• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

DK. SAMIA KUFANYA MKUTANO MKUBWA WA KAMPENI ZA CCM GOMBANI YA KALE

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 19, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. SAMIA KUFANYA MKUTANO MKUBWA WA KAMPENI ZA CCM GOMBANI YA KALE

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH,

Pemba

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kutikisa kisiwani Pemba kwa kufanya mkutano mkubwa wa kampeni katika viwanja vya Gombani ya Kale.

Mkutano huo, utakaofanyika Septemba 20, 2025, maelfu ya wakazi wa kisiwa hicho, watapata fursa kusikiliza ahadi mbalimbali zitakazotolewa na mgombea huyo wa Urais.
Tayari mitaa mbalimbali ya Pemba, imepambwa kwa bendera za CCM huku mabango yenye picha za Dk. Samia zikipendezesha maeneo mbalimbali zikiwemo barabara mashuhuri kisiwani hapa.

Wakizungumza kuhusu mkutano huo baadhi ya wananchi wameeleza matarajio yao kwa Dk. Samia ambapo mfanyabiashara wa Chakechake, Ali Masoud Mzee, alisema anatarajia Dk. Samia atatoa msisitizo zaidi kukifungua kisiwa hicho kiuchumi.

“Pemba kwa sasa imeanza kufunguka, lakini kwetu wafanyabiashara tunaamini fursa zaidi zikifunguka ndipo mzunguko wa fedha utaongezeka,” alieleza.

Naye, Kombo Issa Kombo, alimpongeza Rais Dk. Samia kwa kuendelea kuimarisha ulinzi na usalama katika kisiwa hicho.

“Amani imetawala siyo kama kipindi cha zamani wakati wa uchaguzi hali inachafuka, lakini sasa kampeni zinafanyika kwa ustaarabu na ulinzi umeimarishwa,” alisisitiza.

Pemba ni miongoni mwa maeneo yaliyonufaika kupitia miradi mbalimbali yenye lengo la kuboresha maisha na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi.

Miongoni mwa miradi hiyo ni kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia iliyozinduliwa kisiwani hapa Mei tano mwaka huu na kuwanufaisha wananchi kwa kupata huduma za kisheria.

Vilevile, kisiwa hicho kimenufaika kupitia mradi wa hifadhi ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi ambao unatekelezwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SJMT).

Wilaya za Pemba zilizonufaika kupitia mradi huo ni Wete na Micheweni ambao umejikita kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula kwa gharama ya sh. bilioni 1.2.

Kadhalika, kisiwa hicho kinaendelea kunufaika na fedha zitolewazo na wadau wa maendeleo kupitia SJMT ambapo baadhi ya miradi hiyo ni ujenzi wa barabara ya Chakechake hadi Wete kupitia kwa Binti Abeid na ujenzi wa shule, hospitali na masoko.

Pia, Serikali ya Dk. Samia kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) imeendelea kutekeleza mradi wa kuboresha mawasiliano katika baadhi ya vijiji. Miongoni mwa vijiji vilivyonufaika ni Kojani, Kinyikani, Kidundo na Wete mjini vilivyopo Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Kwa upande wa nishati, serikali ipo katika mpango wa kuimarisha njia zinazosafirisha umeme kwa njia ya bahari kwa lengo la kuongeza kiwango cha upatikanaji nishati hiyo Unguja na Pemba.

Kazi hiyo inafanywa kwa ushirikiano baina ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) ambapo njia ya umeme inayotoka Tanga hadi eneo la Wesha kisiwani Pemba itaimarishwa.

Juzi, Dk. Samia alihitimisha mikutano yake ya kampeni mjini Unguja kwa kuhutubia maelfu ya wananchi waliofurika katika uwanja wa Hamburu, Jimbo la Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Katika mkutano huo, Dk. Samia alisema Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi ndiye mgombea sahihi atakayeshirikiana naye kuleta maendeleo kwa manufaa ya pande mbili za muungano.

Alisisitiza kuwa matokea ya ukuaji uchumi na utekelezaji ahadi za CCM kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita, umeonekana dhahiri uwezo wa kiongozi huyo katika kuwaongoza Wazanzibar.

“Pamoja na majanga yote tuliyopitia ikiwemo Covid, tumeweza kufanyakazi kubwa pamoja katika sera za kifedha na uchumi na ndiyo maana hatukuweza kukwamisha miradi yetu.

“Kwenye sera za kifedha na sera za kiuchumi, Dk. Hussein ameweza kusimamia na kuimarisha uchumi ambao kwa sasa unakuwa kwa kasi kubwa,” alisisitiza.

Rais Dk. Samia alibainisha kuwa ukuaji uchumi kwa Tanzania bara umeongezeka kwa asilimia sita huku Zanzibar ukiwa juu zaidi kwa asilimia 7.1 kwa mwaka.

“Zaidi uchumi umekuwa hata mifukoni kwa kila mwananchi. Wakati nilipokuwa nikiwasili Nungwi nilikuwa nikitazama kila pande na kujionea namna ambavyo kumejengeka nyumba nzuri za makazi, biashara zinafanyika na mambo yanaenda vyema kwa amani na utulivu,” alisisitiza.

Previous Post

WASIRI : CCM INAFANYA KAZI KUBWA YA KULETA MAENDELEO

Next Post

KISHINDO CHA DK. NCHIMBI RUVUMA

Next Post
KISHINDO CHA DK. NCHIMBI RUVUMA

KISHINDO CHA DK. NCHIMBI RUVUMA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. NCHIMBI AMTAJA DK. SAMIA UJENZI BANDARI YA KWALA

DK. NCHIMBI AMTAJA DK. SAMIA UJENZI BANDARI YA KWALA

4 days ago
KAMPENI YA DK. SAMIA YAACHA GUMZO TABORA

KAMPENI YA DK. SAMIA YAACHA GUMZO TABORA

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.