• ePaper
Thursday, June 4, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

NYOTA TAIFA STARS  MZUKA UMEPANDA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 12, 2025
in Burudani, Kitaifa, Michezo
0
NYOTA TAIFA STARS  MZUKA UMEPANDA
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

WAKATI kikosi cha timu ya Taifa Stars kikiwa nchini Misri kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya mchezo dhidi ya Kuwait, wachezaji wa timu hiyo wameweka wazi kuwa watahakikisha wanapambana kwa jasho na damu ili kupata ushindi.

Stars inatarajiwa kushuka dimbani kumenyana na Kuwait katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki wa Kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) utakaochezwa Jumamosi ya wiki hii,  Uwanja wa Al Salam jijini Cairo nchini Misri saa 1:00 usiku.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, beki wa timu hiyo, Shomari Kapombe alisema kuwa wamejipanga vizuri kuhakikisha wanapata ushindi katika mchezo huo.

Kapombe alisema kuwa kila mchezaji yupo tayari na mchezo huo kwani kila mmoja ana morari ya kutosha kuhakikisha wanatumia vyema nafasi watakazozipata kupachika mabao.

“Tumejipanga vizuri kuelekea katika mchezo huo, tunajua ni mchezo mgumu na wenye changamoto kubwa lakini tutahakikisha tunapambana mwanzo hadi mwisho ili kupata matokeo mazuri,” alisema Kapombe.

Akimzungumzia Kaimu Kocha Mkuu, Miguel Gamondi, Kapombe alisema mabadiliko hayo hayataathiri chochote katika timu yao kwani ni kocha ambaye wanamfahamu.

Nyota huyo aliwataka mashabiki na wapenzi wa soka nchini kuendelea kuipa sapoti ya kutosha timu yao ili iweze kufanya vizuri katika mechi itakazocheza.

Naye nyota wa timu hiyo, Mohamed Hussein ‘Tshabalala’, alisema kuwa kama wachezaji wamejipanga vizuri ili kuweza kupata ushindi katika mchezo huo muhimu.

Tshabalala alisema kuwa kila mchezaji anajua jukumu lake ndiyo maana hawatakubali kuona wanapoteza mchezo huo.

Alisema kuwa mchezo huo ni moja ya maandalizi mazuri kuelekea katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON), itakayofanyika kuanzia mwezi ujao nchini Morocco.

“Kila mchezaji anajua umuhimu wa mchezo huo dhidi ya Kuwait, tumejipanga vizuri kuhakikisha tunapata ushindi katika mchezo huo muhimu, wachezaji wote wana morari ya kutosha kwa ajili ya kupambania taifa lao,” alisema Tshabalala.

Dikson Job alisema kuwa kila mchezo una umuhimu kwao, hivyo hawaangalii kama ni wa kirafiki au mashindano, mipango yao ni kupambana na kupata matokeo chanya.

“Kila mchezaji yupo tayari na amejipanga vyema kuhakikisha wanapambana ili kupata matokeo mazuri, tunaenda kupambania ushindi ili kuendelea kuipa heshima timu yetu,” alisema Job.

Kuhusu kocha mpya, Job alisema Gamondi ni kocha ambaye anamfahamu  hivyo haitakuwa ngumu kwao kufuata maelekezo ambayo atawapatia.

Previous Post

RONALDO KUTUNDIKA DALUGA

Next Post

JINA LA WAZIRI MKUU MTEULE KUWASILISHWA BUNGENI LEO

Next Post
JINA LA WAZIRI MKUU MTEULE KUWASILISHWA BUNGENI LEO

JINA LA WAZIRI MKUU MTEULE KUWASILISHWA BUNGENI LEO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SERIKALI YAIVALIA NJUGA TANZANITE

SERIKALI YAIVALIA NJUGA TANZANITE

6 months ago
DK. SAMIA AAHIDI WAKULIMA DAWA YA KUPULIZIA MIKOROSHO BILA MALIPO

DK. SAMIA AAHIDI WAKULIMA DAWA YA KUPULIZIA MIKOROSHO BILA MALIPO

8 months ago

Popular News

  • TANZANIA, RUSSIA KUPAISHA UCHUMI

    TANZANIA, RUSSIA KUPAISHA UCHUMI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ASANTE SERENGETI BOYS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?