• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

SERIKALI YAIPA TANO YANGA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 17, 2025
in Habari, Kitaifa, Michezo
0
SERIKALI YAIPA TANO YANGA
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na VICTOR MKUMBO

SERIKALI imeipongeza klabu ya Yanga kwa kutwaa ubingwa wa Ngao ya Jamii msimu huu, baada ya kuifunga Simba kwa bao 1-0, katika mchezo uliofanyika, Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam.

Bao pekee lililoipa Yanga ubingwa katika mchezo huo liliwekwa kimiani dakika ya 55 na staa wake Pacome Zouzoua baada ya kupiga shuti lililojaa wavuni moja kwa moja.

Akizungumza baada ya mchezo huo, Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa, amesema anaipongeza Yanga kutokana na kuonyesha kiwango bora na kuibuka na ushindi katika mchezo huo.

Hata hivyo timu zote zilionyesha ushindani wa aina yake kutokana na kufanya usajili bora msimu huu.

Waziri Mchengerwa amesema hiyo yote imetokana na serikali kuendelea kutoa mchango mkubwa katika sekta ya michezo na kuhakikisha Tanzania inakuwa moja ya nchi zenye ligi bora.

Amesema kuwa ameshashuhudia mechi zilizozikutanisha Simba na Yanga kwa nyakati tofauti, lakini mchezo wa juzi wachezaji wote walionyesha kiwango cha hali ya juu.

Amesisitiza katika mchezo huo wachezaji walionyesha kiwango kizuri na kutoa burudani kwa mashabiki zao tofauti na wengi walivyotarajia.

Amesema katika fainali lazima mshindi apatikane, hivyo anaamini Simba watakwenda kujipanga upya kuhakikisha wanarudi kivingine msimu ujao.

“Ninawapongeza Yanga kwa kubeba taji la mchezo wa Ngao ya Jamii msimu huu kwani walionyesha kiwango cha hali ya juu.

“Hii imetokana na serikali kuendelea kuwekeza katika sekta ya michezo kuhakikisha mchezo wa soka unakuwa moja ya ajira kwa vijana.

“Timu zote zilionyesha kiwango bora na kila mmoja alionyesha jitihada, hivyo ninaamini Simba watakwenda kujipanga na kurudi kivingine katika mechi zinazo,” alisema Mchengerwa.

Huo ulikuwa mchezo wa 11 kwa timu hizo kukutana katika Ngao ya Jamii, huku ukiwa mchezo wa 21 tangu kuanza kwa kombe hilo mwaka 2021.

‎Yanga inakuwa timu ya kwanza kuweka rekodi ya kushinda mara sita taji hilo na kujiwekea rekodi ya kushinda mara nyingi zaidi ya mpinzani wake kwani michezo 10 iliyopita kila timu ilishinda mara tano.

‎Yanga waliifunga Simba mabao 2-1 (2001), mikwaju ya penalti 3-1 (2010), bao 1-0 (2021), mabao 2-1 (2022) na bao 1-0 msimu uliopita kabla ya juzi kushinda bao 1-0.

Simba ilishinda mechi zake za Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga mabao 4-1 (2002), ikiifunga mabao 2-0 (2005), 2-0 (2011), mikwaju ya penalti 5-4 (2017), kabla ya kushinda tena kwa mikwaju ya penalti 3-1 (2023) mechi pekee iliyofanyika Uwanja wa Mkwakwani, jijini Tanga.  

Previous Post

KISHINDO CHA DK. SAMIA MIKOA 10

Next Post

SIMBA, YANGA AKILI ZOTE KIMATAIFA

Next Post
SIMBA, YANGA AKILI ZOTE KIMATAIFA

SIMBA, YANGA AKILI ZOTE KIMATAIFA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA ATANGAZA HATUA ZA MWISHO UTEKELEZAJI MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

DK. SAMIA ATANGAZA HATUA ZA MWISHO UTEKELEZAJI MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

2 weeks ago
DK. SAMIA ASEMA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VIPO TAYARI KULINDA NCHI WAKATI WA UCHAGUZI MKUU

DK. SAMIA ASEMA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VIPO TAYARI KULINDA NCHI WAKATI WA UCHAGUZI MKUU

4 weeks ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.