• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Burudani

SIMBA, YANGA AKILI ZOTE KIMATAIFA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 17, 2025
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
SIMBA, YANGA AKILI ZOTE KIMATAIFA
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

WAKATI timu za Simba na Yanga zikiondoka nchini jana, viongozi wa timu hizo wameweka wazi kuwa akili zao zote ni katika mechi za kimataifa ili waweze kupata ushindi na kurudi na pointi tatu muhimu.

Yanga imeondoka kwenda Angola kwa ajili ya mchezo wake wa raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL), dhidi ya Wiliete ya nchini humo, mchezo utakaochezwa Septemba 19, mwaka huu Uwanja wa 11 de Novembro.

Hata hivyo, Simba pia wameondoka kwenda Botswana kwa mchezo wa CAFCL dhidi ya Gaborone United utakaopigwa Septemba 20, katika Uwanja wa Obed Itani Chilume.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti viongozi wa klabu ya Simba na Yanga walisema kuwa akili zote kwa hivi sasa wameziamishia katika mechi za kimataifa.

Meneja wa Habari na Mawasiliano Simba, Ahmed Ally alisema kuwa wametoka kupoteza dhidi ya Yanga lakini ana imani kubwa na kikosi chao kinaenda kufanya vizuri na kufika mbali katika michuano ya kimataifa.

Alisema kuwa anajua mchezo utakuwa mgumu na wenye changamoto nyingi lakini watapambana kuhakikisha hawapotezi.

“Tumeelekea nchini Botswana kwa ajili ya mchezo wetu dhidi ya Goborone United, hautakuwa mchezo rahisi kwetu lakini tutapambana kwa kila namna ili tuweze kupata matokeo,” alisema Ahmed.

Ahmed alisema kuwa matokeo ambayo wameyapata dhidi ya Yanga wameachana nayo na hivi sasa akili na mawazo yao yote ni kuelekea katika mchezo wa kimataifa.

Ofisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe alisema kuwa wamejipanga vizuri kuhakikisha wanakwenda kupata ushindi japokuwa na kurejea nyumbani na pointi tatu.

Kamwe alisema kuwa anajua hautakuwa mchezo mwepesi kwao lakini hawatakubali kupoteza kwani lengo lao ni kuona wanashinda katika kila mchezo watakaocheza.

“Tumetoka kupata ushindi dhidi ya Simba hii ni kubwa kwetu na ni mwanzo mzuri kuelekea katika mechi yetu ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika, kikubwa tunahitaji ushindi ambao ni muhimu,” alisema Kamwe.

Ofisa Habari huyo aliwataka mashabiki na wapenzi wa timu yao kutokuwa na hofu kwani wanakwenda kupambana kuhakikisha wanaibuka na ushindi.


Katika hatua nyingine, Singida Black Stars nayo iliondoka nchini jana kwenda  Rwanda katika mchezo wa Kombe la Shirikisho (CAFCC), dhidi ya Rayon Sports huku Azam FC ikiwa nchini Sudan Kusini kuivaa Al Merreikh katika mchezo wa kwanza wa raundi ya awali ya michuano hiyo mechi zote zikichezwa Septemba 20, mwaka huu.

Previous Post

SERIKALI YAIPA TANO YANGA

Next Post

DK. SAMIA ASEMA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VIPO TAYARI KULINDA NCHI WAKATI WA UCHAGUZI MKUU

Next Post
DK. SAMIA ASEMA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VIPO TAYARI KULINDA NCHI WAKATI WA UCHAGUZI MKUU

DK. SAMIA ASEMA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VIPO TAYARI KULINDA NCHI WAKATI WA UCHAGUZI MKUU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WASIRA ATABIRI RUNDO LA KURA KWA DK. SAMIA

WASIRA ATABIRI RUNDO LA KURA KWA DK. SAMIA

1 month ago
DK. SAMIA AACHA GUMZO SONGEA AKIAHIDI NEEMA TELE

DK. SAMIA AACHA GUMZO SONGEA AKIAHIDI NEEMA TELE

3 weeks ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.