• ePaper
Saturday, March 7, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 13, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH,

Geita

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, amewahakikishia wananchi kuleta maendeleo na kujenga uchumi jumuishi.

Akizungumza katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika viwanja vya Shule ya Msingi Bukombe, Dk. Samia, aliwahakikishia wananchi kwamba, atawatumikia kuleta maendeleo na kujenga taifa jumuishi.

Alisema wachimbaji wa wilaya hiyo, walikuwa wakivamia Pori la Akiba Kigosi Moyowosi, kuchimba madini ya dhahabu kwa njia isiyo rasmi.

Alieleza kuwa, rasilimali hiyo ambayo Mungu ameishusha nchini, iwanufaishe vijana na serikali, imeamua kuwamilikisha baadhi ya maeneo kuliko vijana kuendelea kuiba. 

“Kuliko wapigwe na askari wa uhifadhi, wapelekwe mahakamani, nikasema hapana. Nikamtaka Dk. Doto Biteko (Naibu Waziri Mkuu) na wenzake serikalini, waangalie namna watakavyoweza kufanya rasilimali hiyo iwafae vijana wa Bukombe.

Aliongeza: “Leo wanachimba, wanauza, tumewajengea masoko na maisha yanakwenda vizuri sana.

“Huku ndiko kujenga utu wa Mtanzania, ndiko kujenga utu wa vijana wetu. Ndiko kuwawezesha waendelee na maisha yao yawe mazuri, wapate heshima ya kutosha.”

Kwa upande wa kilimo, Dk. Samia, alisema wapo wakulima ambao kwa muda mrefu, walikuwa wakitaka kuvuna kwa kiasi kikubwa, wapate fedha za kutosha kuendesha maisha yao

Alibainisha hatua zilizochukuliwa na serikali kuwapatia ruzuku ya mbolea, dawa za kilimo kisha kuwajengea skimu za umwagiliaji walime na kuzalisha mazao kwa wingi.

Previous Post

DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

Next Post

MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

Next Post
MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WAZIRI MKUU : WATANZANIA TUNZENI AKIBA YA CHAKULA

WAZIRI MKUU : WATANZANIA TUNZENI AKIBA YA CHAKULA

3 months ago
SINGIDA BS, YANGA SC KAZI IPO LEO

SINGIDA BS, YANGA SC KAZI IPO LEO

2 days ago

Popular News

  • SALOME AIBANA KAMPUNI YA DONGFANG KWA KASI ISIYORIDHISHA MRADI WA UMEME MALAGARASI

    SALOME AIBANA KAMPUNI YA DONGFANG KWA KASI ISIYORIDHISHA MRADI WA UMEME MALAGARASI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASAUNI AZINDUA BODI YA KABONI, AIPA MAAGIZO MATANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • FCC, TCRA KUCHUNGUZA GHARAMA ZA BANDO NCHINI 

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AIPA HESHIMA DIPLOMASIA YA TANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ULINZI, USALAMA KUIMARISHWA AFCON

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?