• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Burudani

SIRI YA SIMBA YAVUJA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 21, 2025
in Burudani, Michezo
0
SIRI YA SIMBA YAVUJA
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

PAMOJA na kupata ushindi katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL), uongozi wa Simba umetoboa siri kwamba mechi ilikuwa ngumu kutokana na uzuri wa wapinzani wao.

Juzi, Simba ilishinda bao 1-0 dhidi ya Gaborone United katika mchezo uliofanyika nchini Botswana.

Akizungumza kupitia ukurasa wa mtandao wa klabu hiyo, Meneja wa Habari na  Mawasiliano, Ahmed Ally alisema wapinzani wao wana timu nzuri na hawapaswi kubezwa.

“Tunayo furaha kubwa kupata ushindi tulitegemea tutapata upinzani na tulifahamu katika mechi za awali lazima tutakutana na timu zenye ushindani.

“Lakini Elie Mpanzu alipambana na kuhakikisha tunapata ushindi ugenini, tulipoteza nafasi nyingi za kufunga mabao katika mchezo wetu, laskini tunashukuru tumepata pointi tatu,” alisema Ally.

Meneja huyo alifafanua kuwa mechi ya marudiano wana kazi kubwa ya kuzuia na kupambana kupata matokeo mazuri.

“Mechi ya marudiano tuna kazi mkubwa,lakini tutahakikisha tunapambana kupata matokeo mazuri ambayo yatatusaidia kusonga mbele,” alisema meneja huyo Ally.

Hata hivyo, Meneja huyo alisema wamepokea taarifa kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) katika mchezo huo wa marudiano dhidi ya Gaborone United, Simba hairuhusiwi kuingiza mashabiki kutokana na adhabu walipewa.

“Tumefanya mazungumzo na CAF kwa kukata rufaa, hivyo tunasubiri majibu ya rufaa hiyo kama hiyo mechi inaruhusiwa kuwepo kwa mashabiki au hawaruhuwi hivi sasa hatupo katika nafasi nzuri ya kuzungumza, ” alisema Ally.

Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, James Bwana alisema klabu ya Simba imeonesha hatua mkubwa na utulivu katika mchezo wao dhidi ya Gaborone United.

“Simba imeonesha hatua kubwa, imeonesha mchezo mzuri, nawapongeza Watanzania waliojitokeza kwenda kuiunga mkono timu hiyo hadi imepata ushindi wa bao 1-0,” alisema.

Simba inatarajiwa kushuka dimbani Septemba 28, mwaka huu katika mchezo wa marudiano dhidi ya Gaborone United utaopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Previous Post

‘GOLI LA MAMA’ LAIPA MORALI YANGA

Next Post

DK. NCHIMBI : TUTAJENGA BARABARA WILAYANI LUDEWA

Next Post
DK. NCHIMBI : TUTAJENGA BARABARA WILAYANI LUDEWA

DK. NCHIMBI : TUTAJENGA BARABARA WILAYANI LUDEWA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MPINA APIGWA ‘STOP’ URAIS ACT-WAZALENDO

MPINA APIGWA ‘STOP’ URAIS ACT-WAZALENDO

2 months ago
DK. SAMIA AAHIDI NEEMA MPYA KWA WAKULIMA

DK. SAMIA AAHIDI NEEMA MPYA KWA WAKULIMA

2 months ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.