• ePaper
Monday, June 8, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

CCM YAJIVUNIA KAMPENI ZA KISTAARABU – DK MWINYI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 23, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
CCM YAJIVUNIA KAMPENI ZA KISTAARABU – DK MWINYI

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi

0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na HANIFA RAMADHANI,

Pemba

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema CCM inajivunia kwa kufanya kampeni za kistaarabu, kisayansi na kuyafikia makundi yote ya wananchi Unguja na Pemba.

Amesema CCM, inatarajia ushindi wa kishindo kutokana na namna ilivyofanya kampeni zake na kunadi sera nzuri na hamasa kubwa waliyoipata kwa wananchi katika kila mkutano.

Dk. Mwinyi, aliyasema hayo, akifunga kampeni zake za Urais katika Kisiwa cha Pemba huko Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Alisema wamefanya kampeni za kistaarabu na wameweza kunadi sera kwa kuyafikia makundi yote Unguja na Pemba.

Alisema wakati CCM inanadi sera zake, vyama vingine visivyokuwa na sera, vilikuwa vikihubiri matusi na kejeli kila vikipanda majukwaani.

“Wazanzibari hawataki kusikia hayo, hawataki kusikia matusi wala kejeli, wanachotaka wao ni kusikia nini tutafanya katika kipindi cha miaka mitano ijayo,” alisema.

Alisema Chama Cha Mapinduzi, kimefanya mikutano mingi ya hadhara ya makundi yote Unguja na Pemba.

Pia, alisema Chama kilijinadi kwa kuyasema yake ambayo kimeyafanya katika kipindi cha miaka mitano iliyopita na kueleza nini kitafanya kipindi kijacho.

Alisisitiza kuwa, Oktoba 29 ni siku ambayo wananchi wataamua hatma ya nchi na kuwataka wasibweteke, kwani ndiyo siku ya maamuzi.

Vilevile, aliwataka wananchi kuichagua CCM kwa lengo la kulinda tunu za kitaifa kama vile Mapinduzi na Muungano.

DK. DIMWA

Naye, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dk. Mohammed Said Mohammed ‘Dimwa’, alisema CCM ilifanya kampeni zake kwa ustaarabu mkubwa na kwamba, kampeni zilikuwa za kitaalamu bila ya kumbughudhi mtu.

Previous Post

DK. SAMIA AFUNDA VIJANA

Next Post

WASIRA AHIMIZA KILA MMOJA KUPIGA KURA

Next Post
WASIRA AHIMIZA KILA MMOJA KUPIGA KURA

WASIRA AHIMIZA KILA MMOJA KUPIGA KURA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SPIKA ZUNGU : NITAZINGATIA HAKI, UWAZI

SPIKA ZUNGU : NITAZINGATIA HAKI, UWAZI

7 months ago
CCM YAONESHA KUKUBALIKA, MAELFU WAMIMINIKA

CCM YAONESHA KUKUBALIKA, MAELFU WAMIMINIKA

9 months ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA ZATOA MSIMAMO LIGI KUU BARA

    YANGA, SIMBA ZATOA MSIMAMO LIGI KUU BARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WFP KUENDELEZA USHIRIKIANO NA TANZANIA USIMAMIZI WA MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • HESHIMA KUBWA KWA TANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU: MAMBO MAZURI YANAKUJA, AIPA TANO SERENGETI BOYS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?