• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

VIONGOZI WA DINI WAKEMEA MATUMIZI MABAYA MITANDAONI

admin by admin
August 26, 2025
in Habari, Kitaifa
0
VIONGOZI WA DINI WAKEMEA MATUMIZI MABAYA MITANDAONI
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ZIANA BAKARI

BAADHI ya viongozi wa dini, wasomi na wadau mbalimbali, wamewashauri vijana kutumia vyema mitandao ya kijamii, kujiajiri na kuacha kuiga utamaduni wa kigeni.

Pia, wamezisihi taasisi za kielimu, kuendelea kuwaelimisha vijana kutumia vizuri mitandao ya kijamii, huku wazazi na walezi, wakishauriwa kuwalea watoto katika maadili mema yenye hofu ya Mwenyezi Mungu.

Wakizungumza na gazeti hili jana, kwa nyakati tofauti, viongozi hao na wadau mbalimbali, walisema ni vyema mitandao ya kijamii ikatumika vizuri, siyo kuharibu maadili yaliyopo nchini.

METHODIUS KILAINI

Askofu Msaidizi mstaafu wa Jimbo Katoliki Bukoba, Methodius Kilaini, alisema siku zote, maadili yanajengwa kutokana na malezi bora kutoka kwa wazazi na walezi.

“Mtu asipokuwa na maadili ni rahisi kuiga utamaduni wa kigeni kupitia mitandao ya kijamii, hivyo, niwasihi viongozi wenzangu wa dini, kuendelea kuwafundisha watoto misingi mizuri ya dini inayotakiwa,” alisema.

SHEIKH ZAIRAY HASSAN

Sheikh wa Wilaya ya Temeke, Zairay Hassan, aliwasihi wazazi na walezi, kuwa karibu na vijana wao na kuwafundisha namna nzuri ya utumiaji wa mitandao ya kijamii.

DK. PHILIP DANINGA

Mhadhiri wa Idara ya Uongozi, Maadili na Utawala wa Chuo cha Kumbukumbu cha Mwalimu Julius Nyerere, Dk. Philip Daninga, aliwashauri vijana kutumia vyema mitandao ya kijamii kwa kujiajiri.

Alisema hivi sasa fursa zipo nyingi katika mitandao ya kijamii,  hivyo wanapaswa kuzingatia namna ya utumiaji huo unavyotakiwa.

“Natamani kuona vijana wakitumia mitandao ya kijamii muda mwingi kuangalia vitu vitakavyowasaidia kujikimu kimaisha na siyo vitakavyowapotezea muda, taasisi za kielimu ziendelee kuwaelimisha vijana namna ya utumiaji unavyotakiwa kwa kutengeneza fursa zao,”alisema.

GREYSON MWIKOLA

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi, wilayani Kigamboni, Greyson Mwikola, alisema suala la mmomonyoko wa maadili unatokana na namna ya mitandao ya kijamii inavyotumika.

Akizungumzia chimbuko la mmomonyoko wa maadili linapoanzia, alisema linatokana na utandawazi ambapo baadhi ya vijana hutumia kwa kuiga tamaduni za kigeni, ambazo siyo maadili ya taifa.

“Niishauri jamii kupenda maisha yetu halisi, tunajua simu zina mambo mengi, tunategemea kutengeneza vizazi vyenye maadili na kuja kuisimiamia vyema nchi yetu hivyo, wazazi na walezi wanapaswa kuwalea watoto katika maadili mazuri.

“Sisi kama Jumuiya kupitia CCM, wajibu wetu ni kupambana na kuhakikisha tunazungumza na vijana, watoto wetu kuwa maadili mema katika jamii,”alisema.

JANETH MAWINZA

Mkurugenzi wa Shirika la Wanawake katika Jitihada za Kimaendeleo (WAJIKI), Janeth Mawinza, alisema jamii inapaswa kuwa na hofu ya Mwenyezi Mungu ambayo itamsaidia mtu kuwa na tabia njema.

Alisema mtu yeyote akiwa na hofu ya Mwenyezi Mungu itamsaidia hata kuacha kuiga tabia zisizokuwa na maadili katika mitandao ya kijamii.

Previous Post

DK. MPANGO ATOA MAAGIZO6 MUHIMU TAASISI ZA UMMA

Next Post

VYAMA 18 Z’BAR VYASAINI FOMU KUELEKEA UCHAGUZI

Next Post
VYAMA 18 Z’BAR VYASAINI FOMU KUELEKEA UCHAGUZI

VYAMA 18 Z'BAR VYASAINI FOMU KUELEKEA UCHAGUZI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. NCHIMBI : CCM INAJIVUNIA MTAJI MKUBWA WA WANACHAMA

DK. NCHIMBI : CCM INAJIVUNIA MTAJI MKUBWA WA WANACHAMA

1 month ago
DK. NCHIMBI ATAJA VIPAUMBELE CCM 2025-2030

DK. NCHIMBI ATAJA VIPAUMBELE CCM 2025-2030

2 months ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.