• ePaper
Friday, November 14, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Burudani

SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 14, 2025
in Burudani, Kitaifa, Michezo
0
SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ABDUL DUNIA

WAKATI Ligi Kuu Tanzania Bara ikisimama kupisha mechi za kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2026, Simba ndiyo timu iliyofunga mabao mengi katika michuano hiyo hadi sasa msimu huu.

Katika michuano hiyo mikubwa zaidi kwa ngazi za klabu nchini, jumla ya mabao 36 yamefungwa msimu huu, huku Simba ikipachika mabao sita.

Kwa mujibu wa msimamo wa ligi hiyo, jumla ya michezo 20 imechezwa ambapo baadhi ya timu zimeingia dimbani mara mbili na nyingine mara tatu.

Katika mchanganuo wa mabao, Simba inafuatiwa na JKT Tanzania na Dodoma Jiji zilizofunga mabao manne kila moja.

Yanga na Azam FC zimepachika mabao matatu kila moja zikifuatiwa na Singida Black Stars, Mashujaa, Namungo, Mtibwa Sugar, Coastal Union na Tabora United zilizopachika mabao mawili.

Timu zilizofunga bao moja ni Mbeya City, Tanzania Prisons, KMC na Pamba Jiji.

Hata hivyo ni Fountain Gate pekee ambayo hadi sasa haijapachika bao lolote katika mitanange mitatu iliyocheza msimu huu.

Akizungumza kwa njia ya simu, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally alisema kikosi chao kimedhamiria kufanya vyema zaidi msimu huu.

“Sisi ni timu kubwa na tunahitaji mambo makubwa, huu ni mwanzo tu na Wanasimba wanapaswa kujua kwamba tuna timu ya kutoka kifua mbele kufanya makubwa katika kila mechi,” alisema.

Previous Post

JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

Next Post

DK. NCHIMBI AELEZA MKAKATI WA RELI SGR HADI KIGOMA

Next Post
DK. NCHIMBI AELEZA MKAKATI WA RELI SGR HADI KIGOMA

DK. NCHIMBI AELEZA MKAKATI WA RELI SGR HADI KIGOMA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

‘WALIPENI WAKULIMA, WAFANYAKAZI’

‘WALIPENI WAKULIMA, WAFANYAKAZI’

2 months ago
VIONGOZI WA DINI WAKEMEA MATUMIZI MABAYA MITANDAONI

VIONGOZI WA DINI WAKEMEA MATUMIZI MABAYA MITANDAONI

3 months ago

Popular News

  • NYOTA TAIFA STARS  MZUKA UMEPANDA

    NYOTA TAIFA STARS  MZUKA UMEPANDA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RONALDO KUTUNDIKA DALUGA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JINA LA WAZIRI MKUU MTEULE KUWASILISHWA BUNGENI LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWAKINYO KUPANDA ULINGONI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WADAU WA SOKA WAMPONGEZA ZUNGU 

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.