• ePaper
Sunday, November 16, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

MBETO : RAIS DK. SAMIA, MWINYI WAMEAPA KULINDA WATANZANIA NA AMANI YA TAIFA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 6, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa
0
MBETO : RAIS DK. SAMIA, MWINYI WAMEAPA KULINDA WATANZANIA NA AMANI YA TAIFA

KATIBU wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM, Zanzibar, Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Khamis Mbeto Khamis

0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na Mwandishi Wetu,
Zanzibar

KATIBU wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM, Zanzibar, Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Khamis Mbeto Khamis, amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, na Rais wa Zanzibar ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, wamekula kiapo cha kuwalinda Watanzania kwa mujibu wa Katiba, hivyo wananchi hawapaswi kuyumbishwa na wachochezi wa uvunjifu wa amani kutoka ndani au nje ya nchi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo (6 Novemba 2025) katika Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui, Mbeto amesema viongozi hao wanatekeleza wajibu wao wa kikatiba wa kuwalinda wananchi na kulinda utu wao dhidi ya watu wasiolitakia mema Taifa.

“Viongozi wetu wanatekeleza takwa la kikatiba. Wananchi wanapaswa kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa amani, hasa wakati huu ambapo hatua zaidi zinaendelea kuchukuliwa dhidi ya waliopanga na kuchochea vurugu za Oktoba 29, 2025,” amesema Mbeto.

Amesisitiza kuwa amani ni tunu ya Taifa, hivyo kila Mtanzania ana wajibu wa kuilinda, na kwamba nchi haitashurutishwa na mtu, kikundi, au taifa la kigeni katika utekelezaji wa mambo yake ya ndani.

Mbeto amewaasa hasa vijana kukataa kutumika kuvuruga amani na kusababisha uharibifu wa mali, akisema ikipotea, amani ni vigumu kuirudisha.

Aidha, ametumia nafasi hiyo kuwapongeza Rais Dkt. Samia na Rais Dkt. Mwinyi kwa ushindi wa kishindo walioupata katika Uchaguzi Mkuu uliopita, akisema matokeo hayo yanaonyesha imani kubwa ya Watanzania kwa viongozi hao.

Katika uchaguzi huo, mgombea wa CCM kwa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dk. Samia Suluhu Hassan, alipata zaidi ya asilimia 97 ya kura, huku mgombea wa CCM kwa nafasi ya Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, akiibuka na ushindi wa asilimia 74.08.

Previous Post

LATRA KUTOA VIBALI KWA WAENDESHA DALADALA KUPITA NJIA YA MWENDOKASI BRT (I)

Next Post

COMORO YAENDELEA KUDUMISHA USHIRIKIANO NA TANZANIA KATIKA SEKTA YA AFYA

Next Post
COMORO YAENDELEA KUDUMISHA USHIRIKIANO NA TANZANIA KATIKA SEKTA YA AFYA

COMORO YAENDELEA KUDUMISHA USHIRIKIANO NA TANZANIA KATIKA SEKTA YA AFYA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA AACHA SIMULIZI RUFIJI

DK. SAMIA AACHA SIMULIZI RUFIJI

4 weeks ago
MATOKEO YA DARASA LA SABA YATANGAZWA

MATOKEO YA DARASA LA SABA YATANGAZWA

1 week ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.