• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

DK. MIGIRO ATAJA SABABU ZITAKAZOMPA USHINDI DK. SAMIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 19, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. MIGIRO ATAJA SABABU ZITAKAZOMPA USHINDI DK. SAMIA

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Asha-Rose Migiro

0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Asha-Rose Migiro, amesema mafanikio yaliyopatikana kupitia filamu ya Tanzania The Royal Tour chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ni miongoni mwa sababu zitakazomwezesha  mgombea huyo kupata ushindi wa kishindo.

Dk. Migiro alieleza hayo, alipozungumza katika mkutano wa kampeni wa CCM, uliofanyika Uwanja wa Hamburu, Jimbo la Nungwi, Mkoa wa Kaskazini Unguja, ambao Mgombea urais kupitia CCM, Dk. Samia alihutubia maelfu ya wananchi.

Alisisitiza mafanikio ya filamu hiyo, yameongeza thamani ya utalii, kuimarisha uchumi na kuonesha wazi dira ya maendeleo ya viongozi hao.

“Katika kazi nyingi walizofanya, hatuwezi kusahau mchango mkubwa wa Rais Dk. Samia katika kuandaa filamu ya Tanzania The Royal Tour. Ilikuwa kielelezo cha kuipeleka Tanzania kiuchumi na leo tumeona matokeo yake,” alisema Dk. Migiro.

Aliongeza Zanzibar imenufaika zaidi kupitia filamu hiyo, kwani ni kisiwa chenye utajiri wa viungo, manukato na vivutio vya kipekee vinavyoongeza mvuto wa kitalii duniani.

“Ulipokuwa waziri wakati wa Rais Karume, ulitangaza vema Zanzibar na sasa uzoefu huo umetumika katika  Royal Tour. Mwinyi ameendeleza misingi hiyo na utalii leo ni injini ya uchumi wa kisasa,” alisema.

Aliongeza wagombea wa CCM, Dk. Samia na Mwinyi wanatekeleza kwa vitendo kauli mbiu ya ‘Kazi na Utu’, ambapo wameweka msisitizo kupitia uwekezaji wa rasilimali watu, elimu, afya na maji.

“Dk. Samia ameonesha kwa dhati anataka kuitimiza kaulimbiu ya Kazi na Utu. Tumeona jitihada katika kupunguza vifo vya mama na mtoto, elimu, maji na afya. Haya ni mafanikio yasiyopingika,” alisema.

Dk. Migiro alimpongeza Dk. Mwinyi kwa kuimarisha miundombinu, akitolea mfano ujenzi wa barabara na miradi mbalimbali.

Alisema wananchi wameanza kumuita ‘Hussein Mabati’ kutokana na mabati mengi yanayozungushiwa katika maeneo ambayo miradi ya maendeleo inatekelezwa.

“Ujenzi wa kisasa unaendelea. Zanzibar inaelekea kuwa na uchumi wa kisasa. Tuna kila sababu ya kuwaunga mkono wagombea hawa,”  alisisitiza.

Previous Post

DK. SAMIA AAHIDI FURSA ZAIDI KWA VIJANA NCHINI

Next Post

DK. SAMIA ANAVYOTAFSIRI ‘KAZI NA UTU’ KWA VITENDO

Next Post
DK. SAMIA ANAVYOTAFSIRI ‘KAZI NA UTU’ KWA VITENDO

DK. SAMIA ANAVYOTAFSIRI 'KAZI NA UTU' KWA VITENDO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SERIKALI IMEIMARISHA BARABARA – DK. SAMIA

SERIKALI IMEIMARISHA BARABARA – DK. SAMIA

1 month ago
KAHAWA YA TANZANIA KUONGEZEWA THAMANI KABLA YA KUPELEKWA NJE

KAHAWA YA TANZANIA KUONGEZEWA THAMANI KABLA YA KUPELEKWA NJE

3 weeks ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.