• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

DK. MWINYI : YAJAYO YANAFURAHISHA KASKAZINI UNGUJA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 22, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. MWINYI : YAJAYO YANAFURAHISHA KASKAZINI UNGUJA
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na HANIFA RAMADHANI,

Zanzibar

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema kukamilika miradi mikubwa ya kimataifa katika Mkoa wa Kaskazini Unguja, kutaufanya mkoa huo kutokuwa na tofauti na Mkoa wa Mjini.

Amesema hivi karibuni kutaanza ujenzi wa bandari kubwa ya kisasa ya kimataifa katika eneo la Mangapwani na ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Nungwi, eneo la Kigunda.

Dk. Mwinyi aliyasema hayo katika mkutano wa kampeni katika uwanja wa Shangani, Mkokotoni, Mkoa wa Kaskazini Unguja.

“Baada ya bandari ya Mangapwani na uwanja wa ndege Nungwi kukamilika, huu Mkoa wa Kaskazini Unguja hautakuwa na tofauti yoyote na mikoa ya mjini kwa maendeleo na jinsi utakavyofunguka,” alisema.

Alisema miradi hiyo ya kimataifa ambayo itaufanya Mkoa wa Kaskazini Unguja, kufunguka katika kila sekta kwa sababu kutakuwa na milango mikuu ya kuingia na kutoka katika visiwa vya Zanzibar.

Alisema serikali imejipanga kujenga barabara zote za Mkoa wa Kaskazini Unguja ikiwemo ya Mkwajuni hadi Matemwe, Mkwajuni-Kijini na Kinyasini-Kiwengwa.

Alisema lengo ni kuhakikisha kunakuwa na muunganiko baina ya mkoa mmoja kwenda mwingine.

“Mambo yatakuwa mazuri sana katika kipindi kinachokuja, tutahakikisha tunamaliza tuliyoanza pamoja na kuanza miradi mingine mipya,” alisema Dk. Mwinyi.

Alisema serikali imeimarisha huduma za kijamii za ujenzi wa skuli, hospitali za wilaya na mkoa ambazo zimeanza kujengwa eneo la Mahonda.

Alisema serikali imedhamiria kuanza mradi mkubwa wa upatikanaji wa maji safi na salama katika mkoa wa Kaskazini ambako hivi karibuni mradi huo unatarajiwa kuanza.

DK. DIMWA

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dk. Mohammed Said Mohammed ‘Dimwa’, alisema Dk. Mwinyi ni kiongozi mtulivu, mnyenyekevu na madhubuti.

Alisema mgombea huyo ni miongoni mwa viongozi wachache waliobeba hekima na busara za wazee na mtu mwenye kufanya uamuzi sahihi.

Alisema katika kipindi cha m afya na miundombinu ya barabara, amefanya mambo makubwa, hivyo aliwaomba wananchi kumpigia kura nyingi sana Dk. Mwinyi aendeleze safari ya maendeleo.

Mgombea uwakilishi wa jimbo la Kijini, Badria Atai Masoud, alisema majiaka mitano Dk. Mwinyi hakutumia muda wake kujibu maneno ya mitaani, bali aliweka misingi madhubuti ya kuwaletea maendeleo wananchi wa Zanzibar.

Alisema katika elimu,imbo yote ya Kaskazini wanatiki kwa CCM sababu wananchi hawana chama mbadala.

Naye, Mgombea ubunge wa jimbo la Donge, Sadifa Juma Khamis, alisema Dk. Mwinyi amefanya mambo makubwa katika jimbo hilo ambalo wananchi wameahidi kumpigia kura nyingi Oktoba 29.

DK.SAADA MKUYA 

Kwa upande wake, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Dk. Saada Mkuya Salum, aliwaomba wana-Kaskazini kuacha kusikiliza upotoshaji unaofanywa na badhi ya wanasiasa wanaotaka umaarufu wakati hawana sera.

Alisema Serikali ya Awamu ya Nane imefanya maendeleo makubwa kwa wananchi wa Zanzibar, hasa ujenzi wa barabara mjini na vijijini za kiwango cha lami.

Previous Post

DK. SAMIA AACHA GUMZO SONGEA AKIAHIDI NEEMA TELE

Next Post

DK. SAMIA : TUNATAKA USHINDI WA HESHIMA

Next Post
DK. SAMIA : TUNATAKA USHINDI WA HESHIMA

DK. SAMIA : TUNATAKA USHINDI WA HESHIMA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA, BALOZI NCHIMBI WAAHIDIWA KURA ZA KISHINDO

DK. SAMIA, BALOZI NCHIMBI WAAHIDIWA KURA ZA KISHINDO

2 months ago
DK. SAMIA  AELEZA MAFANIKIO YA UONGOZI WAKE

DK. SAMIA AELEZA MAFANIKIO YA UONGOZI WAKE

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.