• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 14, 2025
in Burudani, Kitaifa, Michezo
0
SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ABDUL DUNIA

WAKATI Ligi Kuu Tanzania Bara ikisimama kupisha mechi za kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2026, Simba ndiyo timu iliyofunga mabao mengi katika michuano hiyo hadi sasa msimu huu.

Katika michuano hiyo mikubwa zaidi kwa ngazi za klabu nchini, jumla ya mabao 36 yamefungwa msimu huu, huku Simba ikipachika mabao sita.

Kwa mujibu wa msimamo wa ligi hiyo, jumla ya michezo 20 imechezwa ambapo baadhi ya timu zimeingia dimbani mara mbili na nyingine mara tatu.

Katika mchanganuo wa mabao, Simba inafuatiwa na JKT Tanzania na Dodoma Jiji zilizofunga mabao manne kila moja.

Yanga na Azam FC zimepachika mabao matatu kila moja zikifuatiwa na Singida Black Stars, Mashujaa, Namungo, Mtibwa Sugar, Coastal Union na Tabora United zilizopachika mabao mawili.

Timu zilizofunga bao moja ni Mbeya City, Tanzania Prisons, KMC na Pamba Jiji.

Hata hivyo ni Fountain Gate pekee ambayo hadi sasa haijapachika bao lolote katika mitanange mitatu iliyocheza msimu huu.

Akizungumza kwa njia ya simu, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally alisema kikosi chao kimedhamiria kufanya vyema zaidi msimu huu.

“Sisi ni timu kubwa na tunahitaji mambo makubwa, huu ni mwanzo tu na Wanasimba wanapaswa kujua kwamba tuna timu ya kutoka kifua mbele kufanya makubwa katika kila mechi,” alisema.

Previous Post

JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

Next Post

DK. NCHIMBI AELEZA MKAKATI WA RELI SGR HADI KIGOMA

Next Post
DK. NCHIMBI AELEZA MKAKATI WA RELI SGR HADI KIGOMA

DK. NCHIMBI AELEZA MKAKATI WA RELI SGR HADI KIGOMA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RAIS DK. SAMIA ATUMA UJUMBE WA AMANI

RAIS DK. SAMIA ATUMA UJUMBE WA AMANI

4 months ago
KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TABORA, UZALISHAJI WAANZA RASMI

KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TABORA, UZALISHAJI WAANZA RASMI

1 month ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?