• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

DK. NCHIMBI AGUSIA HISTORIA MPYA ILIYOANDIKWA NA DK. SAMIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 8, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. NCHIMBI AGUSIA HISTORIA MPYA ILIYOANDIKWA NA DK. SAMIA

MGOMBEA Mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Emmanuel Nchimbi

0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NJUMAI NGOTA,

Tabora

MGOMBEA Mwenza wa Urais kupitia Chama  Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Emmanuel Nchimbi, amesema Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, ameandika historia mpya ya uongozi kwa kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo na huduma kwa wananchi kwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa.

Dk. Nchimbi, aliyasema hayo katika Uwanja wa Mpira wa Kigwa, wilayani Igalula, mkoani Tabora, alipohutubia mamia ya wananchi, waliojitokeza katika mkutano wa hadhara wa kampeni za CCM, kuelekea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu.

“Katika kipindi cha miaka minne na nusu ya uongozi wake, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, amefanya kazi nyingi katika miradi ya maendeleo na huduma kwa kiwango ambacho hakijapata kutokea katika nchi yetu,” alisema.

Alisema mafanikio hayo makubwa, yameleta faraja na fahari kwa kila Mtanzania, hasa wanachama wa CCM ambao, hivi sasa wanatembea kifua mbele kwa sababu ya kazi nzuri ya Rais Dk. Samia.

“Ndiyo maana leo, tunakwenda kifua mbele tukijivunia kazi alizofanya Rais wetu.

“Kila kiongozi aliyesimama hapa, ameieleza kwa fahari kazi iliyofanyika.

“Kila kiongozi wa CCM na kila mwanachama wetu, anakwenda popote kwa kujiamini,”alisema.

Dk. Nchimbi, alibainisha kuwa, hivi sasa CCM ina wanachama milioni 13.5, wote wakiwa na imani kubwa na uongozi wa Dk. Samia, ambaye amejenga heshima ya serikali na Chama.

Aliwahimiza wananchi wa Igalula, kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura Oktoba 29, mwaka huu na kuhakikisha wanamchagua Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, wagombea wa ubunge na udiwani.

Mgombea Mwenza wa Urais, Dk. Nchimbi juzi alihitimisha mikutano yake ya hadhara ya kampeni mkoani Tabora.

KUTIKISA ZANZIBAR

Dk. Nchimbi, leo anatarajiwa kufanya mikutano ya hadhara ya kampeni za Chama eneo la Kinyasini- Wete, Kaskazini Pemba kisha kwenda kuzuru kaburi la Hayati Mohamed Seif Khatib.

Pia, mkutano mwingine, unatarajiwa kufanyika katika Jimbo la Chwaka lililopo Kusini Unguja.

Previous Post

DK. SAMIA KUISUKA MWANZA YA KIMATAIFA

Next Post

NEEMA YAJA WAKULIMA WA MIKARAFUU ZANZIBAR

Next Post
NEEMA YAJA WAKULIMA WA MIKARAFUU ZANZIBAR

NEEMA YAJA WAKULIMA WA MIKARAFUU ZANZIBAR

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. NCHIMBI : TUTAJENGA BARABARA WILAYANI LUDEWA

DK. NCHIMBI : TUTAJENGA BARABARA WILAYANI LUDEWA

3 weeks ago
WITO WA DK. NCHIMBI KWA VIONGOZI WA DINI

WITO WA DK. NCHIMBI KWA VIONGOZI WA DINI

2 days ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.