• ePaper
Wednesday, September 9, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

SIMBA, YANGA  ZAITA MASHABIKI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 23, 2025
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
SIMBA, YANGA  ZAITA MASHABIKI
0
SHARES
11
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

WACHEZAJI wa timu za Simba na Yanga, wamewaomba mashabiki wake kujitokeza kwa wingi katika Uwanja wa Benjamini Mkapa, Dar es Salaam kuwapa sapoti katika mechi za marudiano katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL).

Katika ratiba ya hatua ya pili ya mtoano ya CAFCL, Yanga itachuana na Silver Striker ya Malawi kesho wakati Simba ikishuka dimbani dhidi ya Nsingizini Hotspurs ya Eswatini keshokutwa.

Yanga itaingia katika mtanange huo ikiwa na kumbukumbu ya kichapo cha bao 1-0 ilichokipata Malawi wakati Simba ikipata ushindi wa mabao 3-0 nchini Eswatini.

Nyota wa Simba, Jonathan Sowah, alisema bado hawajamaliza kazi hivyo mashabiki na wapenzi wa Simba wanatakiwa kujaa kwa wingi uwanjani kuwapa sapoti ya kutosha.

Sowah alisema anajua utakuwa mchezo mgumu lakini wachezaji watapambana kuhakikisha wanatimiza malengo ya timu.

 “Tunakwenda kukamilisha mchezo wetu wa marudiano na lengo kubwa ni kuhakikisha tunapata ushindi hivyo tunawaomba mashabiki na wapenzi wa Simba kujaa kwa wingi uwanjani watupe sapoti ya kutosha na kutuongezea morali ya ushindi,” alisema Sowah.

Beki wa Wekundu hao wa Msimbazi, Shomari Kapombe, alisema ushindi walioupata ugenini umewaongezea morali ya kutosha katika mchezo wa marudiano lakini bila ya mashabiki wao itakuwa ni ngumu kufanya vizuri.

 “Tunawaomba mashabiki wetu wajae kwa wingi uwanjani watupe sapoti ya kutosha kwani bila wao sisi si kitu, umoja na mshikamano wao kwetu utatuongezea nguvu ya kufanya vizuri zaidi,” alisema Kapombe.

Mlinzi wa Yanga, Ibrahim Bacca alisema mashabiki na wapenzi wa timu yao wanatakiwa kuingia kwa wingi uwanjani kuwapa sapoti ya kutosha watinge makundi.

“Jamani mchezo wetu ni bure hivyo niwaombe mashabiki wa Yanga kuhakikisha wanakuja kwa wingi uwanjani kuipa sapoti ya kutosha timu na kutuongezea morali tutinge hatua ya makundi,” alisema Bacca.

Naye nahodha wa timu hiyo, Dikson Job, alisema huo ni mchezo muhimu kwao kuhakikisha wanapata ushindi hivyo mashabiki wana mchango mkubwa katika mchezo huo.

“Uzuri mchezo wetu ni bure, mashabiki na wapenzi wa timu yetu wanatakiwa kujaa kwa wingi uwanjani ili waweze kutupa sapoti ya kutosha kwani sapoti yao nduo itatuongezea morari kubwa ya kupata ushindi,” alisema Job.

Previous Post

WASIRA AHIMIZA KILA MMOJA KUPIGA KURA

Next Post

DK. SAMIA AHIMIZA UPIGAJI KURA OKTOBA 29

Next Post
DK. SAMIA AHIMIZA UPIGAJI KURA OKTOBA 29

DK. SAMIA AHIMIZA UPIGAJI KURA OKTOBA 29

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MAAGIZO YA RAIS SAMIA, KARIAKOO YATEKELEZWA 95%

MAAGIZO YA RAIS SAMIA, KARIAKOO YATEKELEZWA 95%

7 months ago
WANASIASA WAELEZA IMANI YAO TUME YA JAJI CHANDE

WANASIASA WAELEZA IMANI YAO TUME YA JAJI CHANDE

5 months ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI AONYA, ATOA SIKU 60 WENYE SILAHA HARAMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NDEJEMBI MZIGONI RASMI, AKEMEA KAZI KWA MAZOEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASAUNI AANIKA UMAHIRI WA TANZANIA INAVYOLINDA UDONGO, MATUMIZI MBOLEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?