• ePaper
Sunday, November 16, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

WASIRA AHIMIZA KILA MMOJA KUPIGA KURA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 23, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
WASIRA AHIMIZA KILA MMOJA KUPIGA KURA

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira

0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na SULEIMAN JONGO,

Geita

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, ametoa maelekezo kwa viongozi wa Chama kuanzia ngazi ya shina, kuhakikisha wananchi wanatoka nyumba kwenda kupiga kura Oktoba 29, mwaka huu, siku ya kumchagua Rais, Wabunge na Madiwani.

Amesisitiza kuwa, msukumo zaidi uwekwe katika maeneo ambayo wagombea waliosimamishwa na Chama, wamekosa wapinzani wa kuchuana nao kwa kuwa, huko wanaCCM wajisahau kwa kudhani wamepita bila kupigiwa kura.

Wasira alitoa maelekezo hayo, alipozungumza na viongozi wa CCM Wilaya ya Geita, jana, akiwa katika mwendelezo wa kumnadi na kumwombea kura Mgombea Urais kupitia CCM, Dk. Samia Suluhu Hassan na wagombea ubunge na udiwani, wanaopeperusha bendera ya Chama.

“Mamlaka ya nchi yapo mikononi mwa watu, tungependa watu wengi sana wapige kura na kwa sababu ya mazingira ya uchaguzi wa mwaka huu, kwa mfano, ukija hapa mjini (Geita), yupo ndugu yangu Waja (Mgombea Ubunge Jimbo la Geita Mjini), hana mpinzani, sasa katika mazingira hayo, watu wanaweza kudhani Waja ameshapita kumbe bado.

“Kwa hiyo, twende kwa wanachama, twende kwa wananchi, mabalozi ndiyo nguvu ya chama chetu na chama chetu ni chama cha wanachama na wanachama, wanaongozwa kuanzia nyumba kumi kumi.

“Tunawaomba wakuu wa mashina siku ya kupiga kura, muwatambue wapigakura wote, siyo wanachama tu, wapigakura wote washaurini tu hata wanaotukataa waende (kupiga kura) ili na zao zihesabiwe.

“Wanaosema hapana, waende wakapige kura na wanaosema ndiyo nao waende, halafu tuhesabu (kura) watashika kichwa, waseme hatukujua kama mambo yangekuwa hivi,” alisema.

Wasira alisisitiza kuwa, kila kiongozi anapaswa kuhakikisha wananchi wanapiga kura kuanzia ngazi ya nyumba kumi.

Alieleza kuwa, wananchi wakipiga kura, dunia itafahamu kwamba, uchaguzi umefanyika Tanzania na Watanzania wamepiga kura.

Pia, aliwasisitiza viongozi kuhakikisha Watanzania hawanunui woga wanaouziwa na mitandao ya kijamii.

“Kataa kununua woga, nenda upige kura nchi iko salama na dola ya CCM iko pale, hakuna mtu yeyote atakayechezea chochote,” alisisitiza.

Previous Post

CCM YAJIVUNIA KAMPENI ZA KISTAARABU – DK MWINYI

Next Post

SIMBA, YANGA  ZAITA MASHABIKI

Next Post
SIMBA, YANGA  ZAITA MASHABIKI

SIMBA, YANGA  ZAITA MASHABIKI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

NCHIMBI : NIDHAMU NGUZO KUIMARISHA DEMOKRASIA

NCHIMBI : NIDHAMU NGUZO KUIMARISHA DEMOKRASIA

2 months ago
SIMBA, YANGA  ZAITA MASHABIKI

SIMBA, YANGA  ZAITA MASHABIKI

3 weeks ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.