• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Burudani

LIVERPOOL, ARSENAL KAZI IPO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
August 31, 2025
in Burudani, Kimataifa, Michezo
0
LIVERPOOL, ARSENAL KAZI IPO
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

LONDON, England

TIMU za soka za Liverpool na Arsenal, leo zinatarajiwa kupambana katika mchezo wa Ligi Kuu ya England.

Pambano hilo, limepangwa kufanyika katika Uwanja wa Anfield ambapo Liverpool itakuwa mwenyeji wa mchezo huo.

Hadi leo, Arsenal inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi sita baada ya kushuka dimbani mara mbili katika michuano hiyo.

Liverpool katika ligi hiyo, ipo nafasi ya tatu katika msimamo huo, ikiwa na pointi zake sita baada ya kucheza mechi mbili tangu msimu huu wa 2025/26 ulipoanza hivi karibuni.

Katika msimamo huo, timu ya Tottenham ipo nafasi ya pili ikiwa na alama sita baada ya kushuka dimbani mara mbili katika ligi hiyo yenye ushindani mkubwa.

Hata hivyo, baadhi ya mechi ambazo Liverpool imecheza imeonesha udhaifu  katika safu ya ulinzi licha ya kupachika mabao saba katika mechi zao mbili za kwanza katika ligi.

Katika pambano la leo kati ya Liverpool na Arsenal, macho ya mashabiki yatakuwa kwa

 Eberechi Eze.

Timu ya Arsenal ipo katika hali tete ya kuwakosa Kai Havertz ambaye amefanyiwa upasuaji wa goti.

Pia, kocha wa Arsenal, Arteta yupo katika muda mgumu kufuatia Bukayo Saka na Martin Odegaard kuwa na majereha huenda wasiwepo katika mchezo dhidi ya Liverpool.

Viktor Gyokeres anastahili kupata nafasi nyingine ya kuanza mchezo huo dhidi ya Liverpol huku Jeremie Frimpong, atakosa pambano hilo la leo.

Mechi nyingine zitakazo fanyika leo ni Brighton & Hove Albion itapambana na Manchester City, Nottingham Forest  itacheza na West Ham.

Pambano jingine litakuwa kati ya timu za Aston  Villa dhidi ya Crystal Palace.

Liverpool huenda ikawakilishwa na Alisson, Bradley, Konate, Van Dijk, Kerkez, Szoboszlai, Gravenberch, Salah, Wirtz, Gakpo na Ekitike.

Arsenal: Raya, Timber, Saliba, Gabriel, Calafiori, Eze, Zubimendi, Rice, Madueke, Gyokeres na  Martinelli.

Previous Post

DK. MWINYI ACHUKUA FOMU ZANZIBAR, AHADHARISHA CHUKI

Next Post

KIBAIGWA IMEFUNIKA, OKTOBA WANATIKI KWA DK. SAMIA

Next Post
KIBAIGWA IMEFUNIKA, OKTOBA WANATIKI KWA DK. SAMIA

KIBAIGWA IMEFUNIKA, OKTOBA WANATIKI KWA DK. SAMIA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WITO WA DK. NCHIMBI KWA VIONGOZI WA DINI

WITO WA DK. NCHIMBI KWA VIONGOZI WA DINI

2 days ago
ARAJIGA, KAYOKO HAOO CAFCL

ARAJIGA, KAYOKO HAOO CAFCL

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.