• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

MTWARA KUCHELE! NCHIMBI AAHIDI MAMBO MAKUBWA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 2, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
MTWARA KUCHELE! NCHIMBI AAHIDI MAMBO MAKUBWA

MGOMBEA Mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi

0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NJUMAI NGOTA,

Mtwara

MGOMBEA Mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, amesema katika kipindi cha miaka mitano ijayo, iwapo watapata ridhaa ya kuongoza nchi, wamedhamiria kujenga meli mpya ya mizigo itakayorahisisha usafirishaji bidhaa kutoka Mtwara kwenda Comoro.

Dk. Nchimbi, amesema hayo kwa nyakati tofauti, alipohutubia wananchi katika mikutano ya hadhara ya kampeni za Chama kuelekea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu, majimbo ya Mtwara Vijijini na Nanyamba, mkoani Mtwara.

Amesema lengo la kujenga meli hiyo ni kuinua uchumi wa wakulima na wafanyabiashara, kuhakikisha bidhaa zao zinapata masoko ya kimataifa kwa gharama nafuu na faida kubwa.

“Hakuna sababu ya wakulima wa Mtwara kukosa soko la bidhaa wakati tupo karibu na Comoro.
“Meli hii ya mizigo, itavusha bidhaa kwa urahisi na tutakuwa na uhakika wa bei nzuri kwa wakulima wetu. Huu ndiyo uchumi wa bahari tunaotaka kuuimarisha,” alisema.

Amesema katika miaka mitano ijayo, CCM imedhamiria kuanzisha mradi mkubwa wa kuchukua maji kutoka Mto Ruvuma na kuyasambaza maeneo ya Mtwara Vijijini, Nanyamba na Tandahimba.

“Mto Ruvuma ni mkubwa, bado wananchi wetu wanapata tabu ya maji. Hatutakubali hali hii iendelee. Tunatekeleza miradi mikubwa ya maji, kila mtu apate huduma hii muhimu bila shida,” amesema.

Akizungumzia sekta ya nishati, Dk. Nchimbi amesema serikali ijayo ya CCM, ina mpango wa kusimamia ujenzi wa bomba la gesi la kilometa 34 kutoka Ntorya hadi Madimba, kuhakikisha wananchi wanapata gesi ya uhakika kwa matumizi ya nyumbani na kibiashara.

MTWARA VIJIJINI

Akiwa Nanguruwe, Dk. Nchimbi, alisema katika kuhakikisha maendeleo ya sekta ya usafiri wa anga, Serikali ya CCM, imedhamiria kupanua Kiwanja cha Ndege cha Mtwara kwa kuongeza majengo ya abiria, mnara wa kuongozea taa na eneo la Zimamoto.

“Ilimradi hadhi ya uwanja wa ndege ionekane na kuongeza usafirishaji wa watu na bidhaa zetu,”alisema.

AFYA

Alisema CCM katika Jimbo la Mtwara Vijijini, wamekusudia kujenga vituo vya afya vitano na zahanati 12, kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya karibu na makazi yao.

ELIMU

Pia, alisema CCM imedhamiria kuinua kiwango cha elimu kwa kujenga sekondari nne na shule za msingi tano ndani ya jimbo hilo.
Alisema hatua hiyo, inalenga kuhakikisha watoto wanapata elimu bora katika mazingira rafiki, yanayowezesha kujifunza kwa ufanisi.

BARABARA

Akielezea mpango wa CCM katika miundombinu, Dk. Nchimbi alisema barabara kadhaa muhimu zitatengenezwa kwa kiwango cha lami na kukarabatiwa kurahisisha usafirishaji wa bidhaa na watu.

Alizitaja baadhi ya barabara hizo na kilometa zikiwa katika mabano ni Nanguruwe – Masasi (160), Mtwara – Mingoyo (201), Madimba – Msimbati (35) na  Mbuyuni – Newala (42).

NANYAMBA

Akiwa Nanyamba, Dk. Nchimbi, alisema wamekusudia kujenga shule mbili za msingi, sekondari tatu na kuongeza madarasa katika shule zilizopo, kwa lengo la kuhakikisha watoto wote wanapata fursa ya kusoma katika mazingira bora na ya kisasa.

Pia, alisema CCM imedhamiria kujenga barabara mbalimbali kwa kiwango cha lami na changarawe, zikiwemo za  Nanyamba – Mkodolo na Mahakama Road – Nanguruwe – Mkulwa yenye urefu wa kilometa 1.8.

TANDAHIMBA

Akiwa katika mkutano wa hadhara wa kampeni Viwanja vya Kassim Majaliwa, alisema wamekusudia kujenga vituo vya afya viwili na zahanati  12, huku Hospitali ya Wilaya ya Tandahimba, ikiendelea kuboreshwa kwa kuongeza vifaatiba na miundombinu ya kisasa.

Kuhusu elimu, alisema CCM itajenga shule za msingi nne na sekondari mbili huku shule za zamani zikijengwa madarasa mapya 185.
Alisema katika miaka mitano ijayo, wanakusudia kujenga maabara 10 kwa masomo ya sayansi.

Aidha, wanakusudia kujenga baadhi ya barabara kwa kiwango cha lami na changarawe ikiwemo ya Mtama – Newala (74), hatua itakayorahisisha usafiri wa mazao, watu na bidhaa katika maeneo ya Tandahimba na maeneo jirani.

Kuhusu sekta ya biashara, Dk. Nchimbi alisema imepewa kipaumbele kwa kujengwa stendi ya kisasa, soko la kisasa huku wakiendelea kushirikiana na Bodi ya Korosho kwa kuhakikisha bei ya zao hilo inaendelea kuwa nzuri.

Dk. Nchimbi akiwa katika mikutano hiyo, alimwombea kura Mgombea Urais wa Chama, Dk. Samia Suluhu Hassan, wabunge na madiwani wote wa CCM.

Previous Post

DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA BARABARA ZA NDANI KWA KIWANGO CHA LAMI PANGAWE

Next Post

DK. SAMIA ASEMA MIAKA MITANO IJAYO, SERIKALI ITAENDELEA KUIMARISHA MASLAHI YAO

Next Post
DK. SAMIA ASEMA MIAKA MITANO IJAYO, SERIKALI ITAENDELEA KUIMARISHA MASLAHI YAO

DK. SAMIA ASEMA MIAKA MITANO IJAYO, SERIKALI ITAENDELEA KUIMARISHA MASLAHI YAO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan

MAELFU WAZIDI KUMIMINIKA KUMSIKILIZA MGOMBEA URAIS WA CCM DK. SAMIA

2 months ago
TANZANIA IMEJIPANGA – DK. MIGIRO

TANZANIA IMEJIPANGA – DK. MIGIRO

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.