ligi Kuu ya Saudi Arabia, ameshafunga mabao 143 katika timu yake ya taifa ya Ureno.

Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United, Real Madrid na Juventus alisisitiza baada ya kumalizika michuano ya Kombe la Dunia, atatundika daluga na kuendelea kufanya shughuli zingine nje ya soka.

“Acha niwe mkweli, baada ya mwaka mmoja au miwili ijayo nitalazimika kustaafu soka kwani umri wangu utakuwa umefikia hatua hiyo, lakini nitaendela kuwa karibu na mchezo huo kila muda nitakaotakiwa kutoa msaada,” alisema.

Ronaldo alishaisaidia Ureno kubeba Kombe la Euro 2016 na kutwaa mara tano tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia, Ballon d’Or.

Tayari kikosi cha Kocha Roberto Martinez, kimeshafuzu kushiriki michuano ya Kombe la Dunia msimu ujao.

Previous Post

MWAKINYO KUPANDA ULINGONI

Next Post

NYOTA TAIFA STARS  MZUKA UMEPANDA

Next Post
NYOTA TAIFA STARS  MZUKA UMEPANDA

NYOTA TAIFA STARS  MZUKA UMEPANDA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MACHO YA MASHABIKI AFCON 2025 YAPO HAPA RABAT, MOROCCO

MACHO YA MASHABIKI AFCON 2025 YAPO HAPA RABAT, MOROCCO

4 months ago
DIARRA, LOEMBA, OURA WALIVYOTIKISA DABI YA K’KOO

DIARRA, LOEMBA, OURA WALIVYOTIKISA DABI YA K’KOO

2 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?